Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-01-07

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


ama
Imekuwa ni kawaida kuwepo kwa kila aina ya upinzani wa ushabiki katika vyama vyetu, lakini kauli ya Mwinyi inawakumbusha viongozi wetu kuwa wananchi wanachotaka ni sera na si manjonjo wawapo jukwaani na vitisho vya kuchafuana bila sababu ya msingi, uwezo wa mtu ama chama upo katika sera na ndio wananchi wanachotaka kusikia. [1]
ambao
Kaimu katibu mkuu wa UWT, Domina Ngwada alisema jana kuwa jumla ya wajumbe 905 watahudhuria mkutano huo, ambao pia umealika wawakilishi wa vyama vingine vya siasa pamoja na mabalozi. [2]
ambapo
Simba inayoendela na mashindano hayo yatakayomalizika Januari 12, tayari imeshacheza mechi mbili ambapo imetoka sare moja na kufungwa moja. [3]
ana
Alisema anajiamini kuwa ana uwezo wa kutosha wa kuwa kipa bora na kuongeza kuwa anatarajia kocha wake Patrick Mwangata atampa mbinu tofauti za kulinda lango lake na hatimaye kuwa kipa bora. [4]
anasema
Maximo anasema kwamba timu imara zinakandamizwa na mazingira ya viwanja vibovu na ndio maana mpaka sasa mechi zinazochezwa kwenye uwanja wa Namboole ndizo ambazo zimekuwa zikichezwa kwa kiwango stahili. [5]
au
Ewura imetangaza kuwa bei ya mafuta aina ya petroli iuzwe kwa Sh1,166 kwa lita na dizeli iuzwe Sh1,271 na kwamba uamuzi huo utatangazwa kwenye Gazeti la Serikali ili kila mfanyabiashara atakayekiuka, akumbwe na adhabu ya faini ya Sh3 milioni, au kunyang'anywa leseni au adhabu zote kwa pamoja. [6]
bahati
Kwa bahati nzuri tunayo machimbo ya fosfeiti huko kaskazini mwa nchi karibu na Ziwa Manyara. [7]
bali
Akizungumza na waandishi wa habari jana Afisa habari wa shirikisho hilo Florian Kaijage alisema tayari wameandika barua kwa CECAFA kuelezea matatizo yao na matarajia yao ni kuona hali hiyo inarekebishwa mapema na si kwa michezo ya Kilimanjaro Stars pekee bali ni katika michezo yote itakayochezwa. [8]
barabara
Wanahitaji huduma za afya, elimu, maji, umeme na barabara. [9]
bidhaa
Lakini hivi sasa mafuta yanauzwa kati ya Sh1,450 na 1,600 kwa petroli na dizeli kutoka Sh1,300 hadi 1,500, licha ya maafisa wa Ewura kukutana mara kadhaa na wafanyabiashara wa bidhaa hiyo ambao wamekuwa wakidai kuwa hawawezi kupunguza kwa sababu waliyanunua bei ikiwa juu katika soko la dunia. [10]
bonde
IWRM inaelezea jinsi gani mataifa manane yanayotumia bonde hilo - Angola, Botswana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Zambia, Tanzania na Zimbabwe yanaweza kugawana faida zinazotokana na rasilimali zake kwa usawa. [11]
chote
Kinyume na ilivyotarajiwa na watu wengi, mzee Mwinyi aliwataka wananchi kuchagua mgombea ambaye wanaona sera zake zinafaa katika kuwaletea maendeleo na kuwasisitizia kuwa na umoja na mshikamano katika kipindi chote cha pilika pilika hizo za uchaguzi. [12]
dhahma
Profesa Aida Isinika kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine anasema, dhahma ya chakula na mafuta inayoikabili Tanzania inatokana na kupanda kwa gharama za usafiri na uzalishaji mdogo wa chakula ndani ya nchi. [13]
dua
Akizungumza na waandishi wa habari waliomtembelea nyumbani kwao wakati wa dua ya kumshukuru Mungu baada ya binti huyo kuonekana, Seleman Sheshe, 70, ambaye ni babu wa Sakina, alisema hawaamini kama binti yao amerejea. [14]
duni
Mkakati huo wa IWRM unaangalia masuala manne, ikiwa ni pamoja na uratibu wa rasilimali maji, mifumo mizuri ya kusimamia mazingira, hatua duni za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa na ushirikiano dhaifu wa kikanda na njia za kuungana. [15]
endapo
Zanzibar bado ina nafasi ya kusonga mbele endapo ikishinda mchezo wake dhidi ya Rwanda ijumaa, lakini itategemea na matokeo ya timu zingine. [16]
es
Sophia Simba, ambaye aliripotiwa kukwaruzana na Kahama wakati wa kikao cha CCM mkoa wa Dar es salaam, hakuweza kupatikana na mara kadhaa alipopigiwa simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita kw amuda mrefu na ilipopokelewa ilijibiwa na mtu aliyejitambulisha kuwa msaidizi wake akisema kuwa Simba hana nafasi kwa sababu alikuwa akisaidia majeruhi. [17]
eti
Haya, haya, haya, wapo ambao wamediriki hata kutuita sisi waishiwa kuwa ni mafisadi, eti tumekunywa na kunywaga ushuru wa watu hadi asubuhi siku ya mwaka mpya. [18]
foleni
Kumbe jamaa mwenyewe alikuwa anatafuta nishani ya kiatu peke yake kwa kujaribu kuzuia kila gari linalotaka kuruka foleni. [19]
fulani
Siyo ile tu nyingi amezitoa ambazo ukiangalia unaona alikuwa na matakwa yake au ya watu fulani, ili timu zao zisonge mbele. [20]
gani
Mpira gani huu? Haina maana, huwezi kujua kwamba timu ni nzuri au ni mbaya kwa mtindo huu. [21]
gesi
Pamoja na fosfeiti pia tunayo gesi ya asili ambayo nayo tutaweza kuzalisha mbolea aina ya urea na ammonia. [22]
hadi
Maafisa hao walisema kuwa kwa sasa wameunda baraza maalum la mpito kwa ajili ya kuendesha kundi hilo la waasi hadi itakapoamuliwa vinginevyo, huku msemaji wao, Kamanzi Desire akisema kuwa baraza hilo litahakikisha mazungumzo ya amani yanaendelea. [23]
haina
Nafasi ya makamu mwenyekiti ikiwa haina mvutano mkali kwa kuwa na mgombea ni mmoja pekee, Asha Bakari Makame. [24]
haja
Aliporudi hivi karibuni, tulipata habari kuwa katika chumba alichokuwa amefungiwa alikuwa akimaliza haja zake zote humo humo ndani. [25]
hao
Wajumbe hao, ambao walikuwa wakitumia gari binafsi kutoka Manyara walipata ajali hiyo na kuumia vibaya, akiwemo katibu muhtasi aliyetolewa jicho moja. [26]
hasa
Katika uzinduzi huo kumetokea kitu fulani tofauti na kilichozoeleka kwa miaka mingi katika medani za siasa hapa nchini, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linapaswa kuigwa kwani ndio msingi hasa wa demokrasia ya kweli. [27]
hasara
Jambo hili linaisababishia serikali hasara kubwa ilhali viwanda vichache vilivyopo vikikabiliwa na uhaba mkubwa wa nishati hiyo kwa uzalishaji. [28]
hata
Siwezi kuzungumza mengi unajua ninaumwa kikohozi na hata daktari wangu alinishauri nisifanye hivyo, lakini kwa ufupi ni kuwa nasubiri kuthibitishwa kutokana na ukweli kuwa mimi nilishachaguliwa na Mungu tangu muda mrefu. [29]
hawa
Lakini nikaja kugundua kuwa ile ya wale kuongea ndiyo dawa yenyewe tofauti tu ni kwamba huenda hawa watu hawakuwa wawazi baina yao wakiwa pekee yao, labda mmoja alishindwa kujieleza. [30]
hawezi
Sasa narudia kusema; usiogope kumwambia mwezako unavyotaka akufanyie kwani asipofanya usimlaumu kwa kuwa hawezi kujua. [31]
hayo
Tofauti nyingine kubwa iliyokuwepo katika maeneo hayo ni pamoja na sare za kijani ambazo ni vazi rasmi kwa Wana-CCM halikutamba sana jana na wajumbe wengi walivalia nguo za rangi za kawaida, tofauti na hali inavyokuwa wakati jumuiya nyingine zinapokutana na kuufanya mji huu kufunikwa na kijani na njano. [32]
hii
Uamuzi wa Ewura umekuja baada ya mamlaka hiyo kukutana na wafanyabiashara hao juzi kuzungumzia mwenendo wa bei ya mafuta jijini hapa baada ya mamlaka hiyo kuwataka wauzaji kushusha bei ya mafuta kuanzia Jumatatu wiki hii. [33]
hiki
Huyo baba yake ni mkazi wa kijiji hiki mwenye asili ya Mkoa wa Mbeya. [34]
hili
Zoezi hili la kukusanya kura za maoni kwa wananchi, ili kuweza kubaini wahusika sugu wa mauaji haya, ni moja ya mchakato uliopangwa na serikali kwa mwaka huu, katika hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ya kufunga mwaka aliyozungumza na Taifa wiki jana. [35]
hilo
Ewura pia imesema iwapo tangazo la Mwanasheria Mkuu litaeleza kuwa utekelezaji wa agizo hilo la kuuza mafuta kwa bei mpya unaanza Januari 5, basi wale ambao wanaendelea kuuza mafuta kwa bei ya zamani, watachukuliwa hatua kama zilivyoelezwa. [36]
hizi
Kama utafanikiwa kutoa huduma hizi hasa maji safi na salama karibu na nyumbani kwake, ni wazi kuwa utaboresha maisha yake na mtu huyu atakuwa na maisha bora. [37]
hoteli
Anaitaja miundombinu ya huduma ambayo haitoshelezi mahitajji kuwa ni pamoja na kituo cha Msamvu, soko na hospitali na kukosekana kwa hoteli ya kisasa ambayo itaweza kuwa na ukumbi wa mikutano ya kawaida na ile ya kimataifa. [38]
huduma
MGANGA wa kienyeji, John Lupimo (41), amepandishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive kwa tuhuma za kuendesha huduma ya zahanati na maabara na kutoa dawa za serikali bila leseni ya huduma hizo. [39]
huko
Baada ya kupotea, tulifuatilia sana na hata mama yake mzazi alifika huko alikodaiwa kuwepo, lakini hakukuwa na dalili zozote za kumpata. [40]
huwa
Kwa kweli tumetoa uhuru wa kutosha kwa Mkaguzi Mkuu wa Serikali katika kufanya ukaguzi wa matumizi ya serikali na kwamba pale idara hiyo inapotoa taarifa yake huwa nawaita na kuwaambia kuwa hii ndiyo taarifa ya ukaguzi inayoelezea utendaji wetu. [41]
huyo
KItendo cha kamanda huyo kilifanya waasi hao kukutana katika kikao cha dharura muda mfupi baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa baadhi ya maafisa wake wamemuondoa kwenye uongozi. [42]
huyu
Kinachonivutia kwa mzee huyu ambaye katika kipindi chake cha uongozi ndipo mageuzi ya mfumo wa vyama vingi yalipoingia hakuonekana kutetereka na baadhi ya vitisho kutoka kwa vyama vingine vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi huo kuwa vitamchafua. [43]
ikiwemo
Vyombo vya dola vinatakiwa kuwa makini, kuchunguza wakati zoezi hili la kutoa kura za maoni litakapoanza ili kuondoa malalamiko kwa baadhi ya watu, ikiwemo kuchafuliana majina kutokana na kutokuwa na uthibitisho wa kutosha kwake," alisema. [44]
ile
Profesa Maghembe alisema Jimbo lake limeshuhudia ajali mbaya sana ikiwamo iliyohusisha basi la Buffalo iliyoua abiria 22 na ile iliyoua mapadri na watawa wa kanisa katoliki ambazo zote zilitokana na uzembe wa madereva. [45]
ili
Akizungumza katika Mwananchi kwenye viwanja hivyo, Joyce Maunga alisema kuwa hana shaka na mgombea yeyote atakayechaguliwa ili mradi anatokea ndani ya chama hicho. [46]
iliyopo
Changamoto iliyopo ni kuongeza uzalishaji. [47]
imara
Lakini Maximo amesema kwamba kila timu ni nzuri, lakini baadhi ambazo ni imara zaidi na zenye rekodi nzuri zimekuwa zikilazimishwa kufanya vibaya na mazingira ya viwanja vya jijini Kampala na Jinja. [48]
ina
KILIMANJARO Stars ambayo imeitia hofu kubwa Uganda baada kucheza soka safi na kuifunga Zanzibar mabao 2-1, leo ina mtihani wa mwaka itakapoivaa Rwanda kwenye kombe la Chalenji. [49]
inakuwa
Jibu: Mipango ya kuhakikisha kuwa sekta ya utalii inakuwa muhimu katika maendelo ya nchi kiuchumi ni pamoja na kuona kuwa inatangazwa kwa nguvu zote. [50]
ipo
Prisons sasa ipo kwenye mikakati mizito kuhakikisha inafanya vizuri kwenye mechi ya awali ya kombe la Shirikisho ambapo imepangwa kuanza na timu ya Khalij Sert ya Libya hapo Februari Mosi. [51]
iwe
Tunaona ufisadi wa wengine na kutetea wa kwetu, lakini tulio wengi tulikubali kwamba hata kama ni kuonyeshana tako, na iwe hivyo hadi ushuzi utufanye sisi sote tuone aibu. [52]
iweze
Akizungumza na Mwananchi jana, Mkurugenzi wa Kituo hicho, Francis Kiwango alisema kwamba, ili serikali iweze kufanikiwa katika mchakato huo, ni vizuri vyombo vya dola, vikajipanga vilivyo kukusanya kura za maoni zitakazotolewa na wananchi, pindi utakapoanza. [53]
jamani
HAYA haya jamani. [54]
jengo
Hivyo hawa wanaoona kwamba jengo peke yake ni elimu wamepata nafasi ya tatu katika tuzo lakini ni tako tarajiwa tu kwa sababu wana siku chache za kujirekebisha. [55]
jua
Na kama hato jua basi hawezi kukuridhisha na kama hatokuridhisha jua hutofurahisha na kama hatofurahia basi mengine ndiyo haya yatokanayo. [56]
juu
Pamoja na uamuzi huo kutarajiwa kutangazwa katika muda usiozidi wiki mbili, Ewura ilitaka bei hizo zianze kutumika kuanzia Jumatatu iliyopita, lakini wauzaji wameendelea kuuza kjwa bei ya kati ya Sh1,450 na Sh1,600 kwa lita ya petroli na kati ya Sh1,300 na Sh1,500 kwa lita ya dizeli, huku wakiomba muda zaidi ili wamalizie shehena ambayo wanadai waliinunua kwa bei ya juu. [57]
karibu
Mamia kwa maelfu ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya mji wa Mwanga walikusanyika katika nyumba mbalimbali zilizo karibu katika kitongoji cha Ituri Ibwe Ijiwe kuwazika wananchi hao. [58]
kauli
Ana tatizo katika koo lake hali inayofanya ashindwe kutoa kauli vizuri," alisema. [59]
kazi
Binafsi sijaridhishwa na kitendo cha kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi kwa kosa la kazi ya kuchunguza na kueleza ukweli kwa wananchi," alisema Nooke, ambaye aliongozana na Balozi wa Ujerumani nchini, Guido Herz. [60]
kiasi
Kuna malalamiko mengi juu ya mita za kupimia mafuta katika vituo vya kuuzia mafuta, kiasi ambacho wakati mwingine mtu anauziwa mafuta pungufu kutokana na kuchezewa kwa mita. [61]
kibao
Wachezaji wangu wamekwatuliwa mara kibao, lakini haangalii anaangalia wenzetu tu,îalidai kocha huyo aliyekuwa akizungumza kwa hasira. [62]
kikuu
Mataifa yalionyesha kuwa yalitambua umuhimu wa mto Zambezi kama chanzo kikuu cha maji katika kanda na haja ya kuyahifadhi, kulinda na kutumia kwa uendelevu rasilimali maji ya bonde hilo. [63]
kile
Tatizo hapa ukiangalia ni viwanja, viwanja ni vibovu sana haswa hiki cha Nakivubo na kile cha Bugembe kule Jinja,îanasema Maximo ambaye timu yake inacheza leo na Rwanda. [64]
kina
Katika mchakato huo, jeshi la polisi linatakiwa kufanya uchunguzi wa kina kwa kushirikiana na wananchi ili wanapokusanya kura za maoni pasiwepo na kuchafuliana majina na pia kubambikiziana," alisema Kiwango. [65]
kisasa
Jibu: Tumeanza kuelekeza nguvu zetu katika kilimo cha kisasa, kilimo cha mapinduzi ya kijani. [66]
kuhakikisha
Akizungumuza na Mwananchi, Mwenyekiti Sputanza, Venance Mwamoto amesema kuwa wanaendelea na taratibu za kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa. [67]
kuhusu
Akifafanua kuhusu wa ujenzi wa kituo cha Msamvu, Mwambungu anasema kuwa mradi huo utajengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Serikali za Mitaa (LAPF). [68]
kumalizika
Mbali na mchezo huo Uganda, Somalia itacheza na Uganda majira ya saa 10.00 jioni baada ya kumalizika kwa mchezo wa Stars. [69]
kuonyesha
Alisema timu yake kwa upande wa Wasichana wameshindwa kuonyesha upinzani kwa kuwa wengi wao wanashindwa kuhudhuria vizuri mazoezini. [70]
kupitia
KUMEKUWA na mikakati mingi inayolenga kujinufaisha kiuchumi kupitia Mto Zambezi kwa nchi nane za Afrika ambazo unapita, ikiwemo Tanzania, lakini mikakati hiyo imekuwa haitekelezwi. [71]
kutafakari
Serikali inapaswa kutafakari upya sera za kuondoa umaskini kwa kutegemea Mkukuta na Mkurabita. [72]
kutafuta
Tunahitaji watu wanaoishi katika bonde ambao wanajitolea kutafuta ufumbuzi wa changamoto hizo," anasema. [73]
kutegemea
Nia yetu ni kutegemea chombo kama hicho katika kukuza na kuboresha kilimo. [74]
kutoa
Mazungumzo hayo yamekwama kwa muda huku msuluhishi huyo akieleza kuwa wawakilshi wa upande wa waasi wa CNDP hawana mamlaka kamili ya kutoa maamuzi. [75]
kuu
Kwa sasa Marekani ndiyo soko kuu la utalii wa Tanzania. [76]
kuwapa
Tunaweka mkazo katika kuwapa heshima watu wanaofanya kazi katika sekta hii ikiwa ni pamoja na kuwaongezea viwango vya mishahara ili wasiwe na tamaa ya kupokea 'kitu kidogo' kwa lengo la kujipatia utajiri kupitia njia ya ukusanyaji wa mapato ya serikali. [77]
kuzaa
Tunasikitika tu kwamba huu uchungu hauishii katika kuzaa jamii mpya inayoongozwa na viongozi waadilifu. [78]
kuzalisha
Katika kukabiliana na hali hii, tuna mpango wa kuzalisha mbolea hapa nchini. [79]
kuziba
Tumejitahidi sana katika kuziba mianya ya ukwepaji kodi. [80]
kwako
Watalii wanakuja kwako na unawapeleka Kilimanjaro. [81]
la
Wakati mkutano huo ukionekana kupooza, wajumbe watakuwa wakitikisa vichwa kwa masikitiko baada ya habari kuwa msafara wa mwenyekiti wa umoja huo mkoani Manyara umepata ajali katika eneo la Chenene, huku watatu watatu wakiwa wamejeruhiwa, akiwemo katibu muhtasi ambaye ametolewa jicho. [82]
lengo
Mwamoto amewataka wanachama wa Sputanza kushirikiana kwa lengo la kufanikisha mikakati mbalimbali ya chama hicho kwa ajili ya maendeleo ya wachezaji na soka wa Tanzania. [83]
licha
Zanzibar iliyoko kwenye kundi A la michuano ya Chalenji ina pointi nne licha ya kufungwa mabao 2-1 na Stars juzi kwenye uwanja wenye mabonde wa Nakivubo. [84]
lina
Tunataka kuifunga Rwanda na lazima tushinde kwa vile kama unavyoona sasa hii kundi letu lina mtihani mkubwa na halina mwenyewe. [85]
lipo
Hata hivyo, tatizo katika utekelezaji huu wa huduma muhimu za ugani, lipo katika kutoa elimu ya kilimo bora kwa mkulima. [86]
maana
Kikubwa tulichowaeleza CECAFA ni kuangalia kwa makini makosa yanayojitokeza katika mashindano haya na kuweza kuyarekebisha mapema ili kuleta maana halisi ya mashindano na hatimaye timu zilizo bora zaidi ya nyingine ndizo ziweze kuchukua ubingwa kwa haki bila kuwepo na malumbano yasiyo na msingi kwa timu pinzani,"Alisema Kaijage. [87]
madai
Ziara hiyo itaanzia Manispaa ya Kinondoni na baadaye Temeke kabla ya kumalizia wilayani Ilala na sasa imesababisha baadhi ya viongozi kutopatikana ofisini kwa madai kuwa wanakagua maeneo ambayo Waziri Mkuu atatembelea. [88]
madhara
Tatizo jingine linalokabili Bonde la Zambezi ni madhara ya mabadiliko ya hali nchi. [89]
magari
Baada ya mjadala mkali kutoka kwa washiriki, serikali na Watanzania walitakiwa kupunguza ununuzi na matumizi makubwa ya magari ya kifahari ili nishati inayoingia itumike katika sekta nyingine. [90]
magumu
Maisha yamezidi kuwa magumu na nadhani hata waajiri wetu hawaongezi mishahara kwa sababu wanajua tutajitafutia kwa hizi njia nyingine. [91]
mambo
Pamoja na kulipongeza gazeti hilo, kamishna huyo pia alitaka ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali yanayohusu gazeti hilo, uhusiano wake na serikali pamoja na masuala ya kisheria na haki za binadamu nchini. [92]
manane
Alisema halmsahuri hiyo kwa kuanzia itanunua matrekta ya kusukumwa na mkono manane na kuyasambaza kwa wakulima na mengi zaidi yataelekezwa katika maeneo yaliyo na uzalishaji wa mazao ya chakula kwa wingi zaidi. [93]
maneno
Sekta binafsi ni muhimu sana katika kukuza uchumi, bado serikali haijaonyesha mikakati bora ya kuendeleza sekta hii zaidi ya kutoa maneno matupu pia kutokuwa na sehemu bora yenye miundombinu na usalama wa kutosha ya kufanyia biashara (Kariakoo), na ucheleweshwaji wa kutoa makontena katika Bandari ya Dar es Salam ni vikwazo katika kukuza biashara na kuongeza pato la serikali. [94]
mashindano
Kocha huyo alisema katika mashindano haya timu anayoihofia zaidi ni Burundi kwa upande wa miaka 16 kwani wameonyesha mchezo wa kiwango cha juu zaidi. [95]
maslahi
Kinachotakiwa hivi sasa ni kuwa wazi kwa wananchi wako na uwaelezee kuwa utawaletea nini kama watakupa dhamana ya kuwaongoza na kuwawakilisha katika matatizo yao, na si kujigamba majukwaani na kutumia fursa hizo kuchafua wengine kwa mambo ambayo hayana maslahi kwa taifa hili. [96]
mawili
Katika mchezo huo uliochezwa juzi kulikuwepo na makosa mengi yaliyofanywa na wachezaji wa Zanzibar ambayo yaliachwa bila kuadhibiwa pamoja na mwamuzi kukataa mabao mawili ya Tanzania Bara. [97]
mazao
MBUNGE wa Jimbo la Ulanga Magharibi, Dk Juma Ngasongwa ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga kurejesha asilimia 20 ya fedha za ushuru wa mazao unaokusanywa kutoka kwa wakulima wa jimbo hilo. [98]
mbali
Wakati huo huo: Kaijage alisema kuwa TFF imetupilia mbali maombi ya timu ya soka ya Moro United ya kutaka kuhairishwa kwa mechi yake ya Ligi Kuu dhidi ya timu ya Azam ilipangwa kufanyika Januari 12 kutokana na timu hiyo kushiriki katika mashindano ya kombe la Mapinduzi yanayoendelea visiwani Zanzibar. [99]
mbaya
Katika taarifa ya maafisa hao iliyotolewa kwa BBC na kutiwa saini na Birigedia Jenerali Ntaganda, ambaye ni mnadhimu mkuu wa CNDP, ilieleza kuwa "uongozi na utawala mbaya" wa Nkunda umewafanya washindwe kutimiza malengo yao. [100]
mbele
Uongozi mpya umeahidi mbele ya wanachama wa CNDP, watu wa DRC na jumuiya ya kimataifa kuwa kuwa utaandaa mazingira mazuri ya kurejesha amani katika eneo la mashariki mwa DRC, kwa kusaidiana na jumuiya ya kimataifa na vikosi vya kulinda amani vya Monuc," alisema Desire. [101]
mbinu
Aidha katika mchezo wa kwanza dhidi ya Somalia, CECAFA imeelezwa kuwa kulikuwepo na mbinu za makusudi za ucheleweshaji wa muda uliokuwa ukifanywa na wachezaji wa timu ya Somalia na katika mazingira ya kawaida ilitegemewa muda huo ungefidiwa, lakini muda uliopotea unaonekena ni mwingi kuliko uliofidiwa. [102]
mdogo
KAMPENI za uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini zimezinduliwa rasmi kwa viongozi mbalimbali wa siasa kuanza kunadi sera zao jimboni humo. [103]
mgumu
Kocha wa Stars, Marcio Maximo alisema mchezo wa leo utakuwa ni mgumu, lakini atapanga kikosi cha mshangao kutokana aina ya mchezo. [104]
miji
Anasema kuwa katika maeneo ya Kilwa na miji mengine ya Tanzania tayari mamia ya ekari za ardhi zenye rutuba zimeshakuliwa na wawekezaji wa magharibi kwa ajili ya kuzalishia nafaka kwa mafuta. [105]
mikataba
Bodi ziliungana na kuwa na mikataba ambayo ilikuwa ikimnyonya mkulima kwa kununua mazao ya wakulima kwa bei ya chini. [106]
mikopo
Katika kukabiliana na hali hii, tuna mipango ya kuanzisha benki ya kilimo, benki ya uwekezaji ambayo itakopesha fedha katika utaratibu ambao urejeshaji wa mikopo utakuwa ni wa muda mrefu na pia viwango vyake vya riba vitakuwa ni vya chini. [107]
mimba
Kijumbe aliorodhesha baadhi ya vifaa vilivyokamatwa kwenye zahanati hiyo kuwa ni pamoja na Speculum, kifaa ambacho kinasadikiwa kutumika katika kuangalia sehemu za uzazi, UPT Sticks (19) zinazotumika katika upimaji wa mimba. [108]
mingine
Kilio cha wakulima katika mikoa hii na mingine ni mbolea. [109]
mita
Kwa upanda mwengine Masebu alisema baada ya kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kudhibiti ubora wa mafuta, mamlaka hiyo inafanya utaratibu wa kudhibiti mita za kupimia mafuta katika vituo vya mafuta ili kumfanya mnunuzi apate ujazo sahihi wa mafuta. [110]
mito
Anasema uharibifu wa mazingira umechangia kukauka kwa baadhi ya mito na mabwawa ambayo yamekuwa yakipeleka au kutoa maji kwenye mto huo mkubwa. [111]
mkakati
Jukwaa la mwaka huu lilikuwa na lengo la kubadili Usimamiaji wa Pamoja wa Rasilimali Maji (IWRM) na mkakati wa utekelezaji wa Bonde la Mto Zambezi kwa vitendo. [112]
mkazo
Pamoja na kipaumbele katika huduma za ugani, mkazo pia utawekwa katika kuboresha masoko ya mazao. [113]
moyo
Kocha Tanzania Majuto Majaliwa ameridhika na matokeo kwa kusema "kwa sasa vijana wanaonyesha moyo tofauti na tulivyoanza wengi wameshinda na kufikia hatua ya robo fainali. [114]
mto
Katibu Mkuu wa Umwagiliaji na Maendeleo Malawi, Andrina Mchiela, anatoa tahadhari kwa wadau wote wanaotumia maji ya mto huo kuwa na mikakati mizuri pia inayolenga kusimamia mazingira. [115]
mujibu
Kwa mujibu wa Tegambwage MwanaHalisi itakuwa mitaani rasmi kuanzia Januari 14 mwaka huu baada ya kumaliza siku zake 90 kifungoni. [116]
mwa
Hadi jana mchana, hakukuwepo na bango ya kampeni za wagombea mitaani, tofauti na ilivyokuwa wakati wa mkutano wa uchaguzi wa Umoja wa Vijana wa CCM mwishoni mwa mwaka jana. [117]
mwandishi
Claud Mshana ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi. [118]
mwema
Hata hivyo, mmoja wa wakaguzi alitonywa na msamaria mwema juu ya uhalifu ule uliokuwa ukifanywa katika akaunti ya EPA. Kwa hali hii, tuliamua kufanyika kwa ukaguzi na kugundua jinsi fedha hizo zilivyokuwa zikichotwa. [119]
mwishiwa
Lakini mwishiwa mmoja alisema. [120]
mzee
Hivi mnavyotuona hapa leo tuna shughuli ya Maulidi ya dua ya kumshukuru Mungu," alisema mzee huyo wakati waandishi wakiwasili nyumbani hapo. [121]
na
KINYANG'ANYIRO cha uenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM, ambacho kilitawaliwa na vijembe, tuhuma za kutumia fedha na kupakaziana, kinatarajiwa kuanza kumalizwa leo wakati mkutano mkuu wa jumuiya hiyo utakapofunguliwa na Mwenyekiti Jakaya Kikwete. [122]
nchi
Katika salamu za rambirambi, Profesa Maghembe alisema nchi sasa imefikishwa mahali lazima iseme hapana kwa ajali zinazotokana na uzembe akitaka ukaguzi maalumu wa leseni za madereva wa mabasi ya abiria. [123]
ndio
Lakini wakati maandalizi hayo yakiendelea, msafara wa Manyara ndio gumzo la wajumbe wa mkutano huo baada ya katibu wa UWT wa mkoa, na wenzake wawili kujeruhiwa katika ajali ya gari. [124]
ndoa
Imedaiwa kuwa baba yake aliyemzaa nje ya ndoa alimuuza kwa mama mmoja wa jijini Dar es Salaam kwa kiasi cha Sh70 milioni na gari moja. [125]
ni
Katika mitaa mbalimbali ambayo ni maarufu kwa kampeni (vijiwe) bado kulionekana kutokuwa na watu kabioa hali iliyowafanya baadhi ya wakazi wa mji huu waliozoea kuona mikutano kama hiyo kuanza kuwa na shaka kuwa huenda kuna jambo. [126]
nini
Fedha nyingi za makusanyo ya ushuru tunazozipata pale kivuko cha Mto Kilombero zinapatikana kutoka Ulanga magharibi, kwa nini halmashauri isiandae utaratibu wa kuwapongeza wakulima wanaozalisha mazao kwa wingi kila mwaka,” alihoji Dk Ngasongwa. [127]
nusu
Mwaka 2007 peke yake, watu wengi walikumbwa na mafuriko katika mataifa ya Botswana, Malawi, Msumbiji, Namibia, Zambia na Zimbabwe na kuathiri zaidi ya watu nusu milioni. [128]
nyinyi
Sijui kama nyinyi waishiwa ni wasomi au la. [129]
nyota
Mwambungu anasema pamoja na uendelezaji wa kituo cha mabasi, miradi mingine ya uboreshaji wa huduma za mji wa Morogoro ni pamoja na ujenzi wa hoteli ya kimataifa ya nyota tano, uwekaji wa taa za barabarani na ujenzi wa soko la kisasa katika eneo la Manzese mjini humo. [130]
nyuma
Kufuatia taarifa hizo, msemaji wa Jenerali Nkunda, aliyezungumza na BBC kwa njia ya simu, alikanusha na kusema kuwa kiongozi huyo wa waasi hajaondolewa madarakani na ataendelea kushikilia nafasi yake, huku nyuma yake ikisikika sauti inayodhaniwa kuwa ya Nkunda. [131]
nzuri
Hawa wachezaji hali yao si nzuri sana, lakini Yondani bado namuangalia kwa karibu,î alisema daktati Juma Sufiani. [132]
ombi
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Mafuta na Maji nchini (EWURA), imekataa ombi la wauza mafuta mafuta wa jijini Dar es Salaam la kutaka kuongezewa muda wa kuuza nishati hiyo kwa bei ya sasa kabla ya kuanza kutumia bei mpya zilizotangazwa na chombo hicho. [133]
pande
Tunaanda baadhi ya ada ambazo zitaboresha mazingira ya sekta ya madini kiasi cha kunufaisha pande zote. [134]
pato
Kutokana na mazingira bora ya asili ya utalii iliopo Tanzania, pato la utalii na ajira zitokanazo katika sekta hii ambazo zimefikia 200,000 ni ndogo na serikali inapaswa kuweka mikakati zaidi ili Watanzania wengi wapate kuajiriwa na mikakati zaidi inahitajika kuongeza pato la utalii. [135]
pembejeo
Kimsingi katika ukuaji wa kilimo msukumo zaidi utakuwa katika uboreshaji wa miundombinu inayoendana na kilimo cha kisasa, kuendeleza huduma za ushauri (ugani), kuboresha mifumo endelevu ya kilimo cha umwagiliaji, kuendeleza matumizi ya mbolea na aina nyingine za pembejeo. [136]
pia
Mkutano huo pia utachagua wajumbe wa Baraza Kuu la UWT na wawakilishi wa UWT katika vikao mbalimbali vya chama. [137]
pili
Maximo ambaye kikosi chake kilianza vibaya kwa kufungwa 1-0 na Somalia katika mchezo wa pili aliifunga Zanzibar 2-1 juzi kwenye uwanja wa Nakivubo. [138]
rais
Mwezi Desemba mwaka jana waasi hao walianza mazungumzo ya amani baina yao na serikali ya DRC wakiongozwa na msimamizi ambaye mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa (UN), rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo. [139]
ratiba
KLABU ya soka ya Simba imesema haiwezi kulazimishwa kurejea jijijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu kwa sababu ratiba za mechi zao wanazifahamu. [140]
riba
Jibu: Kwa kweli ni vigumu kukopa fedha kwa ajili ya kilimo wakati riba inayotozwa ni ya kibiashara. [141]
robo
HUKU Mashindano ya Tenisi ya Afrika Mashariki na kati yakiwa yanaendelea katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam wachezaji wa Watanzania wameendelea kufanya vizuri zaidi na kufanikiwa kucheza hatua ya robo fainali. [142]
saa
MJI wa Mwanga na vitongoji vyake juzi jioni ulizizima kutokana na vifo vya wananchi 11 waliofariki kwa ajali ya gari huku mazishi yao yakivunja rekodi kwa kufanyika kuanzia saa 1:00 jioni hadi saa 4:10 usiku. [143]
sawa
Gharama ya kila gari kuliendesha ni sawa na kuendesha kiwanda kidogo cha nafaka. [144]
sera
KITUO cha Sheria na Haki za binadamu (LHRC), kimeishauri Serikali kuweka sera itakayowabana Waganga wa kienyeji, pamoja na wafanyabiashara ambao ni wahusika wakuu wa mauaji ya albino, ili kuweza kurahisisha zoezi la kukusanya kura za maoni. [145]
shule
Sasa juzi mimi nilikuwa kijijini wakati matokeo ya shule za msingi yalipotangazwa. [146]
si
Alisema uhusiano wao na serikali si mzuri kutokana na vikwazo wanavyovipata kutoka kwa serikali na washirika wake. [147]
sifa
Kufanyika kwa zoezi hilo kutasaidia kuwabaini madereva wasio na sifa za kuwa madereva ambao wamekuwa wakibeba dhamana ya maisha ya abiria na kusababisha ajali zinazoua Watanzania wasio na hatia. [148]
siyo
Kwa kuwa na mbolea ya aina ya urea na ammoania na fosfeit siyo tu tutazalisha mbolea kwa matumizi ya nyumbani bali pia tutakuwa ndio wauzaji wakuu wa mbolea nje ya nchi. [149]
soko
SERIKALI sasa imedhamiria kusimamia bei za mafuta baada ya kuingilia kati utekelezaji wa agizo la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji nchini (Ewura), la kuwataka wauzaji wote wa nishati hiyo kushusha bei kulingana na viwango vilivyowekwa vinavyooana na bei ya sasa katika soko la dunia. [150]
sote
Tinoco ameletwa kwa ajili ya maendeleo ya soka la Tanzania, kwa hiyo katika kipindi hiki ambacho hana majukumu ni vizuri kama tutampata ili atuongezee nguvu kwenye benchi la ufundi,Prisons inabeba bendera ya taifa na tukifungwa ni aibu yetu sote," alisema Dk Chambuso. [151]
suala
Tunashukuru kwamba, serikali imeamua kuingilia kati suala hilo, ili kuonyesha kuwa imedhamiria kudhibiti mfumuko wa bei ya mafuta ambayo yana mchango mkubwa katika kukuza na kulinda uchumi wa taifa. [152]
tamaa
Mama mzazi wa binti huyo, Fatuma Sheshe alisema kuwa, siku alipomwona kijana wake huyo akiwasili nyumbani hapo mchana, alianguka na kupoteza fahamu kwa kuwa alishakata tamaa kuwa mwanaye ameuawa. [153]
tamko
Lakini mkurugenzi mkuu wa Ewura, Haruna Masebu aliiambia Mwananchi jana kuwa kabla ya tamko hilo la kushusha bei ya mafuta, walikutana na wafanyabiashara hao Desemba 30 Desemba mwaka jana na kukubaliana kuwa wapewe wiki moja kushusha bei hiyo. [154]
tatu
Kwenye ofisi za manispaa zote tatu za Dar es salaam, Mwananchi haikuweza kuwapata viongozi baada ya kuambiwa kuwa walikuwa kwenye ukaguzi. [155]
tena
Sakina alikataa kuzungumza na waandishi wa habari akihofia kuwa huenda anafanyiwa mpango wa kumpoteza tena kama alivyofanyiwa na baba yake mzazi huyo, huku akibubujikwa na machozi pamoja na ndugu wengine waliohudhuria katika kisomo hicho cha Maulid. [156]
tu
Sheria hiyo inadidimiza uhuru wa vyombo vya habari na kujieleza iwapo inampa waziri mamlaka ya kukifungia chombo cha habari kutokana na mtazamo wake tu. [157]
tulikuwa
Jana (juzi) tulikuwa na kikao pamoja na wafanyabiashara wa mafuta wakisema tuwaongeze muda zaidi kabla ya kushusha bei ya mafuta, lakini tumewakatalia,” alisema Masebu. [158]
tunaona
Sasa tunaona matunda ya ukuaji wa Pato la Taifa ambao unafikia dola za Marekani bilioni 20 kutoka bilioni 15 miaka iliyopita. [159]
tuzo
Lakini kwa kuwa sisi ni watu wa ukweli na uwazi, tumejiweka wenyewe ndani ya tuzo la tako. [160]
ugani
Dk Ngasongwa alipendekeza kuwa fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya kuwawezesha wakulima ni vema zikawaendeleza wakulima badala ya kupelekwa kwa maafisa ugani ambao wengi wao, hawawajibiki. [161]
ujao
Kamishna huyo alisema hayo baada ya kutembelea ofisi za gazeti hilo lililofungiwa mwishoni mwa mwaka jana kutokana na kuandika habari za harakati za maandalizi ya Uchaguzi Mkuu ujao ndani ya CCM, zikieleza kuwa kuna kundi ambalo linapanga kumng'oa Rais wa sasa, Jakaya Kikwete ili asigombee kwa tiketi ya chama hicho. [162]
ukuaji
Tulikuwa na ukuaji wa uchumi wa asilimia saba uliopatikana zaidi ya miaka 10 iliyopita, lakini Pato la Taifa (GDP) limeongezeka mara mbili. [163]
ule
Kitu cha kwanza ambacho kilifanywa na Rais Ali Hassan Mwinyi wakati ule, ilikuwa ni kuwaruhusu wananchi wote waliokuwa na fedha kuleta bidhaa waziuze katika maduka yao. [164]
umeanza
Kuhusu hoteli ya kimataifa yenye hadhi ya nyota tano, Mwambungu anasema kuwa mradi huo tayari umeanza na mwekezaji wake ni mtu binafsi. [165]
umuhimu
Kiwango kilichoonyeshwa na Stars katika mechi iliyopita pamoja na umuhimu wa mchezo wa leo kwa timu zote mbili vimewatia hofu Waganda ambao awali walishaibeza Stars ilipofungwa na Somalia ambayo mashabiki wengi wa hapa wanawaita wafanyabiashara wa mipakani. [166]
una
Mchezo huo wa Uganda na wenyewe una mvuto mkubwa kwa mashabiki, lakini nahodha Andy Mwesigwa amesema hawana mchecheto kwa vile kipigo cha Rwanda ilichotoa kwa Somalia watakifanya mara mbili. [167]
unaweza
Anafafanua kuwa maji, chakula na usalama wa nishati unaweza kufikiwa katika Bonde la Mto Zambezi, akielezea kuwa ni mto mkubwa zaidi katika SADC wenye rasilimali nyingi za maji na ardhi bora ambayo inahitaji kutumiwa ipasavyo. [168]
upo
Mvutano huo unaoonekana ni vita ya kuwania uongozi wa juu wa kundi hilo unaodaiwa kuwa huenda ukahatarisha zaidi hali ya usalama ya DRC kwa kuwa upo uwezekano wa kundi hilo kugawanyika na kuibuka kundi jingine la waasi. [169]
upya
Sasa tumeamua kujenga upya ushirika kwa kuwaelimisha wananchi kujiunga na kuunda vikundi vya ushirika. [170]
usafiri
Pamoja na hilo wanambongi hao waliishauri serikali kuwekeza zaidi katika usafiri wa umma badala ya ule wa binafsi ili kupunguza matumizi makubwa ya nishati katika sekta hiyo. [171]
ushauri
LICHA ya kumuongeza Mshindo Msolla kwenye benchi la ushauri wa mambo ya ufundi, timu ya soka ya Prisons sasa inampigia mahesabu kocha wa timu ya taifa ya vijana Mbrazili Marcus Tinoco ili kukiimarisha kikosi hicho kinachojiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho. [172]
uwazi
Akifungua kampeni hizo Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassani Mwinyi alitoa kauli ambayo kama wanasiasa wengine wataiga mfano wake basi ni wazi kuwa nchi yetu itaendelea kuwepo katika amani ya kudumu ambayo ni matunda ya uwazi na ukweli bila ya kuingiza itikadi na ushabiki wa vyama vyetu. [173]
vile
Tunaingia uwanja kucheza soka na tutatumia kikosi cha mshangao ili kupata pointi muhimu, kwa vile kama mlivyoona kwenye mchezo dhidi ya Zanzibar tumebadilika sana kiuchezaji,îalisema Maximo. [174]
viwanda
Mantiki kubwa ya ushauri wa wanambongi hao ni kuifanya nishati inayoingizwa nchini kutumika kwa wingi katika viwanda kwa ajili ya kuzalishia chakula kuliko usafirishaji. [175]
vya
Hakukuwepo na shamra shamra kama ilivyo kwa vikao vingine vya jumuiya za chama hicho tawala, wakati wajumbe wakiwasili mjini hapata tayari kuchagua viongozi wao wapya. [176]
vyake
Wiki kadhaa zilizopita Nkunda aliripotiwa kuwa katika eneo la Rutshuro kwenye mji wa Kivu Kaskazini akiongozana na batalioni moja ya vikosi vyake. [177]
vyanzo
Mchiela anasema kuna kuongezeka kwa mahitaji ya maji safi katika kanda hiyo inayotumia maji ya Zambezi, ambayo kwa sasa inatumia asilimia 50 ya maji safi kutoka kwenye vyanzo vyote. [178]
vyao
Mwinyi katika hotuba yake ya ufunguzi wa kampeni hizo kwa chama cha CCM jimboni humo alionekana tofauti sana na wanasiasa wengine ambao katika siku kama hizo huonekana katika sare za vyama vyao na kunadi vyama vyao kwa mbwembwe na majivuno yaliyopitiliza. [179]
wageni
Wasomi hao wanaishauri serikali kuwekeza zaidi kutoa ardhi kwa uzalishaji wa chakula badala ya kutoa ardhi kwa wageni kuzalishia nafaka kwa ajili ya uzalishaji wa nishati. [180]
wajomba
Badala yake sasa atawajibika kwa upande mmoja wa wajomba pekee na kutumia ubini wa wajomba. [181]
wako
Lakini ukija kuangalia unakuta kama ilivyokuwa Somalia wale wote wako nyuma ya mpira. [182]
wala
Sheshe alisema kuwa, baada ya binti huyo kurudi nyumbani walifikisha taarifa hiyo mahakamani, ambako waliafikiana kuwa baba mzazi wa binti huyo sasa hana mamlaka yoyote kwake na wala hatatumia ubini wake. [183]
walimu
Na siyo walimu tu. [184]
walio
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisa habari wa TFF, Florian Kaijage alisema kuwa baada ya kupokea barua hiyo TFF ilifutilia ili kufahamu wachezaji wa timu hiyo walio katika timu ya Zanzibar. [185]
wameleta
Watu wameleta mapendekezo yao. [186]
wana
Aidha, ulitaka kujua vikwazo wanavyopata kutoka serikalini na kama wana mpango wa kuanzisha gazeti la Kiingereza, mazuri ya serikali katika haki za binadamu na uandishi wa habari nchini na taratibu na sababu za kulifungia gazeti hilo. [187]
wapi
Licha ya kuwa wajumbe wengi kuwasili jana majira ya mchana kwa mabasi maalumu ya kukodi, bado katika viwanja vya CCM makao makuu kulionekana kutokuwa na watu wa kutosha huku baadhi ya wagombea wakiwa hawajulikani wapi wanafanyia harakati zao. [188]
wapo
Sina muda mrefu kwenye ligi, lakini nataka kuonyesha kuwa sikubahatisha kwenye Kombe la Tusker najua wapo makipa wengi wazuri, lakini lengo langu sasa ni kuwa kipa bora," alisema Kado aliyeibukia timu ya Mabibo United ya jijini. [189]
wawapo
Wananchi wa Tanzania ya sasa si wakubabaishwa na mbwembwe za kila aina za wanasiasa wawapo katika majukwaa na katika shughuli zao za siasa, bali wanachotaka ni kuona utekelezaji wa sera zinazonadiwa na vyama hivyo. [190]
wewe
Ni vizuri kuongea kutokana na tofauti zenu, na kujaribu kuzungumzia wenyewe mambo ambayo wewe unayo moyoni kuhusu mwenzio ili kwa wakati wake ajaribu kuchuja na kujifunza kukuridhisha. [191]
wilaya
Wanadai pia kuwa mbali ya tatizo hilo, jingine kwa mji wa Morogoro ni kutokuwa na hospitali ya wilaya kwa kuwa ya mkoa inazidiwa nguvu kutokana na kuchukua wagonjwa kutoka sehemu mbalimbali za mkoa huo. [192]
wote
Kama mwanasheria akisema utekelezaji uanzie Januari 5, tutaweza kuwafikisha sehemu husika wauzaji wote waliokaidi tamko hilo kuanzia siku hiyo," alisema Masebu. [193]
yana
UONGOZI wa Chama cha Wachezaji soka wa zamani Tanzania (Sputanza) umeiomba Wizara ya Mali Asili na Utalii pamoja na mashirika mbambali hapa nchini yana husika na utalii kuwatumia wachezaji wa soka katika kuutanagaza vivutio mbalimbali vya kitalii nchi. [194]
yao
Lakini alisema baada ya agizo hilo, juzi walijitokeza baadhi yao wakitaka wapewe muda wa mwezi mmoja kabla ya kushusha bei hiyo, lakini Ewura imewakatalia kwa sababu ni vitu vidogo ndio vinavyosababisha hali hiyo na kwamba haiwezekani mkakubaliana kila kitu kwa pamoja na kila mmoja akaridhia. [195]
yenu
Ndugu yenu kutoka pande hizi naomba niendelee kuwashukuru ninyi wasomaji wangu kwa hamasa na changamoto mnnazonipa. [196]
yenye
Mataifa hayo pia yaliahidi kuhakikisha kuwa matumizi ya usawa na yenye sababu na usimamiaji na uendelezwaji endelevu wa rasilimali ya maji katika bonde hilo. [197]
yeye
Huwezi kuwa na hali ambayo ni mtu mmoja tu anayewekeza ndiye anayelindwa, lakini yule ambaye anapoteza dhahabu yeye halindwi. [198]
zaidi
Mkitaka tutazungumza zaidi kesho," alisema Kahama. [199]
zenu
Zaidi nataka niwatakie mwaka mwema wenye baraka kwenu na kwa familia zenu, nataka pia niwakumbushe kuwa huu unaweza kuwa mwaka wa neema kwa watakao jishughulisha. [200]