Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-02-06

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aaah
Yaani niue albino ndio niwe tajiri, aaah hapana sitaki kuwa kwenye orodha ya wauaji, kama ni umaskini acha niwe, hata kama watu watasema nimeporomoka sawa tu,” alijisemea Kazim. [1]
aende
Kuna baadhi na wataalam kule alikokwenda kuhangaika walimshauri labda aende nje ya nchi. [2]
agizo
Baadhi ya shule zilizokuwa na madarasa kwa ajili ya mafunzo ya awali katika jiji la Mwanza zinatekeleza agizo la serikali, lakini zimebuni utaratibu mpya kwa lengo la kuendelea kuipatia fedha. [3]
aina
MWANAISHA Yahaya, mkazi wa jijini Dar es Salaam ambaye alimpaka mwanae wa kike gundi aina ya superglue sehemu za siri, jana alifikishwa mbele ya hakimu mkazi wa wilaya ya Kinondoni akikabiliwa na tuhuma za kusababisha majeraha mwilini. [4]
ajabu
Migomo na maandamano ya ajabu ajabu inatukera sana, na hii ni changamoto nyingine kubwa katika kufikia lengo la kuboresha elimu yetu. [5]
akawa
Kweli walifanya hivyo, wiki moja baadaye walirudi, Kazim akawa amekubali kwamba angependa kufanya biashara zote mbili yaani ya uvuvi na uchimbaji madini. [6]
albino
WAPO watu wanaosema kwamba machozi aliyomwaga bungeni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Alhamisi wiki hii wakati akielezea mauaji ya albino nchini yalikuwa ni machozi ya mamba. [7]
alidai
Mgaya alidai shahidi wa 18 (Pw 18) Dk. [8]
ama
Kuhusu Zombe, Mgaya alidai kuna ushahidi wa mazingira unaomuunganisha katika tukio hilo ikiwa ni pamoja na maelezo ya mshtakiwa wa 11 kuwa aliwafundisha namna ya kujieleza wakiitwa mahali popote, hali inayoonyesha kuwa alihusika kwa namna moja ama nyingine katika mauaji hayo. [9]
amani
Alidai kwa kusema: “Upande wa mashtaka umetumia maelezo yao mbele ya timu ya polisi iliyowahoji na mbele ya mlinzi wa amani, hata hivyo upande huo umeshindwa kuthibitisha iwapo watuhumiwa walikiri kuhusika na kosa ingawa wameeleza kuwa walifika msitu wa Pande na kushuhudia mauaji yakitendeka. [10]
ambako
Kwanza taasisi hiyo imejipambanua kwa kuwa na ofisi au makao yake Tabata, Dar es Salaam ambako pia kuna kituo cha kulelea watoto yatima na waishio katika mazingira magumu. [11]
ambaye
Aliieleza mahakama kuwa Pw 24, ambaye alikuwa mkuu wa Kituo cha Polisi Chuo Kikuu, SSP Sebastian Masinde aliwatambua washtakiwa wa nne, wa sita, wa saba, wa nane na wa 13, ambao wote walitoka kituoni hapo. [12]
ana
Kwa hivyo ana shauri la kujibu aeleze ni nani aliyeamuru mauaji hayo,” alisema Kaishozi. [13]
anasema
Waziri Mkuu wa Bunge hilo lililoshirikisha vijana kutoka vyuo na shule mbalimbali za Dar es Salaam, Christopher Mdoe anasema, kuingia kwa siasa katika sekta ya elimu kumechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa ubora wa elimu nchini na akaiomba serikali na wanasiasa kuacha mchezo wa kuingiza siasa shuleni. [14]
angalau
Ndio maana naipongeza serikali ya awamu ya nne ya kutambua umuhimu wa kuongeza kiwango cha elimu ili angalau Watanzania wengi wakahitimu kidato cha nne. [15]
angalia
Hebu angalia kadi za wenyewe. [16]
asasi
Wazazi, asasi na mashirika kadhaa yamekuwa mstari wa mbele kuyasemea haya mara kwa mara. [17]
au
Hata hivyo, katika majibu yake ya hoja hizo jana, upande wa mashtaka uliieleza mahakama kuwa kwa ushahidi uliotolewa washtakiwa wote wana kesi ya kujibu na wakijitetea au wakinyamaza kimya mahakama itawatia hatiani. [18]
aweze
Baada ya kusoma kifungu hicho, Hakimu Nyasige alimuuliza tena mchungaji huyo kama alikuwa tayari kuapa ili aweze kuendelea na kutoa ushahidi wake mahakamani, hata hivyo mtumishi huyo wa Mungu aliendeleza msimamo wake wa kukataa kuapa. [19]
bado
Tanzania, na haitakuwa kwa JKT au Jeshi au timu nyingine, bado nasema ni Tanzania," alisema Bhanji. [20]
bila
Naye mwendesha mashtaka wa serikali, Angaza Mwipopo, akijibu hoja ya Wakili Rongino Myovela kuwa kitendo cha mshtakiwa wa 8 na 13 kurudisha silaha zao bila kutumika kinaonyesha hawakuhusika katika mauaji, aliileza mahakama kuwa kitendo cha kuficha ukweli ni dhahiri kuwa nao walikuwa na nia mbaya na walihusika. [21]
binafsi
Hiyo ni tofauti kati ya shule za binafsi anayosoma Emmy na za serikali anakosoma Kayumba. [22]
budi
Hata hivyo, alieleza kuwa jamii haina budi kutambua kwamba,  hivyo ni visingizio na wala havina faida yeyote kwao zaidi ya kuleta athari kwa afya zao na kuwataka kubadilika. [23]
cha
Mtukufu Jaji, sasa tunataka kuionyesha mahakama kuwa ushahidi uliotolewa hapa mahakamani umekidhi matakwa ya kifungu cha sheria namba 293 (1) sura ya 20 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai,” alisema Wakili Mgaya. [24]
chozi
Chukua mfano wa huyu aliyedondosha chozi juzi. [25]
desturi
Hayo yalielezwa jana na Katibu msaidizi wa Kamati ya mila na desturi ya mkoa wa Tanga (TIAC), Nestory Ngwega katika mdahalo  juu ya mila na desturi uliyoendeshwa jana na Kamati hiyo kwa wanafunzi wa Sekondari ya Mkwakwani ya Jijini hapa. [26]
dhidi
Hayo yalisemwa jana na Kamishna msaidizi wa idara ya ustawi wa jamii katika wizara ya afya na ustawi wa jamii Donald Chawe katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na  ofisa ustawi wa jamii mkuu katika idara hiyo Jeanne  Ndyetabura wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili  yanayohusu  mapambano dhidi ya biashara hiyo hapa nchini. [27]
dira
Vijana mnatakiwa kuwa na dira kwa sababu serikali ina dira yake, wizara zina dira zake na mashirika yana dira zao. [28]
es
Zombe, aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoani Dar es Salaam, RCO, na kaimu kamanda wa polisi, ARPC, wakati wa mauaji hayo ya wafanyabiashara wanne wa wilayani Mahenge mkoani Morogoro na dereva mmoja wa teksi wa Manzese jijini Dar es salaam, ndiye mtuhumiwa namba moja kwenye kesi hiyo inayosikilizwa Mahakama Kuu. [29]
faini
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi mjini hapa, imewahukumu vijana watano wa kiume wakazi wa kijiji cha Uhamaka manispaa ya Singida faini ya Sh250,000 baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la kukaidi kushiriki mafunzo ya mgambo. [30]
gani
Kujua vinasaba gani vinasaidia mbu kukabiliana na dawa za kuwaua kunaweza kusaidia kutengeneza dawa nzuri zaidi ambazo ni salama kwa binadamu pia, alisema Charles Wondji wa Taasisi ya Dawa za Nchi za Joto ya Liverpool akiwa na wenzake. [31]
hadi
Angepaswa kuelewa kiunagaubaga kuwa nini kilichowafika hao waliodaiwa majambazi hadi wakauawa. [32]
haja
Kuhusu hoja ya kutokuwa na gwaride la kuwatambua washtakiwa iliyotolewa na wakili Majura Magafu, Mgaya alidai hapakuwa na haja kwa sababu washtakiwa waliweza kutambuliwa na mashahidi mbalimbali. [33]
hajui
Katika ushahidi, PW36 hajui ni kwa nini DCI aliamua washtakiwe wachache kwani walikuwa ni wengi. [34]
hakimu
Kitendo hicho kilifanya hakimu huyo kumsomea kifungu cha sheria na 198 (1) kama ilivyorekebishwa mwaka 2002 kinachokataza mtu kudharau mahakama na kumwambia kuwa kuendelea kukataa kuapa ni kuvunja sheria na hivyo anatenda kosa la jinai. [35]
hana
Katika kuishawishi mahakama kuwa Zombe hana kesi ya kujibu Msemwa aliieleza mahakama hiyo kuwa baada ya mauaji hayo kutokea, timu mbili za uchunguzi pamoja na Tume ya Rais iliyokuwa chini ya Jaji Musa Kipenka, ziliundwa ambazo kwa pamoja zilimuona Zombe kuwa hana hatia. [36]
hasa
Baada ya Jaji Masati kutangaza kuahirisha kesi hiyo hadi Jumatatu kwa ajili ya uamuzi washitakiwa walisikika wakiwasisitiza ndugu zao wasikose kufika siku hiyo, lakini baadhi ya ndugu wa washtakiwa hao walionekana kukosa raha ghafla hasa baada ya upande wa mashtaka kumaliza kujibu hoja na kusisitiza kuwa washtakiwa wana kesi ya kujibu. [37]
hasira
Minziro ambaye juzi alikuwa na hasira baada ya mwamuzi, Oden Mbaga kukataa bao lililofungwa na Kudra Omari kwa madai alikuwa ameotea, alisema atahakikisha anautumia muda huo kikamilifu ili timu yake iweze kufanya vizuri kwa mechi zake zilizobaki. [38]
hata
Hatukatai kuwa hakuwapo katika eneo la mauaji lakini kwa nafasi yake wakati huo alikuwa akielewa matukio yote yaliyokuwa yakiendelea jijini, hivyo hata hili alikuwa “aware” nalo. [39]
hatua
Pamoja na ushauri wa Waziri Mkuu kwamba, waafugaji wanatakiwa kuwa na mifugo michache kulingana na rasilimali za malisho zilizopo ili kuondoa migogo kati yao na wakulima, kwa kuwa hali imekuwa hivyo, tofauti na hatua iliyochukuliwa ya kukamata mifugo yao, serikali inatakiwa kuwasaidia kwa kuwahamishia mahali pengi, kama ilivyofanya kwa waliokuwa katika Bonde la Ihefu, wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya ambao walihamishiwa Pwani na mikoa ya Kusini. [40]
hawa
Katika mashahidi hawa wote hakuna hata mmoja aliyeweza kumuunganisha Zombe na mauaji hayo ama akiwa ofisini au katika eneo la mauaji. [41]
hawezi
Whoops, chama tawala!' Ilibidi nipeleke hii barua kwa waishiwa wenzangu maana mimi binafsi nilikuwa nimefurahia sana kuona kiongozi anayeguswa kutokana na kuona wahanga wa ukatili kiasi kwamba hawezi kuhimili mihemko. [42]
hii
Alisema tatizo la usafirishaji  na biashara  ya bianadamu hapa Tanzania kwa sasa  linaendelea kukua kwa kasi zaidi hatua mbayo mwaka jana 2008 serikali kupitia bunge  ilipitisha sheria kali ya kudhibiti hali hii. [43]
hili
Alidai maelezo ya mshitakiwa wa 11 kuwafundisha kupindisha ukweli katika kujieleza popote walipotakiwa kufanya hivyo akiahidi kuwapandisha vyeo na mengineyo yakiunganishwa yanamhusisha Zombe na tukio hili. [44]
hivi
Ndiyo maana wakitumia mwavuli wa Bunge Kivuli la Vijana ambalo lilifanyika hivi karibuni Dar es Salaam wanafunzi nao walijadili nafasi, wajibu na fursa ya kila kijana kushiriki katika uboreshwaji wa elimu nchini. [45]
hizi
Maana, jamani, hizi kadi za biashara ni kama ibada ya dini. [46]
hospitali
Alihangahaika kwenye hospitali nyingi bila mafanikio. [47]
huko
Na kwa bahati mbaya huko ambako tunaagiza maarifa haya, wanazalisha mapya kila siku kiasi kwamba kama hatufanyi warsha na semina tutafika mahali tutapitwa na tutaaachwa mbali. [48]
huku
Alidai kitendo cha kuwateka Pw4 na Pw17 walipokwenda kutambua miili ya marehemu katika Hospitali ya Muhimbili na kuwaweka ndani, huku akiwatishia kuwaua kwa bastola kuwa nao ni majambazi kama waliouawa na kuwadai wampelekee Pw2, kunadhihirisha kuwa alijua kila kitu kuhusu tukio hilo. [49]
huo
Upande huo wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa kujitegemea, Revocatus Mtaki Mgaya ulidai kuwa kwa mujibu wa ushahidi huo kuna maswali mengi ambayo hakuna mtu mwingine anayeweza kuyajibu isipokuwa washtakiwa pekee. [50]
huru
Washitakiwa wote walilipa faini na kuachiwa huru. [51]
huu
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Ephrem Kalimalwendo, alisema mifugo 3,956 imekwishakamatwa tangu kuanza kwa operesheni Januari 29 mwaka huu. [52]
huwa
Wadau hao wamesema kuwa wanafunzi wengi wanaokwenda kwenye shule za binafsi na zile za mashirika ya dini wengi wao huwa hawakuchaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari kwa shule za serikali hivyo hata uwezo wao ni mdogo hali ambayo inawafanya wapate muda wa kuandaliwa kabla ya kujiunga na kidato cha kwanza. [53]
huyu
Kama tuna jamii ya wahitimu wa viwango vile ambavyo mara baada ya kumaliza shule wakatoa talaka kwa vitabu na tabia ya usomaji; na kuwa, kwa mfano, mtu amesoma uchumi, lakini alipoajiriwa benki hajiendelezi tena kusoma, na hatimaye kubakiwa na ujuzi wa kuendesha benki, na kule nyumbani hana hata kamaktaba, ila CD za muziki na sinema tu, sidhani kama mtu huyu hatahitaji tena semina kumkumbusha kuhusu mabadiliko yanayojitokeza katika taaluma yake ya uchumi. [54]
ila
Sasa kama hakuna hujuma ni kwa nini wengine wabaki,? Nina imani hawa hawakuhusika ila wasiokuwepo ndio waliohusika na kuwafanya hawa kuwa kafara kwa matakwa ya wakubwa,” alidai Magafu. [55]
ile
Off-side' gani ile, waamuzi wapunguze mapenzi na timu kubwa, mechi ilikuwa inaisha sare hii sasa wanafanya mambo gani, TFF wawaangalie sana waamuzi wao wanaharibu soka hawa," alisema Minziro. [56]
ina
MWENYEKITI wa Simba, Hassan Dalali amevunja ukimya na kusema timu yake ina wakati mgumu hata kupata nafasi ya pili msimu huu, huku Mtibwa Sugar jana imeshindwa kuchukua nafasi tatu baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Tanzania Prison. [57]
iwe
Tunasema hivyo kwa sababu, asilimia kubwa ya Watanzania na hasa wakazi wa vijijini wana ukosefu wa elimu bora ya uzalishaji iwe kwa kilimo au ufugaji. [58]
iweze
Akikabidhi bendera kwa nahodha wa timu zitakazoshiriki kutoka Tanzania Bara, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Shyrose Bhanji alisema kikubwa ili timu iweze kuibuka na ushindi ni kuzingatia nidhamu na juhudi wakati wa mchezo. [59]
juu
Mwenyekiti huyo pia alimuomba Meja Jenerali Kalembo, awashauri viongozi wa ngazi za juu serikalini wanaomiliki ng’ombe katika wilaya hiyo, waiondoe mara moja, mifugo yao vinginevyo itakamatwa. [60]
juzi
Kocha Marcio Maximo alisema kuwa wachezaji wote wamewasili kambini juzi isipokuwa wachezaji watatu kutoka timu ya Mtinbwa Sugar ya Morogoro. [61]
kanda
Mbali ya kuwania nafasi ya urais, Kimbau pia atawania nafasi ya kamati ya maendeleo ya kanda. [62]
kansa
Zaidi ya kuwa msaidizi wake, jamaa huyo albino, alikuwa ni mvumbuzi wa dawa kutibu kansa ya moyo, hata hivyo hakuwahi kumwambia Kazim. [63]
karibu
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Afisa Mwandamizi wa benki ya Standard Charterd, Jeremy Awori alisema wanariadha hao wanatarajia kuondoka leo kwenda Hong Kong na benki yao inajivunia kuwa karibu na kuleta changamoto katika maendeleo ya michezo hapa nchini. [64]
kata
Akizungumza katika mkutano ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Meja Jenerali mstaafu Said Kalembo na kuwakutanisha wafugaji wa jamii ya Kimasai, viongozi wa vijiji, kata, kimila na wadau wengine, Mkunduge alisema kitendo cha kumilikishwa kwa ranchi za taifa zilizoko katika wilaya hiyo, kumesababisha ardhi iliyosalia isikithi mahitaji. [65]
kati
Pia Mgaya alidai hali hiyo inaondoa hoja ya mapambano ya kurushiana risasi kati ya watuhumiwa na marehemu kama ilivyodaiwa kwa kuwa marehemu walikuwa wamefungwa pingu na bastola moja waliyokutwa nayo ilikuwa imeshachukuliwa na watuhumiwa. [66]
kauli
Hii ni mara ya pili kwa Minziro kutoa kauli hiyo, kwani awali wakati wa mapumziko ya Krismasi alisema kuwa anatumia muda huo kukijenga kikosi chake kwa ajili ya mzunguko wa pili. [67]
kibao
Tunafurahi sana kuona kwamba angalau mmoja wa wale tuliowaona kuwa na roho ya korosho, ambao hawajali mateso ya wananchi ili mradi wanapata posho zao, na marupurupu kibao, na uwezo wa kufisadi wapendavyo, tunafurahi kuona kwamba angalau mmoja wao ameonyesha hali ya kuhuzunika, hata hali ya kushikwa na hasira kutokana na hali hii. [68]
kidato
Katika mtihani wa kidato cha pili mwaka jana, Mbele anatamba kwamba watoto wote waliofanya mtihani walifaulu. [69]
kidogo
Najua kuwa ni kiasi kidogo, lakini naahidi Sh1milioni kama hamasa kwa atakayetwaa ubingwa. [70]
kile
Hii inatokana na uwezo walionao lakini pia mtazamo wao kwa kile wanachokiamini –elimu bora kutoka kwenye shule hizo. [71]
kina
Kituo hicho kina watoto yatima 178 na wajane 72 ambao wote hupata mahitaji ya malazi, mavazi na elimu katika eneo moja. [72]
kuamini
Wakitoa hoja zao za kuishawishi mahakama kuamini kuwa washtakiwa hao hawana kesi ya kujibu, mawakili hao kwa nyakati tofauti waliieleza mahakama hiyo kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani hapo hauwahusishi na tuhuma za mauaji hayo moja kwa moja na badala yake ni ushahidi wa mazingira tu. [73]
kudai
Unajua watu wengi wanajua haki zao lakini wanashindwa kujua njia za kuzipata na hivyo kuamua kutumia vurugu kudai haki hizo," anafafanua. [74]
kufa
Wakati wanaendelea kuangalia ile picha aliingia daktari aliyekuwa akimwangalia Kazim na kumwomba waziri afupishe mazungumzo, badala yake wamsake yule mvumbuzi wa dawa kwani isingepita saa 12 kabla ya Kazim kufa ikiwa hatapata ile dawa. [75]
kufundishia
Sababu kubwa ni kuwa kule kwenye taasisi zetu hakuna vifaa vya kufundishia, wala wataalamu na muda wa kutosha wa kuweza kujifundisha mambo haya. [76]
kujua
Askofu huyo ambaye pia ni mfugaji, alitaka kujua adhabu inayotolewa kwa wakulima wanaopatikana na makosa kama yanayodaiwa kutendwa na wafugaji, kwa kuzingatia kuwa operesheni hiyo inawalenga pia wakulima. [77]
kule
Je, wataalamu wetu kule shuleni wanakwenda sambamba, katika mafunzo yao, na mabadiliko haya katika masoko ya bidhaa ya TEHAMA? Ninachosema hapa ni kuwa kama nchi yetu, kama zilivyo nchi nyingi za dunia ya tatu, haitajiingiza katika uzalishaji wa maarifa na elimu kwa matumizi ya wananchi wake, na kuwa taasisi za elimu vikawa vitovu vya maarifa mapya ili wahitimu wetu watoke wakiwa sio tu washika vyeti, bali wazalishaji elimu na maarifa mapya, huenda tunaweza kupunguza utegemezi wa nje na kupunguza mahitaji ya warsha kwa ajili ya wataalamu wetu. [78]
kuliko
Pia anaungana na baadhi ya watu wanaoilaumu jamii na serikali kwa kuidharau taaluma ya ualimu akisema kwamba jamii haimthamini mwalimu kiasi anaonekana kuwa mtu wa hali ya chini kuliko wengine. [79]
kulipa
Kwa hiyo, mahakama hii inawahukumu kila moja kulipa faini ya Sh50,000 na atakayeshindwa kulipa faini hiyo, atakwenda jela mwaka moja",alisema Massamu. [80]
kumbe
Maelezo haya ya askari huyu, yalinishangaza, sikutegemea kusikia kwamba kumbe mauaji haya yanaendelea kuwepo kutokana na uzembe wa watendaji wetu kusimamia majukumu yao. [81]
kumpa
Hata hivyo, Hakimu Nyasige aliendelea kumvumilia mchungaji huyo ili aweze kubadili msimamo wake kwa kumwamuru asome Biblia hiyo tena katika kitabu cha Warumi 13:1- 5, lakini baada ya kusoma kifungu hicho, mchungaji huyo hakubadili msimamo wake na hivyo kumpa mwanya Hakimu Nyasige kutoa hukumu yake. [82]
kumuua
Ndio akaona ni bora awapigie simu wale jamaa zake na kuangalia ni namna gani wanaweza kumuua albino ili waendelee na biashara ile ya madini na uvuvi wa samaki. [83]
kusema
Haitoshi kwa Waziri Mkuu kusema warudi walikotoka, kwa sababu hawasaidii na kwa kutambua kwamba kama kiongozi mkuu wa serikali ni kama baba wa watanzania wote alitakiwa kuwapa majibu yanayowatia moyo. [84]
kushindwa
Magafu alidai maelezo ya shahidi wa 25 na wa 26 pamoja na maelezo ya washtakiwa wa 11 na wa 12 ulitengenezwa na upande wa mashtaka baada ya kushindwa kuwaunganisha watuhumiwa kwa kosa wanalotuhumiwa. [85]
kutaka
Hata hivyo, aliungana na msimamo wa mkuu wa mkoa wa kutaka operesheni ya kuwaondoa wafugaji waliohamia katika Kilosa bila kufuata taratibu, iendelee. [86]
kuu
MAWAKILI wa washitakiwa wa kesi ya mauaji ya kukusudia ya wafanyabiashara watatu wa madini na dereva teksi wa Manzese Dar es Salaam, jana waliisihi mahakama kuu kuwaachia huru washtakiwa wao kwa madai katika ushahidi uliotolewa unaonyesha hawana kesi ya kujibu. [87]
kuua
Ni suala la kawaida kuua albino na damu zao au viungo vyao tunavitumia kwenye shughuli hizo za uchimbaji madini na uvuvi, watu wengi wanafanya hivyo. [88]
kwake
Pw2 ni Benadetha Ngonyani, ambaye wakati marehemu walikamatwa na washtakiwa nyumbani kwake walipokuwa wamekwenda kumjulia hali na kumpelekea pesa za matumizi kutoka kwa mumewe, Alex Ngonyani (Pw1). [89]
kwenda
Kwa kuwa walikamatwa na watuhumiwa wakiwa hai na kwa kuwa walikufa wakiwa chini ya ulinzi wa polisi basi washtakiwa wanapaswa kusimama mahakamani waieleze mahakama kuwa marehemu walikufaje au waliwezaje kuwatoroka na kwenda kupigwa risasi na watu wengine,” alidai. [90]
la
Kuhusu hoja ya kwamba watuhumiwa ndio waliowaua marehemu Mgaya alidai, imethibitishwa na Pw2, Pw6 na Pw 7 ambao waliieleza mahakama kuwa waliwaona watuhumiwa wakiwakamata marehemu wakapekua na kuchukua bastola aliyokutwa nayo marehemu mmoja wakawafunga pingu na kuondoka nao kwenye gari la watuhumiwa. [91]
labda
Baba alikuwa na wasiwasi kwamba labda mwanaye angemdharau lakini mimi nilimcheka. [92]
lake
NIANZE kwa kusema kuwa mimi naungana na Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda kuhusu katazo lake la warsha, semina, kongamano, mafunzo, semina elekezi na majina mengine mengi yenye kusudio moja kama lengo lake ni kudhibiti matumizi yasiyo ya faida ya fedha za wavuja jasho. [93]
lao
Pia wakati fulani mgonjwa aligoma kuongezewa damu na kuna wakati wanafunzi sita waligoma kufanya mtihani wa darasa la saba kutokana na imani ya dhehebu lao. [94]
lengo
Alisema  kutokana na  hali mbaya ya umaskini unaozikabili familia nyingi  hasa maeneo ya vijijini, watoto wengi wamekuwa wakisafirishwa kwenda mijini kwa lengo la kuwapatia kazi na badala yake watoto hao wamekuwa wakitumikishwa katika kazi mbaya zikiwemo za ukahaba. [95]
leo
Hivyo mahakama inalazimika kujiuliza ni nani walihusika katika mauaji haya maana hadi leo tuko gizani,” alidai Magafu. [96]
letu
Lengo letu kubwa ni kuhakikisha soka inapiga hatua zaidi kutoka hapa ilipo, tunaendelea na mikakati ya kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa na litakuwa ikifanyika kila baada ya minne" alisema. [97]
licha
Akizungumzia utata wa ushahidi, Magafu, licha ya kuileza mahakama kuwa kuna mashahidi waliieleza mahakama kuwa kulikuwa na mapigano kati ya polisi na majambazi, alidai inasikitisha kuwa katika mashahidi hao wengine wanasema mauaji yalifanyika Sinza na wengine msitu wa Pande. [98]
ligi
Mapumziko hayo mafupi ya ligi tutaakikisha tunayatumia vizuri ilikuakikisha nafasi ya pili inabaki kwetu na kucheza michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika. [99]
lugha
KAMPUNI ya MG Graphics ya jijini Dar es Salaam kwa mara ya kwanza imetengeneza filamu ya katuni iitwayo 'Sungura mjanja' ambayo itatumia lugha ya Kiswahili katika kufikisha ujumbe kwa jamii. [100]
maafisa
Msemwa aliongeza kuwa hata mashahidi kadhaa waliotoa ushahidi mahakamani hapo wakiwemo maafisa wa juu wa polisi waliochunguza tukio hilo na Mkurugenzi wa Mashtaka, Elieza Feleshi walithibitisha kuwa Zombe hakustahili kushtakiwa. [101]
madini
Katika kesi hiyo Zombe na wenzake wanatuhumiwa kuwaua kwa makusudi wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Wilaya ya Mahenge mkoani Morogoro ambao ni Sabinus Sabinus Chigumbi maarufu kama Jongo na ndugu yake Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe Juma Ndugu na dereva teksi wa Manzese jijini Dar es Salaam. [102]
mafanikio
Miezi kadhaa baadaye biashara zote alizifungua, kwa kuanzia zilikuwa na mafanikio makubwa. [103]
magumu
Pia huficha ukweli kuwa uwezo wa walimu wengi ni mdogo na hufanya kazi katika mazingira magumu. [104]
maisha
Lengo la mfumo wowote wa elimu, moja ya vigezo vya kufanikiwa kwake, ni kuhakikisha kuwa shule na wanataaluma wanaweza kuzalisha maarifa mapya ambayo yatawafikia wananchi wanaoyahitaji kwa ajili ya kuboresha maisha yao, au kuongeza tija. [105]
maiti
Baba mmoja akaniambia mtoto wake akamshtukiza akilia mbele ya luninga kwa kuona maelfu ya maiti yaliyorundikana. [106]
makao
Inadaiwa baadhi ya asasi hazina hata ofisi wala makao yanayoeleweka na pia inadaiwa zinatumia matatizo ya watoto yatima au wale waishio katika mazingira magumu kujinufaisha. [107]
mapema
Katika mechi ya jana timu ya Prison ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Sokoine ilionekana kama ingepoteza mchezo huo baada ya kukubali bao la mapema lilofungwa na Mtibwa Sugar. [108]
mapya
Tunapozungumia ongezeko la warsha, semina na kadhalika tujiulize kama mfumo wetu wa elimu una uwezo wa kuzalisha maarifa mapya. [109]
mara
Wakati huo huo mshtakiwa wa 11 Rashid Lema, ambaye siku ya kwanza ya kesi alishindwa kupanda kizimbani kwa kuwa mgonjwa, jana hakuweza kufika tena mahakamani hapo kwa mara ya pili mfululizo. [110]
masomo
Mafanikio makubwa yaliyopatikana hadi sasa ni vijana hao kuwa na uhakika wa kusoma muda wote bila kukatishwa masomo kutokana na sababu yoyote ile. [111]
mawaziri
Lakini kwa nini tatizo hili la mauaji ya albino kuuawa limeshindikana kudhibitiwa? Mimi nadhani watendaji wa serikali kwa maana ya mawaziri, ndio wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kudhibiti mauaji haya. [112]
mfuko
Alisema fedha zinazokusanywa kutokana na operesheni hiyo, zitaingizwa katika mfuko wa halmashauri na kupangiwa majukumu ya kimaendelea. [113]
mfupi
Huku akiendelea na kazi Kazim alikuwa ni mtu tajiri kwa muda mfupi mno. [114]
mguu
Alisema kwa mujibu wa daktari wake amesema mchezaji huyo anasumbuliwa na kifundo cha mguu, lakini anaendelea vizuri uenda leo akafanya mazoezi na wenzake. [115]
michuano
Maximo alisema mara baada ya mechi hiyo wachezaji hao wataungana na wenzao kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya fainali hizo. [116]
migomo
Mdoe aliwashukia wanafunzi wanaoabudu migomo na maandamano ya mara kwa mara akiitaja kuwa ni miongoni mwa mambo yanayokwamisha dhamira iliyopo ya kuboresha hali ya elimu kwa vijana nchini. [117]
mila
WASOMI wametakiwa kuwa mstari wa mbele kupiga vita mila potofu ikiwemo ya ukeketaji kwa kueleza bayana athari zake kwa jamii ili kusaidia kuleta mabadiliko kwa haraka zaidi. [118]
milioni
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania, CHANETA, Shyrose Bhanji ameahidi kitita cha shilingi milioni 1 kwa timu itakayoibuka nbingwa Mashindano ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na kati yanayotarajia kuanza Jumatatu kisiwani Zanzibar. [119]
miongoni
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo mifugo 1,373 miongoni mwa hiyo, imekombolewa na kuchukuliwa na wamiliki wake. [120]
mji
MCHUNGAJI wa Kanisa la EAGT lililo Mtaa wa Ichenjezya kwenye mji mdogo wa Vwawa mkoani Mbeya Simon Kitwike, 48, amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela baada ya kukataa kuapa mahakamani kutokana na imani ya dini yake. [121]
mjini
Semina hiyo inawashirikisha maofisa wa polisi, uhamiaji, mahakama, pamoja na wajumbe kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali na inafanyika kwenye hoteli ya Kibo Palace mjini Arusha. [122]
mno
Operesheni ya kuondoa wafugaji walioingia katika wilaya hiyo bila kufuata taratibu, imekuwa ikilalamikiwa mno na watu wa kundi hilo, kuwa imetawaliwa na vitendo vya unyanyasaji dhidi yao. [123]
msitu
Alidai wamekanusha hoja hiyo kupitia kwa Pw9, Pw10 na Pw20, ambao ni wakazi wa eneo lililodaiwa kutokea mapambano hayo, ushahidi ambao unaungwa mkono na maelezo ya washtakiwa wa 11 na wa 12 kuwa marehemu waliuawa katika msitu wa Pande kama vinavyoonyesha vielelezo vilivyopokewa mahakamani hapo. [124]
muda
KOCHA mkuu wa Moro United Fredy Felix Minziro amesema atatumia muda wa mapumziko ya Ligi Kuu kukisuka kikosi chake ili kuepukana na janga la kushuka daraja. [125]
mwa
Mchungaji huyo, ambaye alifika mahakamani hapo kwa ajili ya kutoa ushahidi katika kesi ya wizi kwenye nyumba yake iliyovunjwa mwishoni mwa mwaka jana na kuibiwa mali kadhaa, aliishangaza mahakama baada ya kukataa kuapa kabla ya kuanza kutoa ushahidi wake. [126]
mwanzo
Nimeona ni bora niingie kambini rasmi ili kujiandaa na mchezo huu, nafanya mazoezi pia ya kuogelea ili kuhakikisha namaliza mpambano huo katika raundi ya mwanzo," alisema Cheka. [127]
mwezi
Kwa matokeo hayo Prison imepanda hadi nafasi ya nne ikiwa na pointi zake 22 ikizidiwa pointi mbili na Simba huku Mtibwa imeporomoka hadi nafasi ya tano na pointi zake 21, wakati ligi hiyo inapoingia kwenye mapumziko ya mwezi mzima. [128]
mzazi
Watoto yatima yaani wasio na baba na mama na waishio katika mazingira magumu hulipiwa gharama zote na asasi hiyo wakati wale wenye mzazi mmoja hupata punguzo. [129]
mzuri
Hisabati, Sayansi masomo ambayo humjenga mwanafunzi na hata kumfanya kuwa na msingi mzuri pindi anapoanza kusoma masomo ya kidato cha kwanza. [130]
na
HATMA ya Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Abdallah Zombe katika kesi ya mauaji ya ya kukusudia inayomkabili pamoja na askari wenzake 12, itajulikana Jumatatu ijayo. [131]
naye
Katika sheria zetu hakuna kifungu kinachosema mtu akishuhudia kosa linatendeka hata kama ni la mauaji basi naye anakuwa na hatia,” alidai. [132]
ng
Wengi wao wanadhani mtu akiwa na shamba kubwa sasa au ng’ombe wengi bila kuzingatia kanuni za uzalishaji wa kisasa ndiyo fahari hata kama hawapati faida. [133]
ngapi
Wanaonibisha, waniambie wameangalia kweli kadi ngapi katika hizo alizopewa katika miezi sita iliyopita. [134]
ngumu
Mwenyekiti huyo wa Simba, Hassan Dalali alisema:"Mpaka sasa wanakazi ngumu sana kuchukua nafasi ya pili kwa kuwa kuna timu kama tatu ambazo wanalingana pointi na wanawania nafasi hiyo. [135]
ni
Juzi upande wa utetezi uliwasilisha hoja mahakamani hapo na kuieleza mahakama kuwa washtakiwa hawana kesi ya kujibu kwa madai kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kutoa ushahidi ambao unawahusisha washtakiwa hao moja kwa moja na tuhuma za mauaji na kwamba ushahidi walioutoa ni wa mazingira na wa kusikia tu. [136]
nia
Alidai kwa mujibu wa sheria hiyo upande wa mashtaka unatakiwa kuthibitisha kama marehemu walikufa kwa vifo visivyo vya kawaida pia wathibitishe kama washtakiwa ndio waliowaua marehemu na kwamba washtakiwa walikuwa na nia ovu au dhamira ya kuwaua. [137]
niwe
Lakini wangapi wameonyesha nia ya kwenda kuona hawa wahanga wenyewe na kutafuta usuluhisho? Nakumbuka msemo mmoja wa hayati Trevor Huddleston aliyekuwa mstari wa mbele kupinga ubaguzi wa rangi 'bora niwe na damu mkononi kuliko maji kama Pilato'.’ 'Una maana gani?' 'Namaanisha hivyo. [138]
nzuri
Kamishna msaidizi huyo wa ustawi wa jamii alieleza kuwa kutokana na mji hiyo ya Dar es Salaam , Arusha na Zanzibar kuwa na hali nzuri kiuchumi imekuwa kivutio kikubwa kwa  kushamiri biashara ya binadamu hapa Tanzania. [139]
one
HALIKUWA jambo la ajabu kukuta baadhi ya shule za sekondari za binafsi na za dini zikitoa mafunzo ya awali ya sekondari kwa wanafunzi wake maarufu kwa Kiingereza kama Pre form one. [140]
pale
Ninafundisha pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kozi ambazo mwanafunzi anatakiwa kujua kupiga picha za video, kuhariri habari au picha kwa ajili ya televisheni au redio; kuchanganya rangi kwa ajili ya maigizo ya jukwaani, sinema au televisheni, aweze kupiga picha za analogi na za "digital", waweze kutengeneza sinema au vipindi vya redio, au waweze kutengeneza kurasa za tovuti na kusanifu kurasa za magazeti. [141]
rais
Pia Kaishozi alikanusha hoja kuwa Tume ya Polisi ilimuona Zombe kutokuwa na hatia kwani tume hiyo haikutoa taarifa kwa kuwa haikuweza kukamilisha upelelezi wake baada ya tais kuunda tume yake, na kwamba hata tume ya rais iliyokuwa chini ya Jaji Kipenka ilieleza kuwa haikuweza kutambua mahali mauaji yalikofanyika. [142]
rangi
Akizungumza na Mwananchi jijini jana, Mkurugenzi mbunifu na mtayarishaji wa filamu hiyo Rashidi Mbago alisema hii kwa sasa ndiyo filamu yao ya kwanza ambayo imetumia mtindo wa 2D ambayo wametumia michoro na rangi kwa kupitia kompyuta. [143]
rasmi
TIMU ya Tanzania 'Taifa Stars' jana ilianza mazoezi rasmi kwa ajili ya kujiandaa na fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa wa ndani (CHAN) huku wachezaji wa tatu wakiwa hawajawasili. [144]
riadha
Tunafuraha kuweza kupata nafasi hii ya kushiriki katika mashindano makubwa kama haya ya Marathoni na timu ya riadha ya Tanzania ni moja ya timu zinazoundwa na vijana. [145]
ridhaa
Akizungumza baada ya kuchukua fomu hiyo Kimbau alisema anataka kurudisha heshima ya ngumi za ridhaa nchini. [146]
risasi
Alidai ushahidi huo unaungwa mkono na ushahidi wa Pw4, Pw5, na Pw17, pamoja na maelezo ya washtakiwa wa 11, Koplo Rashid Lema na mshitakiwa wa 12, Koplo Rajabu Bakari yaliyotolewa mahakamani hapo ambao walieleza kuwa marehemu hao waliuawa kwa risasi. [147]
roho
Wanaume wa kweli tutamwelewaje? Narudia kusema, mwanasiasa anapaswa kuwa na roho ngumu kama jabali ya Mwanza. [148]
saa
Inspekta wa polisi, Boniface Edwin, akisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Richard Kabate, alidai kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 18 majira ya saa 12:00 jioni kwenye maeneo ya Kimara Baruti. [149]
sana
Kazi ya kupata chanjo ya ugonjwa huo imekuwa ikienda taratibu sana. [150]
sawa
Ubaba siyo sawa na ubabe. [151]
shaka
Akitoa hukumu hiyo, hakimu Massamu, alisema upande wa mashitaka umethibitisha bila kuacha shaka kuwa washitakiwa wanayo hatia kama walivyoshitakiwa. [152]
shida
Baadhi ya walezi na wazazi hawakuona shida yoyote wala gharama waliyotumia kuwapeleka watoto wao kwenye shule hizo. [153]
shule
Alisema kuwa atahakikisha kunakuwepo na mashindano ya ngumi kwa shule za sekondari ili kupata mabondia wenye sifa za wa ngumi za ridhaa kama ilivyokuwa katika siku zilizopita. [154]
si
Kisheria kuwa na “common intention” (Nia Moja) si lazima washtakiwa wawe wamekaa pamoja na kupanga bali hata mwenendo na matendo yao yanaweza kuthibitisha. [155]
sifa
Bukombe alisema washitakiwa walikaidi maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Singida  katika barua yake ya Mei 28 mwaka 2006 iliyowataka vijana wote wenye sifa ya kuhudhuria mafunzo ya mgambo, wakahudhurie bila kukosa. [156]
sina
Jamani, kabla sijashambuliwa na kuliwa na wanajinsia sina budi kusema kwamba, tofauti na ibada za kidini, hata 'Kadi ya Mama' zipo. [157]
sio
Alikunwa na vijana hao kwa kuonesha kivitendo dira waliyonayo kwa kujikusanya kupitia Bunge Kivuli la Vijana ambalo linawapa njia ya kujiandaa kuja kuwa viongozi wa kuzitumikia jamii zao sio kwa cheo tu bali kwa kazi. [158]
sisi
Wakati Baba wa Taifa hayati Julius Nyerere alitusihi tukimbie kwa vile wenzetu wanatembea, sisi tunatembea wakati wenzetu ndio hasa wanaokimbia. [159]
siyo
Serikali itambue kuwa mpango wa mafunzo ya awali ya sekondari ulilenga kuwaandaa wanafunzi wanaotoka shule za msingi ambazo Kiingereza siyo lugha ya mawasiliano na hii inazingatia kuwa lugha hiyo ndiyo inayotumika sekondari kwa masomo yote isipokuwa Kiswahili," anasisitiza. [160]
suala
Lakini shahidi hawa watatu hawakuwahi kupelekwa katika gwaride la utambuzi ingawa uchunguzi wa suala hilo ulifanywa na maafisa wa juu wa polisi. [161]
tuna
Pia shule inawapa nafasi hata wale watoto ambao sio yatima tuna unafuu wa ada kwani lengo letu si biashara ila kuwapatia elimu watoto wote wa Kitanzania bila kubagua wakoje na wanaishije," amesisitiza Mbele. [162]
ubora
Upungufu katika nyanja hizo ndio unaosababisha kuwepo kwa ubora usioridhisha wa elimu inayotolewa. [163]
ukatili
Kwa mujibu wa UNICEF, kati ya wasichana milioni 100 na 400 milioni wanafanyiwa ukeketaji na hivi leo nchi 28 za Afrika zinaendeleza mila hiyo ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa kike. [164]
uko
Sasa Kazim ujue kwamba uko chini ya ulinzi, kwa sababu ni mgonjwa sana tutakufunga pindu hapa wakati tunaangalia namna ya kukufanyia, uko chini ya ulinzi,” alisema mkuu wa jeshi la polisi ambaye alionekana kusononeka sana kwa kifo cha yule mvumbuzi wa dawa. [165]
umri
Malaria ni moja ya magonjwa hatari duniani, ukiwa unaua watu 880,000 kwa mwaka, wengi wao wakiwa ni watoto walio na umri chini ya miaka mitano. [166]
una
Dai lao kuu, kama ilivyo kwa wazazi na wadau wa elimu nchini ni kwamba mfumo wa elimu yetu una upungufu mkubwa kuanzia ngazi ya utungaji sera, mitaala inayotumika hadi usimamizi kisekta. [167]
usiku
Siku moja usiku akiwa nyumbani alitafakari sana hali ngumu ya maisha ambayo angeanza kuishi. [168]
uso
Zombe alitoka mahakamani hapo tofauti na siku zote baada ya kesi hiyo kuahirishwa, akionekana kuwa mpole na uso ukiwa na tabasamu la mbali tofauti na siku nyingine ambazo hutoka kwenye chumba cha mahakama akirusha maneno. [169]
usoni
Martin Mbonde aliyefanya uchunguzi wa vifo hivyo na taarifa aliyoitoa na kukabidhiwa mahakamani hapo alithibitisha kuwa marehemu walikufa kwa vifo visivyo vya kawaida, yaani kwa kupigwa risasa kisogoni na kutokea usoni. [170]
utoro
Mikakati mingine ya wilaya ni kudhibiti utoro wa wanafunzi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanafika na kuingia darasani na pia kuhakikisha wanaoandikishwa darasa la kwanza wanamaliza darasa la saba. [171]
uwezo
Naye katibu Mkuu wa chama cha riadha Tanzania, Suleiman Nyambui alishukuru benki hiyo kwa udhamini wao na ushirikiano wao katika michezo na kuzitaka kampuni nyinbgine ambazo ziuna uwezo wa kusaidia michezo kama hiyo kuweza kujitokeza na kuisaidia. [172]
vema
Iliwachukua dakika 13 kabla ya mabingwa wao Kombe la Tusker kuandika bao la kuongoza kupita mchezaji wake Rashid Gumbo aliyeunganisha vema kwa kichwa mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime. [173]
vifaa
Hukimbilia dawa hiyo kama njia ya kuficha udhaifu wa serikali yenyewe kushawishi ujenzi wa shule nyingi bila walimu wa kutosha na vifaa. [174]
vile
Kabla ya kutolewa adhabu hiyo,kila mshitakiwa kwa wakati wake, aliiomba mahakama hiyo kumpa adhabu nafuu kwa vile, hilo ni kosa la kwanza na kwamba hawatarudia tena kutenda kosa hilo. [175]
vipi
Huku sasa ni kuzinguana, kumbe hata mawaziri nao huwa wanakuwa wasanii, inawezekanaje niwasiliane na wewe nikiwa nje ya nchi uniambia yuko mvumbuzi wa dawa ya kuponya tatizo langu halafu sasa aniambie hajui atampata vipi, huu ni uhuni,” alijisemea Kazim akiwa mwenye hasira na kuwaza kuwa kama asingempa dawa hiyo angefanya mpango wa kumuua kwa sababu naye alikuwa albino. [176]
vituo
Mbele anatoa ushauri kwa serikali iangalie uwezekano wa kuvipatia ruzuku vituo ambavyo vinashughulikia kuwasomesha watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu hapa nchini ili watoto wengi zaidi wasikose haki hiyo ya msingi maishani. [177]
vya
Alidai kuwa kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa na mashahidi wote 37 (37 Pws) mahakamani hapo pamoja na vielelezo 23, wanaamini kuwa washtakiwa wote wana kesi ya kujibu kuhusu vifo vya watu wanne. [178]
vyake
Kweli wale watu walimuua yule albino na kwenda na viungo vyake kwenye maeneo ya biashara. [179]
wakuu
RAIS Jakaya Kikwete amerejea nchini jana akitokea Addis Ababa, Ethiopia kwenye mkutano wa wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika(AU) akiwa mwenyekiti wa umoja huo aliyemaliza muda wake. [180]
wale
Lakini wale watakaoshindwa kwenda sambamba na kasi hiyo watanyweshwa dawa. [181]
waliotoa
Mawakili wa washtakiwa wote waliieleza mahakama kuwa kati ya watu 37 waliotoa ushahidi mahakamani hapo, hakuna shahidi hata mmoja aliyeweza kuithibitishia mahakama hiyo jinsi washtakiwa hao walivyotenda kosa la mauaji hayo. [182]
wangu
Nasema tu kwamba najaribu kuokoa mfuko wangu kwa kubandika anwani pepe hapo chini lakini bado nikifika kwenye ibada ya mikutano ya watukufu na watukufuru, nadaiwa kadi ya Bwana na mimi. [183]
wapi
Tunaamini ni mshtakiwa wa kwanza hivyo anayo ya kujibu kama aliuliza hao waliokamatwa na pesa hizo ziko wapi. [184]
wasio
Pili inawahudumia wajane na tatu imejenga Shule ya Sekondari ya Tushikamane kwa ajili ya watoto inaowalea na wengine wasio yatima. [185]
watendaji
Na ukweli ni kuwa baadhi ya maafisa wa serikali na hata watendaji katika AZISE wamekuwa wakitumia mwanya wa kulegalega kwa usimamizi kuvuna fedha kwa njia hizo. [186]
wauaji
Lakini katika shauri hili kuna ushahidi wa mazingira na si wa moja kwa moja, kuthibitisha mshtakiwa wa pili na wenzake kuwa wauaji wa marehemu. [187]
wenzao
Kiongozi wa kimila wa jamii ya Kimasai, alimweleza mkuu wa mkoa kuwa, pamoja na mambo mengine, watu wa kundi hilo hawakushirikishwa kikamilifu katika kufikia uamuzi wa namna ya kuendesha operesheni hiyo, kama ilivyofanywa kwa wenzao wakulima. [188]
wetu
Lakini nadhani hoja yake pia inazua hoja nyingi juu ya mfumo wetu wa elimu. [189]
wewe
Je, wewe kijana wa Tanzania una dira gani? Na unatumia juhudi gani ili kufikia dira hiyo?" alihoji na kuongeza kuwa serikali inatambua umuhimu na mchango wa vijana katika nchi kwa kuwapa nafasi ya kujadili na kuhoji mambo yanayoendelea ndani na nje ya nchi. [190]
wiki
Pia, Maximo alisema kuwa mchezaji Godfrey Bonny jana alishindwa kufanya mazoezi hayo kutokana kuwa majeruhi baada ya kuumia katika mechi ya klabu bingwa kati ya Yanga na Etoile ya Wacomoro iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam. [191]
yangu
Kwa hiyo rai yangu ni kwamba washtakiwa wote waachiwe huru kwa kuwa inaonekana hawana hatia wala kesi ya kujibu isipokuwa mshtakiwa wa 11 na wa 12 kama mahakama itaona kuna ushahidi wa kutosha ndiyo, lakini yawezekana nao walidanganywa,” alidai Magafu. [192]
yao
Mgaya aliongeza kuwa namna marehemu walivyopigwa risasi wote kisogoni huondoa dhana ya kuwepo kwa mapambano kwa kuwa yangekuwepo basi marehemu wangekuwa na majeraha usoni au sehemu tofauti za miili yao. [193]
yenye
Kuua mbu kwa dawa ni moja ya njia za kuzuia ugonjwa wa malaria, lakini kupata dawa yenye ufanisi na ambayo gharama zake ni nafuu ni vigumu, alisema Wondji na wenzake. [194]
yetu
Nidhamu ni kitu kikubwa ambacho kila mchezaji anapaswa kuzingatia ili kuweza kufanikiwa na ni mategemeo yetu Watanzania watatupa hamasa ya kutosha ili timu iweze kurudi na ushindi katika mashindano haya. [195]
yeye
Akiongea na Mwananchi, mchungaji aliyejitambulisha kwa jina la Mwakasaka alisema amepokea hukumu hiyo kwa masikitiko na mshangao mkubwa kwani mchungaji huyo amenukuu vibaya Biblia, akisema kuwa kitabu hicho kinakataza mtu kujiapiza yeye mwenyewe lakini inaruhusiwa kuapishwa kwa mamlaka iliyo ya duniani. [196]
yoyote
Kama mahakama itatilia maanani sheria itamwachia huru mshtakiwa wa pili bila kumtaka kutoa maelezo yoyote,” alidai Ishengoma. [197]
yuko
Aliongeza kuwa ingawa Zombe yuko mahakamani, hakustahili kuwa mshtakiwa bali alistahili kuwa shahidi huku akidai kuwa ameshitakiwa kwa nia mbaya tu. [198]
zaidi
Kwa hiyo akipewa nafasi anaweza kueleza zaidi,” alisisitiza Kaishozi. [199]
ziada
Pamoja na uchanga huo shule imekamilika kwa maana kuna maabara kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kujifunza masomo ya sayansi bila matatizo na kuna maktaba inayotoa fursa wanafunzi kusoma vitabu vya ziada. [200]