Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-01-26

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aaah
Yaani niue albino ndio niwe tajiri, aaah hapana sitaki kuwa kwenye orodha ya wauaji, kama ni umaskini acha niwe, hata kama watu watasema nimeporomoka sawa tu,” alijisemea Kazim. [1]
aende
Kuna baadhi na wataalam kule alikokwenda kuhangaika walimshauri labda aende nje ya nchi. [2]
afe
Si bora afe tujue moja. [3]
aina
Baada ya kudai mafao yetu kwa zaidi ya miaka 30, mimi nimekuja na aina mpya ya kudai kwani pamoja na kujazana nje ya geti la Ikulu mara tano, serikali haikuwa tayari kukaa na kuzungumza nasi sasa hapo inafikiri utatumia njia gani zaidi ya kuishikiza kwa nguvu kama tunavyofanya hivi sasa. [4]
ajira
RAIS Jakaya Kikwete, amewataka viongozi nchini kuacha woga katika kusimamia na kutetea ajira wanazozistahili Watanzania. [5]
akawa
Kweli walifanya hivyo, wiki moja baadaye walirudi, Kazim akawa amekubali kwamba angependa kufanya biashara zote mbili yaani ya uvuvi na uchimbaji madini. [6]
akina
Sawasawa wakati akina Mkombozi wanasota kwa mguu. [7]
albino
Nyumbani kwake hapo alikuwa akiishi na watu kadhaa akiwemo jamaa mmoja ambaye ni mwenye ulemavu wa ngono yaani albino. [8]
aliingia
Kazimoto aliingia kuchukua nafasi ya Lucas Simon aliyeumia katika kipindi cha kwanza. [9]
ama
Katiba itakapobadilishwa itaruhusu rais kushitakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka akiwa madarakani ama baada ya kuondoka madarakani, kwa kuwa suala hili limeanza kipindi ambacho suala la rais Mkapa linapasua vichwa vya watu ni lazima Bunge likubali kubadili katiba ya nchi ili haki itendeke,"alisema. [10]
amani
Alisema watu walikuwa wamejiandaa, kwa amani, kupiga ili kuwachagua viongozi lakini mambo yamevurugwa na mikakati ya kuiba kura. [11]
ambae
Hali yetu si nzuri, lakini tutatumia kikamilifu mechi zote za uwanja wa Taifa kuhakikisha kwamba hatushuki daraja, hilo linawezekana,"alisema Mwaisabula ambae amekabidhiwa timu hiyo hivikaribuni ikiwa kwenye hatari. [12]
amewahi
Akizungumzia mchezo wa kesho kati yake na Simba Kilinda ambaye amewahi kuichezea Yanga miaka ya nyuma alisema kuwa hawaihofii kwa vile wanajua udhaifu wao. [13]
ana
Anasema kila mbunifu huwa ana malengo yake lakini ili kufikia malengo hayo zipo changamoto nyingi zinazowakabili, zikiwapo kukosekana kwa vifaa bora kwa ajili ya kufanyia shughuli zao mfano mashine na mitaji. [14]
au
Katika hatua nyingine aliwaonya wale wanaochezea mapinduzi na kwamba kama hawajitaki au hawajipendi basi wachezee mapinduzi, waone kama hawatashughulikiwa. [15]
aweze
Amesisitiza kuwa si kila ajira inahitaji Mtanzania kuwa na uwezo wa kuzungumza lugha ya iingereza, ili aweze kuajiriwa. [16]
bado
Nasema mwaka 2010 tutatesa hatuna sababu ya kushindwa, maendeleo yaliofikiwa ni makubwa ninafurahi kuwa tulioyaahidi tumeyatimiza na mengine tutayatekeleza bado tunaendelea,” alisema. [17]
baina
Alisema baada ya kuanza operesheni mpya za kudai mafao yao, hivi sasa kumekuwa na mazungumzo ya mara kwa mara baina yao na serikali, hatua ambayo isingepatikana kama wangeamua kufanya mambo kimya kimya. [18]
bali
Mikakati hiyo italenga kufafanua kwamba, CCM haifugi mafisadi na kwamba ufisadi sio wa kichama bali ni hulka ya mtu binafsi. [19]
bara
Shehia zote za Unguja zina maji na kwa upande wa vituo vya afya mtu hawezi kufika kilomita tano kabla hajakutana na kituo cha afya,hata mikoa ya Tanzania bara haijafikia maendeleo kama hayo. [20]
baya
Mambo ya usiku wanapolala wazazi hayazuiliki, na watoto hawa wanatabia moja ya kujifunza kila jambo liwe zuri au baya, ni jukumu letu sisi wazazi kuhakikisha hatutoi nafasi yoyote kwa watoto hawa kwani kosa moja dogo linaweza kuzaa goli litakaloweza kuharibu mwenendo mzima wa maisha ya watoto wetu. [21]
chake
Boaz alisema kuwa mama huyo alipowaambia kuwa hana fedha ndipo walipompiga na kitu chenye uzito kichwani na kusababisha kifo chake hapohapo, kisha kupora fedha yake ya mauzo ya shamba. [22]
chochote
Viongozi waliopita walikuwa hawajawahi kufikia hatua niliyofikia mimi hivi sasa, hao wanauzungumza hivyo ni hawaelewi chochote. [23]
es
Akizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam, kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohammed, alisema ameshawasilisha hoja binafsi kwa Spika wa Bunge, Samwel Sitta, kutaka katiba ifanyiwe mabadiliko ili rais apunguziwe madaraka na kuondolewa kinga ili ikiwazekana ashtakiwe hata baada ya kuapishwa. [24]
familia
Madhara haya tunayatengeneza wenyewe bila kujua na wakati mwingine kwa kujua, ingawa kwa familia zingine kunasababishwa na hali ya kipato—kwa maana ya kushindwa kuwa na nafasi ya kutosha katika nyumba ya kuwatenganisha wasichana na wavulana. [25]
fulani
Imekuwa kama ni kawaida kusikia kundi la wasanii fulani la muziki unaoitwa wa kizazi kipya limegawanyika. [26]
haina
Kwanza waziri mwenyewe ni albino, kama ataniambia mambo yasiyoeleweka, nitatuma watu tumuue viungo vyake tuvipeleke kwenye biashara, ambayo hadi sasa bado haina mafanikio licha ya kuua yule albino ambaye alikuwa msaidizi wangu wa karibu,” alijisemea. [27]
haja
Awali, Profesa Msolla alisema kutokana na mabadiliko, tekonolojia, na mifumo ya uzalishaji yanayoendelea duniani, kuna haja ya kuimarisha ,matumizi ya Tekonohama ili kushiriki kikamilifu katika ushindani unaosababishwa na utandawazi. [28]
halisi
Mpaka hivi sasa timu zinazoshiriki ligi ya mchezo wa kikapu mkoa wa Dar es Salaam Kili RBA hazijapatiwa vifaa pamoja na fedha, hali ambayo inazidi kuufanya mchezo huo kukosa mwelekeo na kupoteza maana halisi ya mchezo huo, kwa sababu ligi ya mkoa huo ndio kioo cha kikapu nchini. [29]
hao
Alisema anashangazwa na watu hao ambao wamekuwa wakitumia rasilimali za nchi zilizoletwa na CCM, kuendelea kubeza maendeleo yaliyofikiwa na Visiwa vya Unguja na Pemba. [30]
hapa
Hii hali siyo nzuri lakini nilichogundua hapa ni kutokuwepo kwa elimu ya kutosha ya uraia na kusabisha kuwepo kwa mapungufu kama haya ambapo ni hatari kubwa katika mchakato wa uchaguzi,"alisema. [31]
hapo
Dk Nyaoro katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana alisema kuwa wajibu wa UDASA ni kuhakikisha inafanya kila linalowezekana kusaidia kurudisha chuoni wanafunzi wote na kurudisha hali ya kawaida chuoni hapo. [32]
haraka
Kwa upande wake, Waziri Bihire alisema ujenzi wa reli hiyo, unatarajia kuanza haraka ili kuondoa tatizo la usafiri wa mizigo na abiria katika nchi za Tanzania, Rwanda na Burundi. [33]
hasa
Nimefanikiwa kukutana na wabunge hasa wale wa kambi ya upinzani wamekubali kuiunga mkono hoja yangu na sifikirii kama inaweza kupata upinzani hata kwa wabunge wengine,"alizidi kufafanua Hamad Rashid. [34]
hawa
Nilikuja na hawa vijana nikiwa na matumaini makubwa sana lakini bahati haikuwa yetu, nashukuru kwamba katika mechi zote ilizocheza ukimuuliza mtu kuhusiana na Burundi atakwambia ni timu tishio,"alijisifu Younde. [35]
hayo
Katika maeneo yenye sura ya kimji, wananchi wengi hawahakujitokeza kupiga kura na maeneo hayo ni pamoja na Mbalizi lililokuwa na takribani vituo 12, lakini watu waliojitokeza kupiga kura, wakiwa wachache. [36]
hicho
Pamoja na mambo mengine, alishuhudia kukosekana kwa orodha ya majina ya wapiga kura, katika kituo hicho na aliishutumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)kwa kushindwa kusimamia vizuri uchaguzi wa jimbo la hilo, uliofanyika jana. [37]
hii
Ni vema tukaelekeza vita hii ya ufisadi kwa wanachama ili waweze kuielewa sawasawa kwani, itasaidia kurudisha imani ya Chama,"alisema. [38]
hiki
Lengo letu ni kuwa na katiba itakayoweza kumpunguzia rais madaraka ili maamuzi yake yasiwe yake peke yake na hili litamhusu rais yeyote iliyeko madarakani kwa kipindi hiki, aliyeondoka na wote watakaofuata. [39]
hiyo
Alisema hali hiyo imemsikitisha kwa sababu inarudisha nyuma demokrasia nchini. [40]
hizi
Tunakumbuka tuliishazitakia timu hizi maandalizi mema kwa ajili ya michezo yao hiyo mikubwa ambayo watakuwa wanacheza nyumbani na ugenini, kwani wote tunaelewa ushindi wa timu hizi utakuwa ni furaha kwa Taifa. [41]
hizo
Alisema hatua ya nyaraka hizo kubebwa kiholela, inaweza kusababisha watu kutoaminiana. [42]
huko
Anasema kitu kingine kilichomsukuma kutumia vitu vya asili katika ubunifu ni katika harakati zake za kudumisha utamaduni wa muafrika ambaye huko nyuma wamekuwa wakitumia mavazi ya ngozi, magunia na magome ya miti. [43]
humo
Alisema katika kufanikisha hilo wameandaa semina elekezi kuhusu ufahamu wa EPA katika matawi yote 19 ya jimboni humo itakayokuwa ikielezea nini maana ya EPA na ufisadi kwa lengo la kukinusuru Chama. [44]
huo
Akizungumza kwenye hafla ya kuzindua mkakati huo, Katibu Mtendaji wa masuala ya jimbo kata ya hiyo Chikaka Robby alisema mkakati huo, unalenga kurudisha imani za wanachama wa ndani na nje kwa Chama chao. [45]
huu
Uongozi wa UDASA unapenda kuchukua fursa hii kuuelezea umma na wanafunzi wote kuwa hauna taarifa ya maandalizi ya huo mgomo na wala uongozi haujapokea pendekezo kama hilo au kulijadili katika kikao cha UDASA kilichofanyika tarehe 21 Januari Mwaka huu," aliongeza kusema. [46]
huwa
Mbali na ubunifu huo wa mtindo ya mavazi, mwanamke huyo anajishughulisha na biashara ya vitu vya asili ambavyo huwa anavipata kutoka katika nchi za Afrika Mashariki na Kati. [47]
huyu
Kwanza ya yote kuna vitu shostito vya kuangalia; huyu mtu anakuheshimu kiasi gani anakupenda kiasi gani na anakujali kiasi gani. [48]
ijayo
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Makamu Mkuu Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa Luhanga, alsema Kamati yake itatumia uwezo wake utakaoisaidia Wizara katika utendaji wake kwa ajili ya maendeleo ya Taifa na kwamba wiki ijayo watakaa kutafakari namna ya kutekeleza majukumu hayo. [49]
ikawa
Mfano zipo meseji watu wanatumiana "Vipi Dear!" unakuja, na hii ikawa ni meseji ya kawaida kabisa kwa mtu na mfanyakazi mwenzake kazini lakini kwako ikawa na sura nyingine tofauti kabisa na makusudiao yenyewe. [50]
ila
Chama hakijahusika hata kidogo katika jambo hili la ufisadi wa EPA, ila ufisadi ni hulka ya mtu mwenyewe, kwa hiyo si vizuri kukitwisha mzigo Chama," alisema. [51]
ile
Kama kiongozi hatakiwa kuzungumza maneno kama yale, kwa mfano siku ile tumekwenda kituo cha polisi Kati, Mlaki alizungumza maneno ya ajabu kiasi kwamba hata alivyokwenda kuonana na kamanda Kova alifokewa," alisema mmoja wa wastaafu hao. [52]
ilivyo
Ni suala lililo wazi kuwa maendeleo haya machache ya soka yametokana na wadau mbalimbali pamoja na serikali kuwekeza katika mchezo huo, ambapo awali kabla hata kocha Marcio Maximo hajaletwa na serikali kukinoa kikosi cha Stars hali ya mchezo huo haikuwa kama ilivyo hivi sasa. [53]
ina
Uelekeo ni mzuri sana ukiangalia timu ambayo ina wachezaji wadogo na iliyoonyesha mafanikio zaidi utabaini ni Burundi, angalia nchi nyingine zilivyoleta wakongwe. [54]
injili
CHESCO Kilemile ni mlemavu wa miguu ambaye aliyeamua kuhubiri injili kwa njia ya kuimba. [55]
ipo
Akirejea kauli yake aliyoitoa Kisiwani Pemba alisema ni kweli waliwamabia wananchi kwamba wakati umefika wa wapinzani kushirikiana na serikali kwa kuwa wabunge na wawakilishi hawana serikali na serikali ipo chini ya Rais Kikwete na Rais Karume. [56]
isiwe
Waziri Mkuu amesema tofauti za kisiasa na kiitikadi isiwe sababu ya kutofanya shughuli za maendeleo kwani ikitokea hivyo nchi haiwezi kwenda kwa mtindo huo na wanaoumia kwa kukosa maendeleo ni wananchi ambao ndio waliowaweka viongozi madarakani kwa kuwachagua na kuwaamini kuwa viongozi hao watawaletea maendeleo. [57]
iwapo
Alisema kuwa kumekuwepo na taarifa za kupotosha zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa chama chao kinafanya maandalizi ya kugoma iwapo uongozi wa chuo utapuuza maazimio ya kikao chao. [58]
japo
Sio kweli kuwa kumpekuwa ni kumdhibiti na si kweli kuwa wanaume hawapekuliwi, kwa kuwa japo wengine wanadai hawajali lakini najua japo kwa siri au kwa kujua au kutokujua wanapekua. [59]
jazba
BAADHI ya Wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wamemlaumu mwenyekiti wao, Nathaniel Mlaki kwa madai kuwa amekuwa akiongea maneno ya jazba yanayochangia kuchelewa kwa ulipaji wa mafao yao. [60]
jirani
Makoi alisema kuwa kwa kuanzia mpango huo utaelekezwa kwa baadhi ya shule zilizoko jirani na Klabu ya Gymkhana ya jijini Dar es Salaam. [61]
jukumu
Akizungumza mara baada ya kukabidhi misaada hiyo,mrembo huyo ambaye amerejea masomoni nchini Australia alisema kuwa ni jukumu la jamii nzima kuhakikisha kuwa linawajali na kuwalea watoto yatima kwani hawakupenda kuwa hivyo. [62]
juu
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) jimbo la Kawe kimevunja ukimya na kuanza mikakati ya kujisafisha kwa kutoa elimu ya ufahamu juu ya utata wa Akaunti ya malipo ya mdeni ya nje ( EPA) , kwa wanachama wake, ikiwa ni moja ya hatua za kukisaficha Chama. [63]
juzi
Wakati huo huo, Kaimu Kamanda huyo, juzi alitoa wito kwa wananchi wa Manispaa ya Arusha wa kata ya mjini Kati, kuwa makini katika kipindi cha uchaguzi wa diwani wa kata hiyo uliofanyika jana. [64]
kabisa
Furaha yangu ni kuona Tanzania inakuwa mbali kabisa na Ukimwi. [65]
kaka
Mzazi mmoja ameniambia jambo moja lililonisikitisha kuwa watoto wawili ndugu mtu na kaka yake mmoja mwenye umri wa miaka 12, na mwingine 13 wamepeana mimba bila wenyewe kujua, yule binti mwenye miaka 12 ameulizwa akasema yeye hajui lakini amekuwa akifanya mchezo huo na kaka yake. [66]
kanda
Tunaangalia mbele kufanya mambo makubwa zaidi, michuano hii ya chalenji imetusaidia sana kufikia malengo tuliyojiwekea ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezo wa vijana kwa kujipima na timu nyingine za kanda hii. [67]
kando
Pia Pinda katika ziara hiyo aliwakumbusha wananchi wa kisiwa hicho kuweka kando tofauti za kisiasa zilizopo kati ya Unguja na Pemba na kuwaeleza kwamba kamwe maendeleo hayawezi kupatikana visiwani Zanzibar iwapo kutakuwepo malumbano ya kiitikadi. [68]
kansa
Zaidi ya kuwa msaidizi wake, jamaa huyo albino, alikuwa ni mvumbuzi wa dawa kutibu kansa ya moyo, hata hivyo hakuwahi kumwambia Kazim. [69]
karibu
Kagera Sugar inayokwenda kwa kusuasua na ikifutiwa kwa karibu na Mtibwa na Simba ambayo imekuwa ni moto wa kuotea mbali katika raundi hii ya pili. [70]
kasi
MJADALA mzito unaolenga kumwondolea kinga Rais mstaafu Benjamin Mkapa, huenda ukashika kasi katika mkutano 14 wa Bunge unaoanza kesho ambao pamoja na mambo mengine utajadili masuala mazito yanayogusa ufisadi katika mkataba wa Richmond, uendeshaji wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) na urejeshwaji wa nyumba za serikali. [71]
kati
Katika vituo hivyo idadi ya watu waliotakiwa kupiga kura ilikuwa ni kati ya 300 na 350 lakini waliopiga kura walikuwa kati ya 10 na 40 na ilitarajiwa kuwa ambao wangejitokeza zaidi kupiga kura ni wa maeneo ya vijijini. [72]
kibao
Unafikiri wale waliokatika shule za ukata wanaweza kushindana na wale wanaotoa mamilioni kwa ajili ya shule ya wanafunzi wachache na walimu kibao, na kufanya tuisheni juu mpaka wanaweza kufaulu bila hata kuelewa kitu. [73]
kile
KATIKA kile kinachoonekana kukosa mwelekeo kwa wanamuziki wa hapa nchi hivi sasa kumekuwa na marumbano mingongano baina ya wasanii. [74]
kimataifa
Kocha wa Burundi, Gilbert Younde alisema kwamba anakiandaa kikosi cha kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ya miaka ijayo. [75]
kipya
Suala linaloumiza vichwa vya mashabiki na wadau wa muziki wa kizazi kipya inakatisha tamaa pia ni hali halisi ni kwamba kundi la TMK Wanaume Family limemeguka kwa mara ya pili na kusababisha kuzaliwa kundi jingine la tatu kutoka ubavuni mwake. [76]
kiume
Tunao wajibu wa kuwavutia wanafunzi wa kike na wa kiume wapende kusoma masomo ya sayansi na teknolojia. [77]
kocha
Ina aina Fulani ya wachezaji ambao ukiwa kocha wa timu pinzani inabidi ufanye kazi sana muda wote kwa vile hawachoki, wala hawakubali kushindwa kirahisi. [78]
kote
Duniani kote kabla ya kijana huyo albino kugundua hiyo dawa, ilikuwa inajulikana kuwa ukiwa na kansa ya moyo hakuna dawa ni kifo tu. [79]
kubuni
Malengo yangu ya baadaye ni kuwa mbunifu mwenye mafanikio makubwa kwa kubuni nguo zitakazoweza kushindana kwenye soko nje ya Afrika. [80]
kuelewa
Ni jambo lililo wazi kuwa asilimia kubwa ya wachezaji wa kikapu nchini ni wanafunzi ambao katika hali ya kujifunza wanakuwa wepesi kuelewa, Hivyo kama BD na TBF watajipanga vizuri na kuandaa mikakati ya kueleweka, ni wazi kuwa watapata wadhamini ambao watauendeleza mchezo huo. [81]
kufa
Wakati wanaendelea kuangalia ile picha aliingia daktari aliyekuwa akimwangalia Kazim na kumwomba waziri afupishe mazungumzo, badala yake wamsake yule mvumbuzi wa dawa kwani isingepita saa 12 kabla ya Kazim kufa ikiwa hatapata ile dawa. [82]
kuishi
Nyota hao walitoa mafunzo ya mchezo huo na kuwahamasisha vijana kuishi kwa kujiamini pamoja na kutambua afya zao. [83]
kuja
Mambo yote ya Bodi yanaweza kuja baadaye. [84]
kujua
Tatizo hilo lilijitokeza katika vituo vingi vya wapiga kura na kusababisha watu kurundikana vituoni huku wakishindwa kujua sehemu za kupigia kura zao. [85]
kule
Sisi kule bara tunataka kuiga hapa Zanzibar tunataka tuhakikishe kila kilomita tano kuna kituo cha afya. [86]
kumbe
Nilidhani nikija huku nitakuta watu wameshika mapanga na marungu ndio hali hii iliyojengeka huko kwetu bara kuwa watu wa Pemba hawasikilizani hawazikani lakini kumbe inawezekana kitu cha msingi ni dhamira ya kweli ya kuwaunganisha wazanzibari," alisema Waziri Mkuu. [87]
kumpa
Hamad Rashdi aliweka bayana kwamba kauli hiyo ya waziri mkuu pia ilizidi kumpa msukumo wa kuandaa hoja hiyo. [88]
kumuua
Ndio akaona ni bora awapigie simu wale jamaa zake na kuangalia ni namna gani wanaweza kumuua albino ili waendelee na biashara ile ya madini na uvuvi wa samaki. [89]
kundi
Nchi hiyo ambayo ilikuwa imepangwa kundi B ambalo mechi zake zilichezwa kwenye uwanja chakavu wa Bugembe mjini Jinja, ilikuwa ikionyesha soka la uelewano zaidi uwanjani na kuwatoa kijasho wazoefu. [90]
kuona
Rais Kikwete alisema katika ziara yake amepata kuona mambo mengi aliyokuwa ameyaahidi wakati wa kampeni zikiwemo kero za muungano. [91]
kuu
Meneja wa mradi huo mwalimu msaafu Daudi Hagai alisema kuwa shule hizo ziko katika tarafa ya Kinampanda na Kisiriri na lengo kuu la msada huo, ni kuunga mkono jitihada za kufufua michezo mashuleni. [92]
kuua
Aidha amewataka wanachama kuweka vizuri hesabu za mapato na matumizi bila ya hivyo wataweza kuua chama kwani pahala penye pesa pana shetani ambaye anaweza kuharibu mara moja mipango yote mizuri iliyokusidiwa kufanyika katika kuendeleza chama. [93]
kuuza
Hagai alisema kuwa hawatasita kuwachukulia hatua walimu wa shule watakaobainika kutofikisha mipira hiyo waliyopewa kwa madhumuni ya kuibua vipaji vya michezo kwa vijana waliopo katika shule zao na badala yake kwenda kuuza au kubadilisha matumizi yake. [94]
kwangu
Kama kuna vitu ambavyo vinanisumbua sana akilini kwangu ni tohara ya kike na watoto yatima, nitajitahidi kuhakikisha kuwa karibu na watu hawa na kuwasaidia pale ninapoweza,"alisema Michelle. [95]
kwani
Ni kweli nimeshapokea hoja tatu mpaka sasa lakini ni mapema sana kuzitaja kwani yawezekana kuna wengine bado watawasilisha hoja zao,"alisema Spika Sitta. [96]
kwao
Nawataka watu wajitokeze kupiga kura na kurudi nyumbani kwao, waache kukaa makundi na kuleta maneno ya uchochezi na vurugu, ili kuepuka matatizo" alisema Boaz. [97]
kwetu
Faida ya mahoteli haya katika Zanzibar ni kuwa soko kubwa la bidhaa zinazozalishwa ama kulimwa Zanzibar," alisema Rais Kikwete na kusisitiza "mwekezaji akinunua mchele unaolimwa kwetu wakulima wetu wanufaike. [98]
la
Katika tukio mojawapo mwanafunzi, Severine Gama wa shule ya msingi alikutwa akiwa mebeba sanduku la kupigia kura na alikuwa hana msimamizi wala polisi wakati akipeleka sanduki hilo katika kituo cha kupigia kura cha eneo la Mbalizi katika Kata ya Utengule Usongwe. [99]
labda
Mwanzo tulijua labda Juma Nature na wenzake ndio wakorofi kwa kuamua kujiengua kutoka kundi hilo na kuunda TMK Halisi. [100]
lake
MWANAMKE aliyetambuliwa kwa majina ya Lucia Saitobi(25) amefariki baada ya kupigwa na kitu kizito kichwani na hatimaye kuporwa zaidi ya Sh 2 milioni za mauzo ya shamba lake. [101]
lao
Ni dhahiri wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanasikilizwa hapa nchini na watu rika zote hivyo lazima waelewe wao ni kioo cha jamii, nguzo ya kujifunzia, wanatakiwa watambue jukumu lao ni kuburudisha, kuelimisha na kufahamisha jamii mambo ya msingi na siyo kubweteka na mambo yanayowayanya washindwe kuelewana. [102]
lazima
Alisema kama tume itakuwa na wafanyakazi wake, lazima watakuwa na woga katika kusimamia uchaguzi. [103]
leo
Mchezo wa leo unatazamiwa kuwa na ushindani mkubwa kwani Villa ya Kocha Kennedy Mwaisabula imepanga kuutumia kikamilifu uwanja wa Taifa kulinda heshima yake na kukwepa kushuka daraja. [104]
ligi
Mabingwa watetezi, Yanga ndio wanaoongoza msimamo kwa pointi 36 huku Villa ikishikilia nafasi ya pili toka mkiani mwa ligi kwa pointi 11 ikiwa imezidi pointi tano na Polisi Moro. [105]
mabao
Matokeo hayo yaliifanya ikumbane na Tanzania katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu ambako iliambulia kipigo cha mabao 2-1 huku Tanzania ikionekana kuzidiwa. [106]
macho
Hii ndio kazi moja iliyonifungua macho kuwa tunaweza tofauti zetu za kisiasa zikakaa kando na isiwe sababu ya kutofanya shughuli za maendeleo nchi nyingi tu zinashirikiana katika kuleta maendeleo katika nchi zao," alisema Waziri Mkuu. [107]
mahiri
Mafanikio hayo ni pamoja na ziara ya wachezaji mahiri wa Ligi ya kikapu nchini Marekani (NBA) Jennifer Azzi na Matt Bonner wanaotokea Klabu ya San Antonio Spurs. [108]
malezi
Kama nilivyogusia wiki iliyopita kuwa runinga zimeachiwa kwa kiasi kikubwa kuwa chombo cha kuwalea watoto, na kwamba malezi wanayoyapata watoto kupitia televisheni zao zimepelekea kuwaharibu kimaadili badala ya kuwajenga. [109]
mara
Ahadi yetu kubwa ilikuwa kufufua mazungumzo kwa viongozi wetu waziri mkuu na waziri kiongozi kukutana ili kuzungumzia kero za muungano na kwa hilo nadhani viongozi hao wameshakutana zaidi ya mara sita sasa kama kuna jambo hawajamaliza basi ni mimi na mheshimiwa Karume tutamaliza," alisema Rais Kikwete. [110]
masomo
Lengo letu ni kusaidia kurudisha hali ya chuo chetu kama kawaida ili kuwezesha wanachuo kuendelea na masomo yao na si vinginevyo," alisema. [111]
mbele
Wakizungumza kwa masharti ya kutotajwa majina, wastaafu hao walisema ingawa Mlaki ni kiongozi, lakini amekuwa akiongea maneno yasiyofaa hata mbele ya polisi, huku baadhi ya askari wakisikia jambo walilodai linaweza kusababiisha baadhi yao kukamatwa na kufunguliwa mashitaka. [112]
mbunifu
Huyu ni Fatma Amour, mbunifu mahiri wa mitindo hapa nchini. [113]
mema
Alisema masuala ya ufisadi na EPA yamepewa kipaumbele katika vyombo vya habari na kufukia mambo mema ambayo yamefanywa na Rais Jakaya Kikwete. [114]
mfupi
Baadhi ya wasomaji walionipigia simu na wengine kunitumia ujumbe mfupi wameniambia ni vyema nikawakumbusha wazazi juu ya madhara yanayosababishwa na kuwalaza watoto wa jinsia tofauti katika chumba kimoja. [115]
mgonjwa
Walipofika wakamzunguka na kuanza kumuhoji maswali mengi kwa hasira ili kujua kama ni kweli au alizungumza vile labda kwa sababu alikuwa mgonjwa sana. [116]
mguu
Mziba amezaliwa miaka 47 iliyopita mkoa wa Kigoma ambapo alinza kucheza soka akiwa shule ya msingi mwanzoni mwa miaka ya 70 na alisitaafu kucheza soka mwaka 1997 baada ya kusumbuliwa na matatizo ya goti la mguu wa kushoto ambalo aliumia mwaka 1989 katika mechi iliyo zikutanisha timu za Yanga na AFC Leopard ya Kenya iliyopigwa katika uwanja wa Shekh Amli Abed jijini Arusha. [117]
minne
Akizungumza mara baada ya kutiwa saini kwa makubaliano hayo, Dk Kawambwa alisema ujenzi wa reli hiyo unatarajia kuanza katika kipindi kisichozidi miaka minne kuanzia sasa. [118]
mipira
Mradi wa elimu kupitia michezo (Education Through Sports) umetoa msaada wa mipira 400 kwa shule za msingi 50 za wilaya ya Iramba mkoani Singida. [119]
miti
KWA kawaida amekuwa akibuni mavazi kwa kutumia magamba ya miti, ngozi, vipande vya magunia huku akinakshi kwa kutumia urembo wa asili. [120]
mke
Amesema CCM ni chama jeuri na kikubwa hivyo bila ya kuwa na ofisi inayoonekana ni sawa na baba mwenye mke aliyekosa kuwa na nyumba. [121]
mno
Chama kimetupwa, uongozi tulionao ni mbovu mno, udanganyifu umekuwa mkubwa kupita kiasi tumegeuzwa sawa na maburdoza, tunasafirisha watu wakishafika safari zao tunawashusha sisi tunaachwa njiani. [122]
mrefu
Kwa muda mrefu kumekuwepo na migogoro katika vyuo vikuu hapa nchini, migogoro ambayo imepelekea vyuo vingi kufungwa na baadhi ya wanafunzi kusimamaishwa masomo kutokana na kushiriki migomo hiyo. [123]
muda
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu Mwenyekiti wa UDASA, Dk Dalmas Nyaoro alisema kuwa kamati hizo ziliundwa katika kikao chao kilichofanyika mwezi Novemba mwaka jana lakini zimeomba kusogezewa muda ili kukamilisha uchunguzi wao. [124]
muhimu
Acha waendelee kuajiriwa, lakini ni jambo muhimu kwa watu wetu pia kunufaika na uwekezaji huu kwa maana ya kupata ajira. [125]
mumewe
Mkewe Kazim, hajui chochote kuhusu mumewe kuua albino; ni mwanamke ambaye anafanya kazi ofisi ya usalama wa taifa na zaidi ya yote anaijua vizuri sheria. [126]
mwa
Azimo lingine ni lile la kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu kunzishwa kwa Chombo cha Kusimamia Usalama na Ulinzi wa Anga - 2007. Pia Bunge litaridhia Itifaki kuhusu Maendeleo ya Jinsia ya Nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC). [127]
mzuri
Alisema wananchi wanatakiwa wapate ufahamu mzuri kuhusu suala la EPA na si vyama vingine kutumia mwanya huo kukichafua Chama. [128]
nami
Ndugu yangu nakupa pole sana, yaani ni bora ungewasiliana nami kabla ya kwenda huko, kwani ukweli ni kwamba dawa imegunduliwa nchini na jamaa mmoja tena ni albino, rudi wahi mapema usipoteze muda wako huko,” alimsisitizia. [129]
nani
Na baada ya kugoma, nani kafukuzwa sasa? Ni wananchi wakati wenyenchi wanazidi kupeta. [130]
nao
Alisema kama ambavyo Tanzania haizuii wageni kuajiriwa nchini, ni haki ya msingi pia kwa Watanzania nao kupata ajira kutokana na uwekezaji wa kigeni katika nchi yao. [131]
naye
Katika mtazamo wa kiume wenyewe wanasema inawezekana kumpenda mke wangu lakini nikamtamani Heriet lakini hili halina maana kuwa ni Heriet nataka kuwa naye, bali mke wangu. [132]
nayo
Simba ambayo nayo ina pointi 20, ina mabao machache ya kufunga. [133]
ndipo
Kutokana na majibu ya kijana huyo ambayo yaliyoonyesha kutowaridhisha viongozi wa CUF ndipo walipomchukua na kumpeleka kituo kidogo cha polisi kwa ajili kuendelea kuhojiwa na sanduku hilo lilirudishwa na kupelekwa katika kituo cha kupigia kura. [134]
ndoa
Anasema katika wimbo huo, ametumia mashairi kuwasihi kujilinda huku akiwahimiza kuvumilia mpaka watakapofunga ndoa. [135]
ngazi
Hiyo ni kutokana na mafanikio ya haraka ambayo yamekuwa yakionekana kwa timu hizo kila mwaka kuanzia ngazi ya klabu mpaka Taifa. [136]
ngumu
Ni vyema changamoto kama hizo zikafanyiwa kazi kwa kuwa utafutaji wa wataalamu wa mchezo huo si kazi ngumu ila ni suala la mipango ,kuzingatia na umakini tu. [137]
ni
Alipohojiwa ni wapi alikuwa anapeleka sanduku hilo, kijana huyo alisema yeye alipewa sanduku hilo na msimamizi wa uchaguzi ili alipeleke katika moja ya kituo cha kupigia kura katika eneo la Mbalizi. [138]
nia
Ni heri kufanya kazi hii kwa nia ya kumtumikia Mungu na si kuichukulia injili kama biashara, anayemtumikia Mungu hakati tamaa hata kama mambo yakimuwia magumu," anamaliza. [139]
nyingi
Alisema Mbali na safari hiyo pia kutakuwa na zawadi mbalimbali kama jezi za Stars, Pen na zawadi nyingine nyingi. [140]
ofisini
Msolla alisema hayo ofisini kwake jana, kabla ya uzinduzi wa Kamati ya ushauri wa masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo iliundwa hivi karibuni. [141]
papo
Waziri Mkuu alisema amepata uzoefu mkubwa akiwa bungeni katika kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo. [142]
pekee
Watoto hawa ambao hucheza na kuzungumza na kufundishana mambo yasiyofaa na wenzao wakati wa mchana, wanapokuwa wenyewe wakati wa usiku hujikuta wakipeana elimu zisizofaa kutokana na kuwa usiku ndio wakati pekee walioupata na ambao wanaweza kufanya mambo yao bila kipingamizi. [143]
pia
Msajili wa vyama vya Siasa, John Tendwa alisema alielezea kusikitishwa kwake na hatua ya masanduku kuhifadhiwa katika nyumba za watu na bila kujali kwamba ni nyaraka za serikali, ambazo pia hazikupaswa kubebwa kiholela na bila ulinzi. [144]
picha
Ikabidi kwa kumtia moyo, ikabidi aende kwenye ofisi ambayo alikuwa akifanyia utafiti huo na kufanikiwa kupata picha yake. [145]
redio
Tayari nyimbo za wimbaji huyo aliyejitoa maisha yake kuhubiri injili kwa njia hiyo zinatamba katika vituo mbalimbali vya redio nchini. [146]
reli
MAWAZIRI wa Muindombinu na Mawasiliano wa nchi za Tanzania, Rwanda na Burundi, wamesaini makubaliano ya ujenzi na upanuzi wa pamoja wa reli ya kati itakayoziunganisha nchi hizo. [147]
runinga
BAADA ya kuandika kuhusu runinga zinavyoharibu watoto, wapenzi wasomaji wa safu hii wamenikumbusha jambo lingine ambalo sikuwahi kuligusia kabisa. [148]
saa
Akizungumza waadishi wa habari katika kituo cha upigaji kura cha Mageuzi A na B baada ya kushuhudia, kukosekana kwa orodha ya majina ya wapiga kura katika kituo hicho huku watu wakiwa wamekusanyika kutoka saa 12 alfajiri, Lipumba alisema hali inasikitisha. [149]
safi
Tazameni nyini wenyewe sasa ni saa 3:15 ndiyo orodha inafikishwa hapa wakati Jaji Lewis Makame alisema mambo safi, lakini watu hawana nafasi ya kupiga kura kuchagua viongozi wanaowataka,"alisema Lipumba. [150]
saini
Makubaliano hayo yaliyotiwa saini juzi mjini Arusha, ni sehemu ya mpango wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki ya kuboresha sekta ya miundombinu katika eneo hili. [151]
sana
Hoja yangu inahusu madiliko ya katiba,katiba yetu sasa inampa rais mamlaka makubwa sana, sasa ili kumpunguzia mamlaka hayo inabidi katiba irekebishwe. [152]
sawa
Rais Kikwete alisema kuchezea mapinduzi ni sawa na kurejesha utumwa katika visiwa vya Zanzibar na kwamba wana CCM lazima wayalinde na kuyaenzi na kwamba hakuna yeyote atakayethubutu kuyachezea bila ya kuchukuliwa hatua. [153]
shaka
Tutaifunga Simba kama tulivyofanya kwenye mzunguko wa awali tunajua udhaifu wao na wala hatuna shaka," alisema Kilinda. [154]
sherehe
Mawaziri wengine waliohudhuria sherehe za kutiwa saini kwa makubaliano hayo ni, Waziri wa Miundombinu wa Zanzibar, Hassan Machano na Naibu Waziri Fedha wa Tanzania, Jeremiah Sumari. [155]
si
Tumekuwa tukiishauri tume ya uchaguzi iwe na watendaji wake ili wawajibishe pale wanapokesea, maana hili la kwaachia watu wa halmashauri na ma-DED ambao si wafanyakaziwa tume, linasababisha mambo kuvurugwa," alisema. [156]
sisi
Msafara wa mamba haukosi kuwa na Kenge, sisi tunaamini kuwa Chama chetu ni safi, ila tabia zetu zinatofautiana, ndiyo maana tunataka watu waache kukichafua Chama, lakini pia wanaokichafua Chama wawajibishwe. [157]
soka
Kocha wa Uganda, Bobby Williamson kabla hajakutana na timu hiyo aliwahi kusema kwamba anajua inacheza soka lakini haihofii kwa vile uwezo wake bado ni wa chini na wa kawaida sana. [158]
soko
Rais Kikwete alisema faida za uwekezaji ni pamoja na watu kupata ajira, serikali kulipwa kodi na wananchi wanaozunguka maeneo ya uwekezaji, kupata soko la bidhaa na huduma zao. [159]
tajiri
Huku akiendelea na kazi Kazim alikuwa ni mtu tajiri kwa muda mfupi mno. [160]
tatu
Alipoulizwa kama ameshapokea hoja hiyo binafsi kutoka kwa wabunge, Spika Sitta alikiri kupokea hoja tatu, lakini hakuzitaja akisema kwamba ni mapema sana kufanya hivyo. [161]
tena
Vyuo hivyo viliweka masharti kwa wanafunzi wote wa shahada ya kwanza kurejea tena cuoni hali ilyoleta mtafaruku wakati vyuo hivyo vilopofunguliwa tarehe 19 mwezi huu. [162]
tu
Hivi hata kutandika vitanda tunahitaji aletwe Mganda, Hivi kufyeka majani nako tunahitaji mtu ajue lugha ya Kiingereza, Hivi kumwagiliaji maji kwenye bustani kunahitaji mtu kuajiriwa kutoka Italia, Hivi kule China watu wanazungumza Kiingereza, Kinachohitajika ni kutandika kitanda tu siyo kuzungumza Kiingereza," alisema Rais. [163]
tuzo
Katika safari yake hiyo kifani amewahi kupata tuzo mbalimbali ikiwa ni matokeo ya kutambuliwa kwa mchango mkubwa wa kazi zake katika kuendeleza utamaduni wa Mwafrika. [164]
ujumbe
Nyota hao pia waliambatana na ujumbe mzito kutoka Chama cha Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) ukiongozwa na Mkurugenzi wa Shughuli za Mpira wa Kikapu wa Chama hicho, Brook Meek, Makamu wa Rais wa Uhusiano wa Jamii wa chama hicho, Todd Jacobson. [165]
ukata
Sasa Mkombozi akifanikiwa kuruka vikwazo vyote hivi, anapelekwa kwenye shule za ukata, shule za kukatisha tamaa moja kwa moja wakati akina Aimbora wanazidi kupeta ndani ya shule za wenyenchi. [166]
ukawa
Mchezo wa leo huenda ukawa wa nguvu zaidi kutokana na timu hizo kutaka kufufua matumaini baada ya kufanya vibaya kwenye mechi za awali za mzunguko wa pili na hakuna hata moja yenye matumaini ya ubingwa. [167]
ukocha
Anesema baada ya kumalizika kwa mkataba wake aliamua kuanza kusoma kozi mbalimbali za ukocha lakini pia akitafuta kazi nyingine tofauti na ukocha ili aweze kujikim kimaisha. [168]
ukoo
Ya nini kumpa matumaini wakati yeye na ukoo wake wote wameshatolewa nje katika dunia ya leo. [169]
umekutana
Umepekuwa umekutana na kitu umekiamini sivyo kwa kiherehere chako cha kusaka mambo. [170]
uwe
Mradi wowote wa uwekezaji ni lazima uwe na manufaa kwa jamii. [171]
uzoefu
Kamati hiyo pia, itafanya mawasiliano na Kamati nyingine za ushauri katika nchi za nje kwa lengo la kubadilishana uzoefu kwa mambo yanayohusu Teknohama, Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya maendeleo ya nchi. [172]
video
Safari yake ya uimbaji si ya muda mrefu kama ilivyo kwa wasanii wengi, yeye anasema alianza kuimba mwaka 2007-alianza kuimba nyimbo zake peke yake na kujikuta akiendelea na kufanikiwa kuikamilisha albamu ya video ambayo anatarajia kuizindua Machi mwaka huu. [173]
vijana
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Peter Msolla ameunda Kamati ya ushauri katika masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo pamoja na majukumu mengine itaishauri Serikali namna ya kuwavutia vijana wasome masomo ya sayansi. [174]
vile
Lakini unaweza kuisahau Burundi kwa vile imekuwa haivumi sana ingawa wachezaji wake wengi wana maumbo madogo na uwezo mkubwa. [175]
vipi
Huku sasa ni kuzinguana, kumbe hata mawaziri nao huwa wanakuwa wasanii, inawezekanaje niwasiliane na wewe nikiwa nje ya nchi uniambia yuko mvumbuzi wa dawa ya kuponya tatizo langu halafu sasa aniambie hajui atampata vipi, huu ni uhuni,” alijisemea Kazim akiwa mwenye hasira na kuwaza kuwa kama asingempa dawa hiyo angefanya mpango wa kumuua kwa sababu naye alikuwa albino. [176]
vitendo
Lakini wakati haya yakionekana kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku, tumejikuta tukiwalea watoto kwa kuwafundisha vitendo visivyofaa na baadaye tukijilaumu wenyewe, bila kujua kuwa sisi wazazi ndio chanzo cha madhara hayo. [177]
vya
Katika hatua nyingine ya kushangaza hadi kufikia jana, baadhi ya vituo vya kupigia kura havikuwa na majina yaliyokuwa yamebandikwa. [178]
vyao
Waishiwa walitingisha vichwa vyao kwa uchungu sana. [179]
vyuo
CHAMA cha Wahadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDASA), kimeunda kamati zitakazoshughulikia migogoro ya wanafunzi katika vyuo vikuu hapa nchini. [180]
wa
UCHAGUZI mdogo wa Mbeya Vijijini jana asubuhi ulianza kwa vituko baada ya kubainika kuwa baadhi ya masanduku ya kura yalihifadhiwa katika nyumba za watu, huku yakitutuswa kiholela kutoka sehemu moja kwenda nyingine huku vituo vingine vikichelewa kubadikwa majina ya wapiga kura. [181]
wadau
Pia itaishauri Wizara njia bora ya kuwashirikisha wadau katika utekelezaji wa programu za Wizara kuhusu Teknohama , sayansi na ubunifu",alisema. [182]
wako
Mzazi au mlezi, usuthubutu kumlaza mtoto wako wa kiume na ama dada yake wa kazi, au hata ndugu yeyote wa kike, kwani huko ndiko unakopeleka vishawishi na mafunzo yasiyofaa. [183]
wale
RAIS Jakaya Kikwete amewaita wale wote wenye kubeza maendeleo yalipatikana chini ya serikali mbili ya Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) walevi wa tende. [184]
walimu
Meneja huyo aliwataka walimu wa shule zote zilizopatiwa mipira hiyo kuiingiza kwenye daftari la kupokea na kutoa na mali za shule. [185]
wanafanya
Na kwa nini wanafanya vizuri. [186]
wanalala
Imezoeleka pia kwa familia nyingine, watoto wanalala katika chumba kimoja bila kujali jinsia zao. [187]
wapo
CHAMA cha Tenisi Tanzania(TTA) wapo mbioni kuanzisha mpango maalumu wa kufundisha mchezo huo katika ngazi za shule za msingi na sekondari kwenye mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Morogoro, Arusha, Dodoma, Mwanza na Kilimanjaro itahusika katika awamu ya kwanza. [188]
waume
Badala ya kumsaidia Rais kuwatumikia wananchi, wanadhani nafasi ambayo wanayo waume zao ya kuiongoza nchi ni kwa ajili ya kujinufaisha wao na ndugu zao. [189]
waziwazi
Mfano wa hali hii ni uchaguzi mkuu wa rais na wabunge wa Kenya mwaka jana ambako tukio la uvurugaji matokeo ya uchaguzi lilifanyika waziwazi na kulazimika Rais Mwai Kibaki kutangazwa mshindi huku sherehe za kumwapisha zikianza. [190]
wewe
Uzinga mkubwa, ondokeni hapa, mbona zamani tulikuwa tukipata fedha nyingi ndio kusema mlikuwa mnaua albino? Sitaki kusikia uchafu huu, wewe ukiuawa utajisikia raha?” alisema Kazim akionekana mwenye hasira. [191]
wiki
Kamati hizo mbili ambazo zinatarajiwa kukamilisha kazi zake ndani ya kipindi cha wiki tatu zitakuwa na majukumu ya kuchunguza chanzo cha migomo ya wanafunzi na pia kuchunguza njia za kugharamia elimu ya juu nchini. [192]
yake
Rais Kikwete aliyasema hayo jana katika Uwanja wa Demokrasia uliopo Kibanda Maiti katika Mkoa wa Mjini Magharibi, alipokuwa akihutubia umati mkubwa wa wananchi waliokwenda kusikiliza mkutano wa hadhara baada ya kumaliza ziara yake ya kutembelea mikoa mitatu ya Unguja. [193]
yako
Mwisho tu nikuachie mwenyewe na mizani yako. [194]
yao
Aliongeza kusema kuwa kamati hizo zitakapokamilisha kutekeleza majukumu yake katika muda waliopewa watawasilisha taarifa yao katika kikao cha UDASA ambapo itajadiliwa na mapendekezo yatapelekwa serikalini kupitia uongozi wa chuo unaogharamia kazi za kamati hizo. [195]
yuko
Bwana Jamhuri Mwananchi anafurahi kutangaza kwamba Bi Elimu Mkombozi hajafa bali yuko mahututi. [196]
yule
Akinunua mchicha uliolimwa pale Bumbwini yule mkulima wa Bumbwini amepata. [197]
zako
Unapompekuwa bila shaka unatafuta makosa! tuseme ukweli; hilo si jambo baya kufanya kama tayari hisia zako na ishara fulani zimeashiria kuwa huyu mtu lazima anakuwa anakutenda au kama huonyeshwi unapendwa. [198]
zangu
Ndoto zangu za kuendelea kucheza soka zilianza kutoweka mara baada ya kuumia mguu kwa sababu wangi wetu wakati huo tiliamini kuwa unapokuwa na matatizo ya goti huwezi kudumu katika soka. [199]
zipo
Ingawa tayari zipo taarifa kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kitawasilisha bungeni hoja binafsi inayolenga kuilazimisha serikali kuhakikisha hakuna mtoto atakayekosa fursa ya kusoma kwa sababu ya umasikini wa wazazi wake. [200]