Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-02-23

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aina
Moja ya mafanikio hayo ni pamoja na kupatikana kwa gari aina ya Toyota Hiace lililokuwa limeibwa Dar es Salaam mwezi Januari na kupelekwa mkoani Dodoma ambako wezi walilirudisha jijini hapa wiki moja iliyopita baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Kondoa kuendesha operesheni kubaini wahalifu. [1]
akaanza
Nilipomwonesha ile barua akaanza kupapasa matako yake kama vile anakumbuka jinsi alivyochapwa. [2]
akawa
Anaweza akawa mjanja, (Mwizi smart) anaweza akawa anafuta namba zote zilizoingia na kutoka kabla ya kuingia kulala. [3]
akifanya
Tunakumbuka, chini ya uongozi wa Mwalimu, kiongozi alikuwa akifanya kosa, lilikuwa likitokea wakati akifanya jambo kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania, lakini sasa hali hiyo ni tofauti kwani viongozi wetu wa sasa wanafanya kazi kwa ajili ya kuwapora wananchi. [4]
akilini
Tayari ulikuwa na wasiwasi, na kuna vitu vilikwambia akilini kuwa hii sio kawaida yake lazima kuna mtu anayejaribu kuingia baina yenu. [5]
akiwemo
Mimi nawajua baadhi yao ambao hawatarudi, akiwemo mheshimiwa Jussa Ismail na Suleiman Dedes. [6]
alijua
Yule Bwana alijua kuchapa. [7]
alipo
Wakati Takukuru ikichukua hatua hiyo kuna wananchi ambao wameviarifu baadhi ya vyombo vya habari kuwa wanaweza kutoa taarifa za alipo Liyumba. [8]
aliweza
Mtanzania Randeep Birdi aliweza kuibuka mshindi kwa kutumia muda wa saa 3 na dakika 33 na sekunde 48 akifuatiwa na Saleem Haji huku akiwasili kwa kutumia muda wa saa tatu dakika 34 na sekunde 30 akimshinda Don Smith wa Kenya. [9]
ama
Naye akanijibu kuwa ama anavipata kutoka huko shuleni anakosoma binti yake au wakati mwingine kutoka maduka ya vitabu kadhaa, yaliyoko hapa Dar es Salaam. [10]
ambazo
Alisema zaidi ya maeneo 14 tofauti yatapata fedha hizo kwa kazi ambazo zimepangwa. [11]
ana
Ni kitendawili, wanajua bila shaka naye ana siri nzito wanajaribu kuficha ukweli. [12]
au
Huku akiainisha eneo moja baada ya jingine, Kyaruzi alitoa pia ufafanuzi juu ya kwanini mradi huo usitekelezwe na Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo nchini (RITA), akisema mradi huo ni jambo la Muungano, hivyo kuweka chini ya RITA au Mpiga Chapa wa Serikali, itakuwa ni kupingana na katiba ya Jamhuri. [13]
aweze
Alisema kuwa baada ya mazungumzo mtuhumiwa huyo aliahidi kumsaidia gharama za matibabu na kumtaka ajiandae kwa ajili ya kwenda hospitali kupata matibabu siku ya pili ambapo wakiwa hospitalini hapo mtuhumiwa alimshawishi kupima choo na damu ili aweze kujua ugonjwa unaomsumbua. [14]
baadaye
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilifuta dhamana ya Liyumba Februari 19 na kutoa amri ya kuwakamata wadhamini wake ambao walikamatwa siku hiyohiyo na baadaye kuachiwa. [15]
bado
Mwendesha mashitaka alisema kuwa upelelezi bado haujakamilika na Hakimu Nkya aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 24 mwaka huu itakapotajwa tena. [16]
baina
Taarifa ya kikao cha usalama cha wilaya hiyo , ambayo nakala imepatikana Dar es Salaam, inaonyesha kuwapo kwa ushirikiano mzuri baina ya vyombo vya usalama na wananchi na kwamba wameweza kubaini wahalifu mbalimbali. [17]
bara
Aidha, homa ya uchaguzi pia ipo kwa wagombea ujumbe wa Baraza kuu la uongozi la chama hicho ambapo hadi sasa kuna wagombea 107 katika nafasi hiyo, 70 kutoka bara na 37 kutoka Zanzibar. [18]
bila
Alifafanua kwamba, linaloshangaza zaidi ni serikali kukaa kimya bila kumchukulia hatua hakimu aliyempa dhamana na kupokea hati ya kusafiria ya Liyumba iliyomalizika muda wake mwaka mmoja uliopita. [19]
calls
Subiri mpaka ajisahau, chukua simu yake wakati yeye hajui, nenda kwenye incomming calls, utainasa hiyo namba. [20]
cha
Habari za kifo cha Komal zilianza kuenea jijini hapa kuanzia juzi Ijumaa huku baadhi ya watu wakidai kuwa ameuawa na wengine wakidai kuwa amejinyonga, lakini msemaji wa Jeshi la Magereza, Omari Mtiga alikanusha taarifa hizo akidai kuwa amewasiliana na maafisa wa magereza ambao wamemuhakikishia kuwa hawana taarifa hizo. [21]
chetu
Siku nyingi watu walikuwa wakijiuliza kuhusu itikadi ya chama chetu, hivyo moja ya shughuli ambazo zitafanyika katika mkutano mkuu ni kutangaza rasmi kwamba CUF inafuata itikadi ya kiliberali," alisema Jussa. [22]
dhidi
Sakata la mradi wa vitambulisho vya taifa, limeibua mjadala mzito nchini kufuatia tuhuma dhidi ya Waziri Masha, kwamba amekuwa na maslahi katika Kampuni ya Sagem Securite ambayo hata hivyo, imetupwa nje ya mchakato wa awali wa zabuni. [23]
duniani
NI jambo lililo wazi kuwa soka ni moja kati ya michezo inayopendwa zaidi duniani huku vijana wengi wenye vipaji wakijipatia utajiri mkubwa kwa kulipwa fedha nyingi. [24]
enzi
Nakupa ubwana kwa shingo upande maana enzi zangu haikuwa hivyo. [25]
es
UTATA umetawala kuhusu maisha ya mke wa mfanyabiashara Vinoth Praven (23) raia wa India aitwae Komal Katakia (22), ambaye anashikiliwa na Jeshi la Magereza katika gereza moja jijini Dar es Salaam, kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara Abdulbasiti Abdallah (21), huku taarifa za awali zikieleza amefariki dunia na zingine zikisema kuwa yu hai gerezani. [26]
faida
Akifafanua jinsi kiasi hicho cha fedha kitakavyotumika, Dk Kyaruzi alisema serikali inapaswa kusimamia baadhi ya maeneo, ikiwa ni pamoja na kuajiri watu watakaofanya kazi hiyo, majengo, kuboresha miundombinu na kutoa elimu kwa wananchi juu ya faida za kuwa na kitambulisho cha uraia. [27]
gani
Dk Kyaruzi alisema kwa mujibu wa tathimini ya mradi, gharama kubwa zitakuwa kwenye kutoa elimu ya umuhimu wa kuwa na kitambulisho na pia ni jinsi gani ya kutambua nani ni raia na nani si raia. [28]
ha
Ha ha ha. [29]
hafanyi
Ndiyo! Bila kiboko mtu hafanyi kazi. [30]
hakika
Tumeshuhudia mchezo wa soka nchini ukikubalika na kufikia hatua nzuri kutokana na kubadilika kwa mfumo wa uongozi ndani ya chama cha mchezo huo (TFF), hakika mabadiliko yakifanyika ndani ya Chaneta ikiwa ni pamoja kuwa na programu za kukuza vipaji kuanzia kwenye mashule mpaka vyuoni tutakuwa na ligi ya aina yake pamoja na timu ya taifa isiyofungika. [31]
hana
Kwa upande wake Naibu DCI, Kivuyo, alisema tukio hilo lilipotokea yeye alikuwa Kamanda wa Trafiki na kwamba hana taarifa zaidi. [32]
hao
Komal amekufa tangu juzi (Ijumaa) lakini tunashangaa mpaka sasa serikali haijataka kutoa taarifa za kifo chake na hata magazeti hayajaandika" alisema mmoja wa jamaa hao na kuongeza. [33]
hasa
Mradi huo ambao unakadiriwa kuchukua miaka mitano utakapoanza rasmi, umezusha malalamiko na utata mwingi, hasa kiasi cha fedha kitakachotumika na nani anapaswa kupewa kazi hiyo. [34]
hati
Hakimu wa mahakama hiyo Hadija Msongo alimpatia dhamana Liyumba baada ya kuwasilisha hati ya nyumba yake yenye thamani ya Sh 882 milioni badala ya Sh 50 bilioni na alitakiwa kufika kesho mahakamani hapo. [35]
hawa
Nani kawapa usugu? Hebu soma barua ya wanafunzi hawa. [36]
hayo
Wakati hayo yakiendelea, jana Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilikaririwa ikitangaza donge nono kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa Liyumba. [37]
hii
Hata hivyo baadhi ya vyanzo vya habari hii vimedokeza kuwa mtuhumiwa huyo amekufa na maiti yake imepelekwa Hospitali ya Rufaa Muhimbili ikiwa na makovu. [38]
hiki
Kituo hiki lengo lake kuu ni kuunganisha watu wa aina mbalimbali duniani kwa kutumia lugha yao na ubunifu wa mawazo yao. [39]
hili
Viongozi wawili wa ngazi za juu wa vyama vya Cuf na Chadema, kwa nyakati tofauti jana waliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam kwamba, kinachofanyika kwa Liyumba ni usanii sawa na ilivyokuwa kwa Balali, kutokana na watu hao kuwa na siri nzito. [40]
hiyo
Juhudi za kuwapata maofisa wa magereza kuthibitisha kifo hicho hazikufanikiwa baada ya ofisa mmoja kupigiwa simu, ambapo mara baada ya kuulizwa swali alikata simu hiyo na kukataa kupokea tena kila alipopigiwa na mwandishi. [41]
hizi
Je, hili ni sawa kwa baadhi yetu, lakini katika mazungumzo na rais sikuona hata msitari ambao wakuu wa wizara walimweleza Kikwete juu ya kuwapo kwa shule hizi za 'watakatifu' waishio duniani, wala hawako mbinguni. [42]
huo
Baada ya kuuweka mwili huo kwenye begi la nguo, washitakiwa hao wanadaiwa kuutelekeza kwenye gari dogo na kisha kulipaki katika Jengo la Harbour View (zamani J Mall) ghorofa ya pili. [43]
hususan
Baadhi ya kazi hizo ni uhamasishaji wananchi, ununuzi wa kompyuta, ujenzi wa ofisi na utengenezaji wa miundombinu hususan barabara. [44]
huu
Febuari 8 mwaka huu Polisi jijini Dar es Salaam walimtia mbaroni raia wa India, Vinoth Praven (23) na watu wengine wanne akiwamo mke wa raia huyo, Komal Katakia (22), kwa tuhuma za mauaji ya mfanyabiashara Abdulbasiti Abdallah (21), ambaye mwili wake ulikutwa ndani ya begi la nguo katika Jengo la Harbour View, Mtaa wa Samora. [45]
huyo
Alipoulizwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hawezi kuzungumzia kifo hicho kwani mtuhumiwa huyo hakuwa mikononi mwao. [46]
huyu
Nimeduwaa,ingawa sina ujanja na hivi sasa ninaelekea dukani nikanunue vitabu hivi, ili Miranda (mwanaye) aende navyo shule Jumatatu, anaeleza mzazi huyu. [47]
ikawa
Inawezekana ulihisi hivyo kutokana na mabadiliko uliyoyaona siku za hivi karibuni, au labda inaweza ikawa ni kutokana na kauli zake, ama umehisi mabadiliko katika mwenendo wake wa maisha siku za hivi karibuni. [48]
iko
Wakati Takukuru ikifikia maamuzi hayo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema kama Takukuru itahitaji msaada wa Wizara hiyo kumtafuta Liyumba iko tayari kutoa msaada huo. [49]
ila
Ninasema hayo kwa sababu nchi nyingi duniani zinakuza lugha zao na kunufaika sana kutokana na lugha kwani lugha ni utajiri mkubwa na sisi tunao utajiri huo wa Lugha ya Kiswahili ambao tumeukalia ila utajiri huo ukitumika ipasavyo utaitajirisha nchi kwa kutoa ajira kwa wataalamu wa lugha hiyo ambayo huzungumzwa pia na wananchi wa Kenya, Rwanda, Burundi, DRC na Uganda. [50]
ile
Mkutano huo unafanyika ukiwa na lengo kuu la kuchagua timu mpya itakayoibeba CUF kwa kipindi kingine cha miaka mitano kuanzia mwaka 2009 hadi mwaka 2014 baada ya ile iliyopo kumaliza muda wake. [51]
ili
Hata hivyo, Masha mwenyewe alikwisha kanusha taarifa hizo akisema hazina ukweli kwani hakuwa na lengo la kuingilia mchakato wa zabuni bali kunusuru hali ili mambo yasije kuharibika mbele ya safari. [52]
ilivyo
Viongozi wa Chaneta waombe udhamini kutoka katika mashirika na Kampuni mbalimbali ili kuendeleza vipaji vya mchezo huu mashuleni, waanzishe ligi za madaraja ya chini mpaka ya juu kama ilivyo wa soka hali ambayo kwa kiasi fulani itaibua ushindani na wachezaji mbalimbali watakuwa katika kiwango cha kuridhisha. [53]
imara
Hili lazima libadilike kama tunataka kuwa na uchumi imara duniani. [54]
ina
Akizungumzia Tanzania, Taifa Stars, Rajevac alisema ina nafasi kama timu nyingine kwa kuwa yoyote anaweza kuwa bingwa kama mwingine atateleza. [55]
ipo
Liyumba anakabiliwa na kesi ya kulisababishia taifa hasara ya Sh 221 bilioni ambayo ipo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. [56]
iwe
Akizungumza makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Msimbazi, Dar es Salaam jana, Mwina Kaduguda alisema timu waliyosajili ilikuwa si ya kimashindano bali walikuwa wanatimiza kanuni za shirikisho hilo ikizitaka kila klabu za Ligi Kuu iwe na timu ya vijana. [57]
japo
Tuliona ni busara tukashiriki katika mashindano hayo japo TFF ilitoa taarifa ya ghafla wakati timu yetu haikuwa na maandalizi yoyote huku pia tukiogopa kuondolewa katika Ligi Kuu na kutuingiza katika migogoro na TFF," alisema Kaduguda. [58]
je
Tunatakiwa kutengeza nyota wengine wapya kwani ni wazi kuwa wachezaji mahili wa mchezo huo hivi sasa umri unawatupa mkono je wakistaafu wapo watakaochukua nafasi zao au netiboli ndio itakuwa imefikia ukingoni. [59]
jibu
Liwalo na liwe, hili la uandishi wa vitabu sawa, matumizi ya mitaala ya aina moja, hakika wakubwa wetu mnazidi kutuchanganya zaidi na hatuelekei kupata dawa au jibu rahisi. [60]
jumla
Liyumba pamoja na aliyekuwa Meneja Miradi wa BoT, Deogratius Kweka wameshitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao katika mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo na kuisababishia hasara serikali jumla ya Sh221 bilioni. [61]
juu
WAKATI kukiwa na wingu zito juu ya upatikanaji wa mzabuni atakayeshughulikia utengenezaji wa vitambulisho vya uraia, mtaalamu mshauri wa serikali kuhusu mradi huo, Gotham International Ltd amejitokeza na kusema gharama za mtambo wa vitambulisho siyo zaidi ya Sh35 bilioni, lakini fedha zingine bilioni karibu 200 zitatumika kwa kazi mbalimbali zikiwemo za ujenzi wa ofisi. [62]
kabisa
Nilikuwa bado na uwezo mkubwa tu wa kusakata kandanda lakini sikuwa na jinsi, watu wengi waliniambia nikafanyiwe upasuaji wa goti lakini nilikataa nikaona ni bora niachane kabisa na soka. [63]
kabla
Chiku alisema siku moja kabla ya kwenda hospitalini hapo, akiwa nyumbani kwa dada yake eneo la Chamwino alikaa kusubiri siku za kujifungua, alitokea mtuhumiwa ambaye alijitambulisha kuwa ni mtoto wa baba mwenye nyumba na alitokea Mwanza ambapo alidai kuwa baba mwenye nyumba huyo alimzaa miaka mingi iliyopita na walikuwa hawajawahi kuonana. [64]
kama
SAKATA la kutoroka aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba, linaelezwa na viongozi wa upinzani kama la kisanii sawa na ilivyokuwa kwa Gavana wa benki hiyo marehemu Dk Daud Balali. [65]
karibu
Habari kutoka kwa jamaa wa karibu wa Komal zinadai kuwa amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia kitambaa cha kichwa (mtandio). [66]
kashfa
Inavyoonekana karibu viongozi wote wa serikali walipo madarakani hivi sasa wamechafuka kutokana na kashfa mbalimbali za utumiaji madaraka vibaya, uporaji wa raslimali za taifa, ndiyo maana hawezi hata kuwajibishana wenyewe. [67]
kasi
Mara kadhaa wamekuwa wakisimama badala ya kukaa wakati wakiwa kwenye mwendo wa kasi huku wakitoa ishara ya kuyataka magari yakae pembeni haraka na kuiruhusu Stars kupita bila ya kukumbana na bugudha ya foleni. [68]
kati
Vile vile sheria zitaboreshwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha usalama, kuboresha utaratibu wa kufanya kazi kati ya Watanzania na wadau wengine pamoja na kuweka sawa mfumo wa huduma kwa mteja," aliongeza Dk Kyaruzi. [69]
katibu
Nafasi zinazogombewa na wanachama mbalimbali wa chamahicho ni za Mwenyekiti na makamu wake, katibu Mkuu na wajumbe 45 wa Baraza kuu la uongozi la chama. [70]
kauli
Hata hivyo wakati zinatolewa kauli hizo, Kesi ya Liyumba inatarajiwa kutajwa tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam ambapo baadhi ya watu wanaamini anaweza kufika. [71]
ke
Chawote akashindwa kuvumilia, akaketi chini kabisa kwenye barabara ya vumbi akiangusha kilio kikubwa, awali kutokana na hasira za kufukuzwa na Binti Chande, Semeni hakutaka kumfuatilia shoga’ke, alizidi kukaza hatua bila kumjali Chawote aliyekuwa akilia kwa uchungu mkubwa baada ya kupiga hatua mbali-tatu huruma za kike zikamuingia, akageuka nyuma na kumtazama shonga’ke aliyemuangalia kwa sekunde kadhaa na hatimaye akaamua kumrudia, akaanza kumfariji. [72]
kiboko
Unajua, kabla ya kuja sisi kiboko alikuwa mnyama tu. [73]
kile
Vipengele ambavyo vimefanyiwa marekebisho ni pamoja na kile kinachohusu upatikanaji wa wagombea wa ubunge, uwakilishi na udiwani ambapo imependekezwa kuwa watapigiwa kura za maoni na wanachama katika majimbo yao," alisema Jussa. [74]
kimoja
Inawezekana tukatoka katika nafasi hizo za mbali katika viwango vya ubora wa soka Duniani kama tu viongozi wa TFF watakuwa kitu kimoja katika utendaji wao wa kazi, naamini hakuna linaloshindikana," anasema. [75]
kina
Kwa mujibu wa Jussa, chama hicho pia kina mpango wa kuongeza uwakilishi wa wanawake katika vikao vya maamuzi ili kwenda sambamba na matakwa ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kiuchumi Kusini mwa Afrika (SADC). [76]
kiwango
Kocha Marcio Maximo alijaribu kuwatoa Godfrey Bonny, Haruna Moshi na Jerry Tegete walioshindwa kuonyesha kiwango cha kuvutia na nafasi zao kuchuliwa na Nurdin Bakari, Musa Hassan Mgosi na Abri Kassimu. [77]
kocha
Wakati fulani kocha wa Stars, Marcio Maximo alijikuta akisema kwa sauti ya juu, "hongera sana" baada ya kuona askari mmoja akiwa ameachia mikono juu huku akiamrisha magari yaachie njia kikosi hicho cha Tanzania kisonge mbele. [78]
kombe
KOCHA wa Ghana, Milovan Rajevac raia wa Serbia amesema kikosi chake kina kila sababu ya kutwaa ubingwa wa michuano ya kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani kutokana na ubora walionao. [79]
kopo
Mwanamke aliyekamatwa kwa tuhuma za kumuiba mtoto huyo ni Beatrice Wapalila (38) mkazi wa mtaa wa Mtoni manispaa ya Morogoro ambaye alikutwa nyumbani kwake akiwa na mtoto huyo huku akimnywesha maziwa ya kopo aina ya Lactojen na maji ambapo alikaa na mtoto huyo kwa muda wa wiki mbili. [80]
kuacha
Mmoja wa mawakili hao wa utetezi, Majura Magafu aliiomba mahakama kutoa amri ya kuutaka upande wa mashitaka kuacha kuinyanyasa familia ya Liyumba na kwamba warudishe gari ya mmoja wa wadhamini ambayo waliikamata. [81]
kuandika
Ninaweza kukubaliana na mawazo au ushauri huo wa JK (Rais Kikwete) katika hili la kuandika na kutumia aina moja ya vitabu kwa shule zetu za Kitanzania hasa kwa kuwa shule zetu zinatumia mtaala mmoja. [82]
kufa
Kubadilika kwa mfumo wa uchumi wa nchini na kuingia kwa ubinafsishaji na makampuni mengi kufirisika kumepeleka timu hizo kufa hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka kwa mchezo huo hapa nchini. [83]
kufanyika
Lakini kiasi hiki ni kama asilimia 20 tu ya kile kinachostahili kufanyika. [84]
kufunga
Aliyataja maeneo mengine yatakayopewa kipaumbele cha matumizi ya fedha za mradi, ni pamoja na kujenga kituo cha taarifa za watu watakaosajiliwa, kununua kompyuta na kufunga mtambo utakaotunza utambulisho na kutoa vitambulisho. [85]
kuingiza
Mradi huu wa kuingiza Kiswahili katika matumizi ya kompyuta utawawezesha wazungumzaji wengi wa lugha hiyo kutumia kompyuta katika kazi zao za kila siku. [86]
kuitumia
Katika kuonesha haki, kwa hakika, benki zimeikubali na kuitumia Teknohama kwa kiasi fulani. [87]
kuitwa
Lakini sasa mambo ni mazuri kila mchezaji anapigana kwa nguvu zote ili aweze kuitwa katika timu ya Taifa kwa sababu wanapata kila kitu muhimu," anasema. [88]
kuja
Nionavyo mimi kama serikali haiwezi kujenga au kukodisha majengo nchi za nje , basi vituo hivyo vingeanzia katika ofisi zetu za ubalozi zilizopo katika nchi nyingi duniani na kuanza kufundisha watu wanaotaka kuja kutembea au kuishi Tanzania. [89]
kukuza
Kampuni ya Vodacom imeamua kudhamini shindano la Bongo Star search ikiwa ni moja ya mikakati yake ya kutaka kukuza vipaji kwa vijana katika nyanja mbalimbali za burudani. [90]
kuleta
Alisema kwa ujumla anaiomba Serikari na wapenzi wa soka nchini kuweza kuwaunga mkono kwa hali na mali kimawazo na hasa kiuchumi, ili kuweza kuipa mafanikio timu yetu ya Taifa na hii ikiwa ni njia pekee ya kuleta mafanikio kwenye timu. [91]
kuliko
Nina mpongeza sana Shyrose Banji kwa juhudi zake anazozifanya, lakini kama haya niliyoyasema atayafanyia kazi ni wazi kuwa mchezo huu utafika katika hatua nzuri kuliko ilivyo hivi sasa. [92]
kumpa
Hata hivyo, baada ya tamko hili wafanyakazi hao walifunga kikao hicho kwa muda bila ya kumpa nafasi Katibu Mkuu wao ya kuzungumza au kujibu hoja , lakini baadhi yao walidai alichotakiwa kufanya ni kujiuzuru na si vinginevyo. [93]
kupiga
AGIZO la Rais Jakaya Kikwete, kutaka kuwepo mpango wa kupiga kura za siri kufichua wahalifu wakiwemo baadhi ya waganga wanaochochea mauaji, limeanza kufanikiwa baada ya kuwepo kwa taarifa za baadhi ya raia kutoa taarifa sahihi zinazowahusu wahalifu hao. [94]
kusaidia
Alisema Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Dk Edward Hoseah ,anakaribisha watu ambao wanaweza kutoa taarifa au kusaidia alipo Liyumba ili aweze kukamatwa. [95]
kusoma
Ni mahali ambapo kusoma ni lazima, si kwa viboko bali kwa hamu ya kujua, nyenzo za kujua zikiwepo. [96]
kustaafu
Baada ya kuzitumikia timu zote zilizotajwa hapo juu alilazimika kustaafu kucheza soka kutokana na matatizo ya goti ambayo yalikuwa yakimsumbua mara kwa mara. [97]
kuu
Hata hivyo washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za mauaji hadi mahakama kuu. [98]
kwanza
Liyumba na Kweka walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza , Januari 27, mwaka huu kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali kiasi cha Sh 221 bilioni. [99]
kwao
Wee huyu mwenzako kwao ameaga kweli, mbona safari hii umeniletea mtu!” Binti Chande aliendelea tu kulalamika peke yake huku akimalizia kuchomoa kijiti cha mwisho, alipomaliza akanawa mikono na kuondoka hapo sebuleni, akaelekea chumbani. [100]
lake
Kwa mtazamo wangu, serikali inapoteza mapato mengi kwa kutolisaidia baraza lake la Kiswahili kuanzisha vituo vya utamaduni wa Tanzania katika nchi mbalimbali duniani au kuchagua nchi kadhaa za kuanzia mradi huo wa kuanzisha vituo vya utamaduni. [101]
langu
Lengo langu kubwa ni kuutazama mchezo wa netiboli ambao kwa asilimia kubwa wachezaji wa mchezo huo ni wanawake, lakini miaka hivi karibuni wanaume nao wameanza kucheza mchezo huu. [102]
leo
MKUTANO Mkuu wa nne na wa mwisho kwa awamu inayomaliza muda wake wa uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) unaaza leo Dar es Salaam, huku homa ya uchaguzi ikiwa imetanda miongoni mwa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti. [103]
letu
Tatizo ninaloliona mimi ni jinsi serikali inavyozisaidia idara na taasisi zake katika kujitanua na kutengeneza ajira ambazo zingesaidia kulinufaisha taifa letu. [104]
ligi
Kaduguda alisema ligi ijayo ya vijana kama itakuwepo, watahakikisha wanaiandaa timu mapema kwa kushirikiana na kocha Mzambia Patrick Phiri kuimarisha kikosi hicho cha vijana. [105]
lingine
Dk Kyaruzi aliainisha eneo lingine la matumizi ya fedha hizo kuwa, ni pamoja na kutumika kununulia mitambo kwa ajili ya kuhifadhia kumbukumbu za RITA kwa upande wa Bara na Ofisi za Msajili kwa upande wa Zanzibar. [106]
lipo
Nimeanza uchambuzi wangu kwa kujaribu kueleza jitihada zinazofanywa na baraza hilo kwa sababu ninatambua kuwa lipo chini ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo katika Idara ya Maendeleo ya Utamaduni. [107]
lugha
Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Microsoft limesanifu istilahi (maneno ya kitaalamu) za kompyuta 1,958 ambazo zitatumika kufasili misemo ya kikompyuta kwa lugha hiyo (Kiswahili). [108]
maadili
Ni wazi kwamba, kuporomoka kwa maadili ya uongozi sasa kumeshika kasi ya kutisha na inahitajika gharama kubwa kuirejesha nchi katika misingi ya maadili aliyojenga Mwalimu Nyerere. [109]
maelezo
Kwa nyakati tofauti, Mwananchi Jumapili ilipotaka maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna wa Polisi, Robert Manumba na Naibu wake, Peter Kivuyo wote walipata kigugumizi kuzungumzia suala hilo. [110]
makini
Taifa Stars iliyoanza mchezo huo vibaya kwa safu ya ulinzi kushindwa kulewana vizuri na kuacha mipira ya juu kutawaliwa na washambuliaji wa Senegal waliokuwa makini zaidi kutumia mwanya huo. [111]
maombi
Akizungumza na Mwananchi Jumapili Waziri wa Wizara hiyo, Lawrance Masha alisema wakipewa maombi ya kumtafuta Liyumba, watasaidia kumtafuta kwa kuwa wote ni Serikali. [112]
mazito
Sikatai sheria ya elimu inaruhusu viboko lakini kwa masharti mazito sana. [113]
mbaya
Hivi karibuni, wakili wa Lema aliomba ruhusa kwa Jaji Salum Masatti kwenda gerezani kumuona mteja kama angeweza kwenda kortini kujitetea na aliporudi alisema hali yake ni mbaya lakini hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa kuhusu matibabu yake. [114]
mbio
WATANZANIA watatu wameng'ara mbio za magari za Pirell mashindano ambayo yaliwashirikisha madereva wenye umri mdogo walioshiriki mbio hizo zilizofikia kikomo jana katika Jiji la Dar es Salaam. [115]
mbona
Tunahisi serikali inajua kinachoendelea, hapa lazima itueleze itachukua hatua gani kwa wahusika, mbona hawakamatwi?" alisema Dk. [116]
mfupi
Msangi alisema kuwa Februari 21 majira ya saa 5 asubuhi walipata taarifa kutoka kwa raia mwema mmoja ambaye aliwaeleza polisi kuwa kuna mwanamke ambaye alikuwa akimtilia mashaka na kumtuhumu kuwa ameiba mtoto huyo kwani alionekana akimnywesha maziwa ya kopo na maji na kwamba mwanamke huyo hakuwahi kuonekana na ujauzito na kuongeza kuwa mwanamke huyo alitoweka nyumbani kwake hapo kwa muda mfupi na kurudi na mtoto huyo. [117]
mgeni
Mkutano huo unafanyika chini ya mgeni rasmi Msajili wa Vyama vya Siasa nchini John Tendwa na kuhudhuriwa na Mabalozi wa nchi mbalimbali, wajumbe kutoka vyama vyote vyenye usajili wa kudumu, Asasi za Kiraia (Azaki) na wasomi. [118]
mia
Uliziangalia hizo dalili ukawa na uhakika wa asilimia mia moja kuwa anakutenda. [119]
michuano
Mbali na hilo, kikao hicho kitajadili ushiriki wao katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Bara ambapo timu hiyo imebakiza michezo saba kuhakikisha wanapanga mikakati ya kupata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya Kimataifa. [120]
mikoa
Taarifa za awali zilizolifikia gazeti hili zilisema kazi hiyo imeanza kwa mafanikio na kwamba kamati za ulinzi na usalama ngazi ya mikoa na wilaya zinaendelea vizuri na kazi hiyo. [121]
mimba
Akizungumza juzi katika maadhimisho ya miaka 10 ya Mpango wa Habari za Afya wa Femina (Femina HIP), yaliyofanyika katika viwanja vya Biafra Kinondoni jijini Dar es Salaam, Sitta alisema wazazi wakizungumza na watoto wao itasaidia pia kupunguza mimba mashuleni. [122]
mimi
Ndiyo, sijui kitu kwani wakati huo tukio linatokea mimi nilikuwa upande wa trafiki hivyo sina ninalojua. [123]
mji
Ghana iko kundi B lililo katika mji wa Bouake Kilomita 400 kutoka jiji maarufu zaidi nchini hapa la Abidjan. [124]
mjini
Hivyo alirudi nyumbani ambako pia hakumkuta mtuhumiwa na ndipo aliporipoti katika kituo kikubwa cha polisi mjini hapa na kutoa taarifa za kuibwa kwa mtoto huyo. [125]
mkali
Kuingia kwa bao hili kulirudisha hali Stars kujaribu kufanya mashambulizi mengi kupitia kwa winga wake Mrisho Ngassa aliyekuwa chini ya ulinzi mkali wa ngome ya Senegal. [126]
mkazo
DAKTARI wa Taifa Stars, Juma Sufiani amechukua uamuzi wa kubadili chakula watakachokuwa wanakula wachezaji wa timu hiyo ikiwa ni pamoja na kutilia mkazo kupikwa kwa uangalifu mkubwa. [127]
mkutano
Musa aliongeza kwamba, baada ya mkutano huo, wahalifu hao waliogopa na kulirejesha gari hilo Dar es Salaam na kuliacha katika nyumba ya mama yake eneo la Kipunguni na kwamba ndani ya basi hilo walivikuta vitu mbalimbali vya kishirikina. [128]
mkuu
Akifafanua, Musa alisema mpango huo ambao uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Kondoa na timu ya usalama, umewezesha kupatikana gari hilo baada ya kuwabaini wezi ambao walitaka kulipeleka basi hilo Kiteto. [129]
mno
Ingawa baadhi ya watu wanadai kuwa nchi hii imevurugwa mno katika kipindi cha awamu ya kwanza kiasi kwamba, hadi sasa haijulikani pa kuanzia kuisafisha, nasema hoja hiyo si kweli. [130]
moyoni
Leo spendi kupoteza muda kuamkia hapa kwani niliyonayo ni mengi moyoni nataka niyatue hapa. [131]
mrefu
Serikali inadai kuwa na mkono mrefu haikufanya lolote, sasa kwa Liyumba wameanza. [132]
mtaala
Nimeduwaa, kwani sielewi ni wapi tunakwenda hasa kwenye elimu ya watoto wetu wa Kitanzania ambao kwa sasa wanafundishwa kwa mtaala mmoja, ambao umeandaliwa na kuandikiwa vitabu na Wakenya, Wamalawi , Waganda, Wahindi na wengineo. [133]
mumeo
Unakumbuka nilitaja dalili ambazo zinaweza kukuhakikishia kuwa mumeo ana mwanamke nje. [134]
mwake
Muda mfupi baadaye alrejea na kunyoosha mkono wake, kiganjani mwake alifumbata kitu ambacho hakikujulikana mwanzoni. [135]
naamini
Hakuna shaka kwamba wale wengi au wachache kati ya wasomi wetu, wakiwamo maprofesa ambao kwa namna moja au nyingine walikuwa wamekwamishwa au kukwazwa na matatizo kama hayo, naamini sasa wamepata mwanya. [136]
najua
Kama umfuatiliaji najua, unajua kuwa wiki iliyopita nilikuahidi kukuletea muendelezo wa makala hii. [137]
nao
Aliongeza kuwa baada ya kutoka chooni akiwa na kinyesi kwa ajili ya kupimwa alitoka nje ya hospitali hiyo na hakufanikiwa kumuona mtuhumiwa, hivyo alirudi ndani ya hospitali na kuwauliza wagonjwa wenzake waliokuwa wakisubiri matibabu, lakini nao hawakufahamu mahali alikoelekea mtuhumiwa. [138]
navyo
NIMELETEWA orodha ndefu ya vitabu ambavyo mwanangu anayesoma darasa la kwanza katika shule ya msingi anatakiwa kuwa navyo. [139]
nayo
Baada ya mtaji kukua niliamua kufungua duka la kuuza vifaa vya michezo biashara ambayo naendelea nayo mpaka hivi sasa, namshukuru Mungu kwani nakabiliana na maisha kama kawaida," anasema. [140]
nazo
Akiizungumzia michuano migumu kwa timu ya Taifa kwa wachezaji wa ndani yaani 'CHAN' Swed ameiona ni ya kawaida kwa jinsi wanavyofanya maandalizi mazuli kulingana na timu yao na wanazichukulia ni timu za kawaida kama timu zozote wanazocheza nazo siku zote. [141]
ndiko
Akizichezea timu mbalimbali nchini zikiwemo Vijana Ilala ambako ndiko alipoanzia kuonekana katika ulimwengu huu wa soka na kuahamia Cargo FC na Pan Afrika zote zikiwa za jijini Dar es Salaam. [142]
ndio
Alisema vijana na watoto ndio nguvu kazi ya taifa na kwamba taifa haliwezi kuendelea iwapi litendelea kupoteza nguvu kazi hiyo. [143]
ndiyo
Naye Mwenyekiti wa TUICO Taifa Omary Juma alipoulizwa alisema huo ndiyo mtizamo wa wanachama wao, lakini si kweli kwamba uongozi uliwadharau bali kilichofanyika kutofautiana kwa uelewa. [144]
ngozi
Mpango wa kupigiwa kura za siri wahalifu ulifafanuliwa pia na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye pamoja na kuwalilia watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) , alisema kura za siri zitafanyika kwa siri na uhakika na kwamba taarifa zinakusanywa Machi mwaka huu. [145]
ni
Katika gari hilo pia kulikutwa na mfuko mdogo wa Rambo uliokuwa na kandambili zinazodaiwa kuwa ni za marehemu, nguo, kisu na bomba la sindano. [146]
nia
JKT inayoundwa na wachezaji kama Evodia Kazinja,Lulu Joseph,Doritha Mbunda na Elizabeth Masenyi imedhihirisha kuwa Tanzania inaweza kupambana katika mashindano yoyote yale kama wachezaji wakiweka nia. [147]
nikiwa
Mwaka 2003 nikiwa na timu ya soka ya Mafunzo ya Zanzibar, niliamua kustaafu kucheza soka kutokana na matatizo ya goti ambayo yalikuwa yakinisumbua kila wakiti. [148]
nina
Sitaki kusema tuige kwa Waingereza, ila ninachosema lugha ya Kiswahili ikitumiwa vizuri kwa kuanzisha vituo katika nchi mbali mbali kwa mfano Urusi, Marekani, Uingereza, Ethiopia, Ujerumani, nchi za Scandinavia na nchi za Mashariki ya Kati nina hakika taifa letu litapata mapato makubwa na kutoa ajira nyingi kwa wataalam wetu wa Kiswahili. [149]
nini
Alisema kiwango hicho cha fedha ni kikubwa, hivyo suala hilo wameamua kulipeleka kwa Kamati ya Utendaji ili kukaa na kutafakari nini cha kufanya. [150]
nono
Lakini kauli ya viongozi wa kambi ya upinzani imekuja wakati Jeshi la Polisi likisisitiza msimamo wake kwamba, halimtafuti Liyumba wakati Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ikitangaza donge nono kwa mtu atakayewezesha kupatikana kwa mtuhumiwa huyo. [151]
nyinyi
Lakini kwa kuwa nyinyi nyote mnapendwa kuitwa mabwana siku hizi, haya basi. [152]
pa
Lakini walimu hawakufundisha kwa sababu ya viboko Bwana! Kilichosaidia enzi zile ni kwamba ilieleweka kwamba shule ni mahali pa madawati, na vitabu. [153]
peke
Enzi zetu tulikuwa mabwana peke yetu. [154]
pekee
Katika nafasi ya mwenyekiti vigogo watatu wanawania nafasi hiyo ambao ni Profesa Abdallah Safari, Profesa Ibrahimu Lipumba na Steven Masanja wakati Makamu Mwenyekiti wa sasa Machano Khamis Ali na Katibu Mkuu wa sasa Maalim Seif Sharif Hamad wakiwa wagombea pekee katika nafasi zao. [155]
rais
Mshambuliaji Given Singuluma ndiye aliyekuwa shujaa wa mchezo huo kwa kufunga mabao yote matatu ya Zambia katika dakika ya 36,47 na 76, kuharibu sherehe zote za ufunguzi mbele ya rais Laurent Gbagbo wa Ivory Coast. [156]
saa
Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashitaka Emma Mkonyi mbele ya Hakimu Mkazi Eva Nkya kuwa, Februari 2 mwaka huu saa 3:15 usiku katika mtaa wa Kipata Kariakoo, washitakiwa walimuua Abdallah. [157]
sarafu
Baada ya hapo mwanadamu akagundua kuwa anaweza kutumia karatasi au sarafu kuwakilisha fedha fulani. [158]
shule
Waziri Sitta aliitaka Femina kushirikiana na wizara yake ili kuzifikia shule zote 3983 za sekondari zilizopo Tanzania. [159]
si
Hivyo, ni lazima ieleweke wazi kuwa fedha hizo zitafanya kazi nyingi sana na ukiangalia utakuta gharama za mtambo wenyewe si' zaidi ya shilingi bilioni 35," alisi'sitiza. [160]
sio
Ukiangalia mechi ilikuwa ngumu sana na tumepishana goli moja hivyo sio mchezao, lakini tuliwakamata hasa na tukasma iwe isiwe kombe lazima libaki Tanzania tunashukuru tumefanikiwa" alisema Shayo kwa furaha. [161]
sisi
Juzi nilitoa tamko kuwa hatujaletewa maombi ya kumtafuta, lakini Takukuru wakituletea tutafanya hivyo, kwa kuwa sisi ni Serikali," alisema Masha. [162]
tatu
Siku moja baada ya kuwasili jijini hapa, Bonny alilazimika kwenda kujisaidia zaidi ya mara tatu wakati wa mazoezi ya kwanza ya timu hiyo, lakini hali hiyo baadaye ikamkuta Nurdin na baadhi ya wachezaji walianza kulalama kuumwa na matumbo. [163]
tu
Kati ya wagombea hao tunahitaji wajumbe 45 tu watakaoviendesha vikao vya Baraza kuu la uongozi ndani ya kipindi cha miaka mitano, 25 kutoka Tanzania bara na 20 kutoka Zanzibar" anasema Joram Bashange Naibu Mkurugenzi wa oganaizesheni. [164]
tuanze
Haya tuanze wapi? Najiuliza kila siku. [165]
uchungu
Mcharaza acharazwe ili akumbuke uchungu wa matako. [166]
ukawa
Akiwa shuleni hapo Mtwa aliweza kug'ara zaidi katika timu ya shule, baada tu ya kumaliza masoma yake alijiunga na timu ya soka ya Vijana Ilala na huo ndio ukawa mwanzo wa safari yake katika soka. [167]
uko
Nikasema inawezekana kwa asilimia kubwa kuwa ukawa uko sawa kabisa. [168]
ule
Hapa kuna mchezo kama ule wa Balali ambapo serikali ilizembea kwa makusudi na kumwacha akaenda Marekani ambapo hakurudi. [169]
umma
Mchezo huu hivi sasa umepoteza mwelekeo tofauti na ilivyokuwa katika miaka ya 1970 hadi mwanzoni mwa miaka ya tisini kulipokuwa na timu nyingi za mashiriki ya umma na serikali zilizokuwa tishio kama Bora, Reli, Tanesco, Bima, NBC United na nyinginezo nyingi zilikuwa na wachezaji mahili. [170]
umri
MTOTO mchanga Issa Shabani mwenye umri wa siku 10 aliyeibiwa wiki mbili zilizopita katika hospitali ya Upendo jirani na hoteli ya Mount Uluguru, Manispaa ya Morogoro hatimaye mwishoni mwa wiki hii amepatikana na mwanamke mmoja amekamatwa kwa tuhuma za kumuiba mtoto huyo. [171]
una
Inadaiwa kuwa amekufa kwa mateso, kwa sababu mwili wake umeharibika kwa mateso na una makovu mengi," kilidokeza chanzo cha habari. [172]
utendaji
Alisema shughuli nyingine za mkutano huo ni kupokea taarifa ya utendaji wa chama ya miaka mitano iliyopita na kupitisha marekebisho ya katiba. [173]
utu
Nyie, endeleeni na maombi yenu kwa watakatifu, wana masikio wanasikia na si kama wa kwetu ambao wamegeuka walafi, mafisadi na wasaka tonge ambao chembe ya utu imetoweka mioyoni mwao. [174]
vyuo
Ninafahamu serikali yetu ina mikataba na nchi mbalimbali za kubadilishana wataalamu wa elimu, ambapo wapo walimu wetu wa Kiswahili wanaofundisha katika vyuo vikuu mbalimbali ulaya, Asia na Marekani. [175]
wageni
Aliwataka watu kuwa watulivu ili kutoa nafasi kwa washiriki wa CHAN kuonyesha walichonacho hasa kwa wenyeji na wageni hadi siku ya mwisho apatikane bingwa anayestahili. [176]
wagumu
Shoga Wanaumme ni wagumu kukubali unapojaribu kuwakabili katika hili suala tena bila vithibitisho vya uhakika. [177]
wako
Kuna wananchi tumesikia wako tayari kuisaidia Takukuru, tunawakaribisha na Dk Hoseah anawakaribisha ili waweze kutusaidia na donge nono litatolewa kwa atakayesaidia kukamatwa kwa Liyumba," alisema Kapwani. [178]
wale
Lakini pia nitabadili kidogo ili wachezaji wale vyakula walivyozoea na walivyokuwa wakila nyumbani kitu ambacho kitawafanya wawe katika hali ya kawaida," alisema daktari huyo mahiri katika mambo ya uganga wa michezo. [179]
walianza
Naye Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya jinai Mkoa wa Morogoro, Ahmed Msangi alisema kuwa baada ya kupata taarifa za kuibwa kwa mtoto, polisi walianza upelelezi ikiwa ni pamoja na kuwaomba raia wema kutoa taarifa zitakazosaidia kupatikana kwa mtoto huyo. [180]
wameharibika
Watoto wameharibika kwa sababu walimu wameharibika. [181]
wanapiga
Na hasa kwa walimu! Wao wanapiga viboko kila siku kama mtoto hafanyi kazi. [182]
wao
Katika hatua nyingine, Gotha International imekanusha habari kuwa wamepewa kazi hiyo ya ushauri kwa kupendelewa na kwamba hawana sifa hizo na kujigamba, wao wana sifa zote na si kweli wameteuliwa kwa upendeleo. [183]
wapi
Hivi sasa hakuna vipaji vipya katika mchezo wa netiboli hata wachezaji wengi wanaocheza mchezo huu pia ni wachezaji wa mchezo wa kikapu na wanashiriki katika Ligi ya mchezo huo mkoa wa Dar es Salaam, Kili RBA hali inayosababisha usumbufu wakati michuanio ya netiboli na kikapu inapokuwa inafanyika kwa wakati mmoja kwani wapo wachezaji hulazimika kuchagua wacheze wapi, sasa hapa tunajenga tunabomoa. [184]
wasi
Unaweza ukutane na namba ambayo ameisevu kwa jina la kiume, lakini ukawa na wasi wasi nayo, tafuta simu nyingine weka private namba kisha piga, sikiliza sauti inayopokea. [185]
we
Akifika shuleni na kuona mwalimu hafundishi vizuri, we! Yule mwalimu alipigwa viboko hadi alilazimika kusimama darasani mwezi mzima maana tako halitaki kugusa kiti wala kitu. [186]
wema
Kupatikana kwa mtoto huyo ambaye aliibiwa Februari 12 mwaka huu, majira ya saa nne asubuhi kunafuatia ushirikiano mzuri wa raia wema ambao walitoa taarifa polisi zilizifanikisha kupatikana kwa mtoto huyo akiwa hai na afya njema. [187]
wengi
Wakati kukiwa na utata huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Gotham International Dk John Kyaruzi, alisema jijini Dar es Salaam kuwa tofauti na watu wengi wanavyodhani, mradi huo unahitaji kuangalia mambo mengi na utaalamu wa hali ya juu. [188]
wenu
Niwieni radhi nyote, hasa wale waumini ambao wanaamini na kuwaomba watakatifu wenu walioko mbinguni ambao asubuhi, mchana na usiku huwaelekezea shida zenu. [189]
wenyeji
Amewataka kuchukua kombe ili kuweka historia kwa kuwa michuano hiyo inafanyika Afrika kwa mara ya kwanza na wao ni wenyeji. [190]
wetu
Wazazi wenzangu tukiwapatia watoto wetu uwezo wa kujiamini, taarifa za ukweli juu ya haki, jinsia, kukua na kujikinga na VVU, tutakuwa tumewapatia zawadi kubwa. [191]
wote
Alisema kutokana na sababu hizo pamoja na mambo mengine wanatoa tamko moja la kuwataka viongozi hao wajiuzuru nafasi zao mara moja kwa maslahi ya wanachama wa NBC pamoja na wanachama wote wa TUICO nchini. [192]
yahoo
Zill20032000@yahoo. [193]
yako
Wengine waliolalamikia chakula ni viongozi wa Senegal ambao waliiambia Mwananchi hawajavutiwa na chakula hicho ingawa walipoongeza maandalizi mengine yako katika mpangilio mzuri unaowafanya wawe katika hali nzuri ya kufanya vizuri. [194]
yale
Si ajabu yakawa yale yale kwani naye bila shaka ana siri nzito," alisema Lipumba. [195]
yao
Mwenyekiti wake Jack Gotham, alisema wamepewa kazi hiyo kwa mujibu wa sheria na wao wanafanya kazi hiyo kwa umakini na kuzingatia taaluma yao na kuongeza kuwa, hadi hivi sasa wameshapata kazi nyingi nje ya nchi za ushauri wa kitaalamu kuhusu miradi ya vitambulisho. [196]
yetu
Tunatoa tamko rasmi la kuwataka mjiuzuru nafasi zenu mara moja, kwa maslahi ya wanachama na Chama chetu kwa ujumla na kama hamtafanya hivyo tutasitisha michango yetu kwa muda na kuwaomba wanachama wengine wa TUICO watuunge mkono kwa hili" vahahula alifafanua zaidi juu ya suala hilo. [197]
yeye
Akizungumzia tukio hilo, mama mzazi wa mtoto huyo Chiku Said (25) mkazi wa Pangawe alisema kuwa aliibiwa mtoto akiwa katika hospitali hiyo ambako alikwenda kupata matibabu baada ya yeye mwenyewe kusumbuliwa na maradhi ya tumbo ambayo yalimpata baada ya kujifungua. [198]
yule
Ili kupata wachezaji bora wa netiboli inatakiwa maandalizi ya kutosha ikiwa ni pamoja na kuandaa ligi mbalimbali zenye ushindani zitakazoa wachezaji wazuri kwani mchezaji bora katika timu ya taifa ni yule anayefanya vizuri katika klabu yake. [199]
zima
Kauli za vigogo hao wawili wa polisi zinazidi kuongeza wingu katika suala zima la kuwatafuta watuhumiwa hao. [200]