Mtumiaji:Robert Ullmann/Mwananchi/2009-02-27

Ufafanuzi kutoka Wiktionary, kamusi iliyo huru

Mwananchi, Dar es Salaam, http://www.mwananchi.co.tz


aina
Mshtakiwa huyo, Saida Hassan, 18, ambaye ni mkazi wa Msasani, alifanya kioja hicho mbele ya Hakimu Anna Mshigwa baada ya kusimamishwa kizimbani na kudai kuwa hataki kusomewa mashtaka na aina yeyote ya hakimu wa kike. [1]
akawa
Anaweza akawa mjanja, (Mwizi smart) anaweza akawa anafuta namba zote zilizoingia na kutoka kabla ya kuingia kulala. [2]
akina
KATIKA kukabliana na tatizo la upungufu wa vifaa vya kujifungulia kwa akina mama wajawazito, kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom jana ilitoa vifaa vyenye thamani ya Sh40 milioni katika hospitali za serikali nchini. [3]
akitaka
Itakumbukwa Kocha wa Yanga, Dusan Kondic aliwahi kusimamisha mazoezi akitaka mashabiki wote kutoka nje ya Uwanja wa Uhuru. [4]
akitoa
Kitendo chake kiliwafanya watu waliokuwa wamekusanyika mahakamni hapo kwa ajili ya kusikiliza kesi ya ndugu yao, kushikwa na bumbuazi kutokana na vituko alivyokuwa akifanya mshtakiwa huyo pamoja na kutoa matusi ya nguoni aliyokuwa akitoa. [5]
akiwa
Alisema kuwa klabu yao ya wakuu wa wilaya Tanzania Bara inasikitika kumpoteza mtu muhimu sana kwani alikuwa mchapakazi mzuri na kwamba mambo aliyofanya wilayani Geita akiwa mkuu wa wilaya ni mfano wa kuigwa kwani alihamasisha wananchi kujenga shule nyingi za sekondari. [6]
akiwamo
Juhudi za Teddy hazikuzaa matunda kwa kuwa viongozi, mashabiki na waandishi wa habari akiwamo Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, NSSF, Dk. [7]
albino
MAUAJI ya walemavu wa ngozi (albino), hapa nchini hususan Mikoa ya Kanda ya Ziwa, yamegubikwa na imani za kishirikina. [8]
alijua
Yule Bwana alijua kuchapa. [9]
alitoa
Profesa Safari alitoa malalamiko hayo jana alipozungumza na Mwananchi kuhusu matokeo ya uchaguzi huo uliomrudisha madarakani Profesa Ibrahim Lipumba, aliyepata kura 646, huku mpinzani huyo akiambulia kura sita tu. [10]
ama
Ni vizuri kuitoa serikali kwenye aibu inayoweza kuipata kama ilivyotokea kwenye zabuni tata ya Richmond ambayo iliweka rekondi mbaya kwa watawala hadi kufikia mawaziri akiwamo aliyekuwa waziri mkuu kujiuzulu na watendaji wakuu wengine wa umma wanaodaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine wakishikizwa kujiuzulu ama kuondolewa. [11]
amani
Katika chaguzi zao kuna rushwa, kupigana, kuchafuana na makundi lakini kwetu kuna amani, utulivu na upendo baina ya wanachama na wagombea. [12]
ambako
Alienda moja kwa moja hadi kwenye hoteli ya Kilimanjaro Kempinski ambako alipata mapumziko mafupi kabla ya kwenda Ikulu kwa mazungumzo maalumu na Rais Jakaya Kikwete. [13]
ambazo
Alizitaja nchi ambazo alizielezea kama 'bahari za matumaini' ambazo zimeonyesha mifano na mafanikio makubwa kuwa ni pamoja na Tanzania, Malawi, Kenya na Uganda. [14]
ana
Ndugu zangu pamoja na Rais kumfukuza kazi Mnali wazazi katika wilaya ya Bukoba pamoja na Umma wa watanzania wanamuunga mkono na kumwona kama shujaa ambaye ana uchungu na taifa letu hasa katika sekta ya elimu,"alisema. [15]
ang
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema amepewa jukumu zito na uzito wake unatokana na chama dola kung’ang’ania madaraka hata kama hakitakiwi nchini. [16]
au
Thomas Kashililah alisema hakuna haja ya kamati kukutana kujadili suala hilo kwa kuwa bunge halina uwezo wa kuilazimisha au kuikataza serikali kufanya manunuzi kama inavyokuwa wakati ikinunua magari yake na vitu vingine. [17]
badala
Ni hatari kuacha kujadili mambo muhimu ya nchi yanayozingatia maslahi ya taifa, na badala yake kuendekeza hisia zisizo na mantiki,"alisema. [18]
bado
Kwa sasa bado tunaendelea kupokea maombi ya wakuu wa shule hizo wanaohitaji walimu na kuyafanyia kazi ili kumaliza tatizo hilo," alisema. [19]
baiskeli
Abiria waliojeruhiwa ni 7,719 na madereva 1,001. Waendesha baiskeli, pikipiki na mikokoteni waliokufa kutokana na ajali ni 860 huku wengine 4,279 wakijeruhiwa. [20]
bali
Alihadharisha dhidi ya mipango ya 'kujihami' inayofanywa na mataifa hayo tajiri ambayo inaonekana kuwa ni ya kulinda mataifa hayo, akisisitiza kwamba pamoja na kwamba mipango hiyo inaweza kuwa mizuri, lakini wakumbuke kuwa migogoro wanayokabiliana nayo si ya mataifa yao pekee bali ni ya dunia. [21]
bara
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa(UN) Ban Ki-moon mesema bara la Afrika linaweza kuwaondoa watu wake katika lindi la umasikini na ni imani potofu kwamba ni bara la giza. [22]
biashara
G27) unaotarajiwa kufanyika nchini Uingereza Aprili mwaka huu, Ki-moon alisema kuwa kuna hatari kuwa mataifa tajiri yakakwepa ahadi zao za misaada kwa mataifa masikini, hali ambayo pia itasababisha kufungwa kwa fursa za biashara katika mataifa hayo. [23]
bila
Kaluba alisema kuwa wanawake hao walipiga yowe kubwa kuomba msaada na bila kuchelewa wananchi walifika eneo la tukio na baada ya kuelezwa juu ya nia ya Ambilike, walimshambulia kwa vipigo hadi alipofariki. [24]
bungeni
Hata hivyo jana Waziri wa Nishati na Madini, William Ngereja alisema jana kuwa, mpango wa serikali kununua mitambo hiyo haihushi ufisadi wa aina yoyote kwa kuwa ulishapitia bungeni na kwamba, mitambo hiyo bado mipya na inauwezo wa kuzalisha umeme kwa kiwango kikubwa wakati wa dharura. [25]
calls
Subiri mpaka ajisahau, chukua simu yake wakati yeye hajui, nenda kwenye incomming calls, utainasa hiyo namba. [26]
cha
Ngeleja alisema kitendo cha watu kuhisi kuna kuna ufisadi katika mpango huo wa kununua mitambo hiyo, hakina mantiki, akisema kuwa serikali iko makini na haiwezi kukubali matokeo kama ya Richmond, ambayo ilipewa zabuni ya kufua umeme wa dharura kwa mazingira tata na kusababisha Bunge kuingilia kati na kufanya uchunguzi uliosababisha Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa uwaziri mkuu na baadaye kufuatiwa na mawaziri wawili. [27]
dhana
Kamanda Rwambow bila shaka alikuwa akielezea dhana ya polisi jamii katika mazingira ya utekelezaji wa vita dhidi ya mauaji ya albino na vikongwe, ambayo yamekuwa yakisumbua vichwa vya Watanzania na serikali kutokana na kuongezeka. [28]
endapo
Mziray alisema endapo timu ya Tanzania ingefanya mashambulizi kama ya Zambia ilikuwa na uhakika wa kushinda mechi yao dhidi ya Senegal iliyopigwa bao 1-0. Stars jana ilikuwa ikicheza na wenyeji Ivory Coast. [29]
enzi
Nakupa ubwana kwa shingo upande maana enzi zangu haikuwa hivyo. [30]
es
Ki-moon aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi mbalimbali jijini Dar es Salaam jana. [31]
ha
Ha ha ha. [32]
hadi
Utafiti uliofanywa katika Power System Master Plan (mpango wa kuendeleza sekta ya umeme) unaonyesha mahitaji ya umeme yanakua kwa wastani wa asilimia 10 hadi 15 kila mwaka katika kipindi cha kuanzia mwaka 2008 hadi 2012," alisema. [33]
hafanyi
Ndiyo! Bila kiboko mtu hafanyi kazi. [34]
haikuwa
Dowans ilirithi mkataba wa Richmond iliyobainika kuwa haikuwa na uwezo wa kuzalisha umeme huo wa dharura. [35]
haina
Kuhusu hali ya maambukizi mapya ya VVU na mipango wanayoichukua kupambana kupunguza, anasema kuwa baadhi ya mikoa haina maambukizi makubwa akitolea mfano wa mikoa ya kusini ya Mtwara, Lindi ambayo hata hivyo, anatahadharisha kuwa kutokana na kukamilika kwa Daraja la Mkapa, watu wengi wameanza kuhamia huko hivyo hali hii inaweza kusababisha kuongezeka kwa maambukizi. [36]
hana
Alipobanwa kueleza iwapo anafikiria kuwania tena nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama hicho, Profesa Safari alisema hawezi na hana nia ya kuwania uongozi wa chama hicho. [37]
hao
Wakizungumza mara baada ya kurejeshwa madarakani katika mkutano mkuu unaoendelea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini hapa, viongozi hao walisema hawataruhusu tena wizi wa kura. [38]
hapa
Sasa hapa, utaona kwamba uamuzi huu hauna msukumo wala mkono wa mafisadi," alisema. [39]
hapo
Eneo la tukio ni hapo nyumbani. [40]
haraka
Fungeni mazoezini tunataka kufunga uwanja tafadhari, haraka haraka,” alisema huku akionyesha kuwa na jazba. [41]
hasa
Viongozi wa dunia hasa wa kundi la mataifa tajiri manane duniani G8 ni lazima yahakikishe yanatimiza ahadi zake za misaada kwa mataifa masikini ili mataifa hayo yaweze kufikia malengo,"alisisitiza. [42]
hasira
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, Celina Kaluba alisema kuwa Ambilike aliuawa na wananchi wenye hasira kali juzi majira ya saa 11:00 jioni katika kitongoji cha Mbweko-kita Manyoni mjini. [43]
hata
Alisema, ameshakaa jela mara nyingi, kwa hiyo hana tena woga na yuko tayari hata kupoteza maisha kwa kulinda maslahi ya umma. [44]
hatua
Richmond ulibainika kuwa tata na serikali ilichukua hatua. [45]
hawa
Vijana wana vipaji na inawezekana kabisa kuzidi hawa wa huku magharibi,' alisema kocha huyo. [46]
hawana
Tukatae CCM kuchukua kura zetu kwa nguvu kwa kuwa wao hawana haki ya kutawala. [47]
hii
Angalia, ATC leo hii inaweza kununua au kukodi ndege lakini si lazima iwe mpya. [48]
hiki
Kwa mateso niliyoyapata kwa kukaa jela, kama ningekuwa muoga ningekwishakaa nje ya chama hiki,” alisema Machano. [49]
hili
Kwa Upande wa Tanzania alisema taifa hili limeonyesha mafanikio makubwa katika udahili wa wanafunzi katika shule, huku akiipongeza Malawi kwa kuonyesha mfano bora katika sekta ya kilimo. [50]
hivi
ALIYEPATA kuwa mfungwa, Ambilike Nassoro Maulidi, 32, mkazi wa Manyoni mjini Singida ambaye aliachiwa huru hivi karibuni kwa msamaha wa mpango wa paroli, ameuawa na wananchi kwa tuhuma ya kutaka kubaka wanawake waliokuwa wakilima shambani. [51]
hizi
Nia na utashi ndiyo moyo wa harakati zote hizi, lakini uwekezaji wa kifedha na utaalamu ni misingi wa mafanikio. [52]
hujuma
UAMUZI wa kikosi cha Taifa Stars kuamua kutokula chakula kwenye hoteli ya Golf ya mjini hapa ili kukwepa hujuma, kulizua tafrani kubwa baada ya askari Polisi aliyepewa dhamana ya kuwalinda kutaka kuwalazimisha kupanda kwenye basi kwa nguvu. [53]
huko
Wachezaji Stars walitoroka kimya kimya kutoka hoteli ya Golf ndani ya Taxi sita kwenda kula huko walikopangiwa, baada ya hapo walinzi hao walianza kuwasaka kila kona ya jiji na mwisho walifanikiwa kuwapata pale walipokuwa kitu ambacho kilimshangaza kila mmoja. [54]
huu
Alisema changamoto ni kwamba mipango iliyopo ya kuongeza uzalishaji haitaweza kuziba pengo kati ya uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme na mahitaji ya umeme yanayotarajiwa kati ya mwaka huu na mwaka kesho, baada ya miradi ya dharura kuondolewa. [55]
huwa
Sina uhakika sana lakini inawezekana majibu yakaja mapema hata kabla ya mwisho wa mashindano, kwa sasa huwa wanayasafirisha kwenda Tunisia na wakati mwingine Afrika Kusini,î alisema daktari. [56]
idadi
Akizungumzia matarajio ya baadaye, alisema watashirikiana na serikali kujenga vyumba vya madarasa, kukarabati vyumba vya kulaza wagonjwa hasa wazazi, na kuongeza idadi ya vifaa vinavyokidhi matakwa ya taaluma ya afya. [57]
ikawa
Walitaka kuanza kutumia nguvu na sisi tukagoma, ikawa mshike mshike, lakini mwisho jamaa wakakubali kufuatana na sisi. [58]
ikiwemo
Uzoefu unaonyesha kuwa iwapo wananchi walishirikishwa katika mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo suala la kupambana na vitendo vya uhalifu kutakuwa na mafanikio makubwa kama ilivyokuwa katika vita dhidi ya ujambazi. [59]
ila
Akizungumza na Mwananchi mjini hapa, Renarp alisema wachezaji wengi wanaotokea katika Ukanda wa mashariki na Kusini mwa mwa bara la Afrika wana uwezo mkubwa kisoka ila tatizo ni kuchelewa kuanza kwa mambo mengi ukiwamo msingi mzuri. [60]
ile
Mitambo ile unaweza kuifunga leo hii katika toroli na kuipeleka mkoa wowote wenye uhaba wa umeme. [61]
imekuwa
Pamoja na kuwa mwenyeji Ivory Coast imekuwa timu ya kwanza kung'oka kwenye mashindano ya CHAN baada ya kupokea vipigo viwili mfululizo kutoka kwa Zambia (3-0) katika mechi ya ufunguzi na Tanzania (1-0). [62]
ina
Walidai kuwa muuaji asingeweza kutoka nje ya eneo hilo kutokana na hali ya ulinzi ilivyo nyumbani kwa marehemu, ambayo ina mbwa wakali ambao hufanya majirani kutozoea kuingia ndani ya uzio huo. [63]
ipo
Nia ya serikali katika kufikia lengo hili haijaonekana na utashi ni mdogo, ipo haja ya kutadhimini ufikiaji wake na kujadili vikwazo mbalimbali vinavyochangia kukwama kwa mafanikio. [64]
juu
Matokeo ya uchunguzi wa kamati hiyo ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge Harrison Mwakyembe ulisababisha Lowassa kujiuzulu baada ya kutuhumiwa kuingilia mchakato wa zabuni na kushauriwa atumie busara kuamua juu ya ushiriki wake katika suala hilo. [65]
juzi
Ofisa mtendaji wa kijiji cha Nyiberekera, Tariani Gesura aliiambia Mwananchi kuwa mwili wa marehemu uligunduliwa juzi majira ya saa 4:00 asubuhi kwenye choo na mtu aliyemtaja kwa jina la Nyaruhembe Sabure(15) ambaye huchunga mifugo ya Nyibu. [66]
kabla
Hii inatokana na ukweli kwamba, ni vigumu kubuni mradi unaoweza kukamilika kabla ya mwaka 2009 kuisha," alisisitiza. [67]
kali
Wakati huohuo, Said Salim anaripoti kuwa viongozi wapya wa CUF, wametoa salamu kali kwa CCM, wakisema kuanzia sasa suala la kuibiwa kura zao katika chaguzi mbalimbali nchini, limekwisha. [68]
kanuni
Katika harakati za kupambana na ongezeko hilo, Kikosi cha Usalama Barabarani kimeandaa kanuni 21 za kudhibiti ajali na tayari baadhi zimeshaanza kutekelezwa na wamiliki wa mabasi. [69]
karibu
Unajua karibu timu nzima ilivurugika baada ya wachezaji zaidi ya wanane kupata timu Ulaya katika hatua ya mwisho kabisa. [70]
kasi
Ukiacha hayo, katika mchezo wa jana, wenyeji walianza kwa kasi na kuanza kushambulia mfululizo lango la wapinzani wao, lakini hata hivyo, ngome ya Stars chini ya Shadrack Nsajigwa, Salum Swed, Juma Jabu na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ walisimama imara kupunguza kasi ya mashambulizi. [71]
kata
Alisema, ajira za walimu hao zimetokana na ongezeko la shule za sekondari linatokana na ujenzi wa shule hizo katika kila kata. [72]
katibu
Hata hivyo, katibu wa Bunge, Dk. [73]
kauli
Alisema hilo linawafanya wanachama wanaoshindwa kulipa madeni yao, kushindwa kutimiza kauli yao ya kukopa kwa busara na kulipa kwa wakati na kuonya kuwa hali hiyo inaweza kuusambaratisha umoja huo. [74]
kiasi
Alisema kuwa Kenya imefanya vyema sana katika kukabiliana na magonjwa ya watoto kwa kuweza kuwakinga wakati jitihada za Uganda kukabiliana na maradhi ya Ukimwi zimeonyesha mafanikio makubwa kiasi cha kutofikiwa na taifa lolote barani Afrika. [75]
kichwa
Stars juzi iliibuka na ushindi wake wa kwanza wa mashindano ya CHAN kwa kuwachapa wenyeji Ivory Coast kwa bao 1-0 lililofungwa na Mrisho Ngassa kwa kichwa cha kuchupa. [76]
kimoja
Kwa mujibu wa mikakati hiyo, TRL itaanza kukata tiketi za safari kwa kutumia mtindo wa mtu mmoja kiti kimoja ili kuondoa msongamano wa abiria na wataanza kujali muda wa treni zake kuondoka. [77]
kisiasa
Hata hivyo, wanasiasa wengine wanaona kuwa uchaguzi huo wa viongozi wa CUF umeonyesha kukomaa kisiasa. [78]
kitabu
SIKU mbili baada ya kuangushwa vibaya katika kinyang'anyiro cha uenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Abdallah Safari amesema wajumbe wa mkutano mkuu walimdhalilisha na kwamba anaandaa kitabu kueleza udhalilishaji huo. [79]
kiume
MSHTAKIWA mmoja jana alifanya kioja katika Mahakama ya Mwanzo ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam baaada ya kukataa kusomewa shitaka linalomkabili la wizi na kutaka kusomewa shtaka lake na hakimu wa kiume. [80]
kombe
Si miezi mingi imepita tangu tulipofanya vizuri na kutwaa kombe tena nje ya ardhi ya nyumbani, tulifanya sherehe pamoja tena kwa raha ya juu. [81]
kondom
Wapenzi watakuwa tayari kufanya mapenzi kwa kutumia kondom, kwani kuwa waaminifu pekee haitasaidia, ni wajibu wapenzi kujua afya zao ili waweze kujilinda lakini kushawishika kutumia kondom kutafuata baada ya kujua afya zao kutokana na ushauri nasaha watakaoupata," anasema Nyanda. [82]
kote
Wengi wanaamini ukanda wa Mashariki na Kusini hawana uwezo mkubwa kama ilivyo kwa hawa wa Magharibi lakini mimi nimefundisha kote, nilikua Magharibi na sasa niko kusini hivyo ninaweza kuwa mtahimini mzuri wa mambo tena kwa uhakika,' alisema. [83]
kuanzisha
Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuanzisha kampeni ya upimaji wa Virusi vya Ukimwi (VVU), katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Julai 14, 2007, Watanzania wengi walijitokeza kupima ili kujua afya zao. [84]
kuboresha
Alisema lengo la kampuni hiyo ni kushirikiana na jamii katika kuboresha sekta muhimu kama afya, elimu na mazingira na kuwa kila mwaka wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali. [85]
kubwa
Tuangalie maeneo ya msingi, jambo kubwa ni watalaamu kuthibitisha ubora na uwezo wa kukidhi mahitaji ya nchi. [86]
kuelewa
Kujitokeza huko kwa wingi nchi nzima, ni wazi kuwa idadi ya maambukizi mapya itakuwa imepungua kwa kiasi kikubwa kwa sasa, kutokana na uamuzi wa kupima na watu kuonekana kuelewa kuhusu ugonjwa huu. [87]
kuiba
Ilielezwa mahakamani hapo na karani Immaculata Phillipo kuwa Said anadaiwa kuiba simu hiyo Februari 22 majira ya saa 12:00 jioni katika eneo la Msasani. [88]
kukopa
Akizungumza wakati akifungua mkutano mkuu wa tatu wa chama cha kuweka na kukopa cha Nyalikungu uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya hiyo, kapteni huyo mstaafu wa jeshi alisema kuwa Mnali ni shujaa ambaye alikuwa akiwatetea Watanzania licha ya kitendo chake kusababisha atimuliwe. [89]
kukosa
Wengi wa wachezaji wao wanaocheza Ulaya wamezaliwa na kukulia huko, tofauti na wachezaji kutoka Kusini na Mashariki mwa Afrika wanalazimika kwenda Ulaya tayari wakiwa wana umri mkubwa na wakati mwingine kukosa nafasi ya kucheza soka huko kutokana na historia kuwa hukumu. [90]
kula
Kamati maalum iliyo jijini hapa ilichukua uamuzi wa kuhakikisha Stars hawali chakula cha hotelini hapo na maandalizi yakafanyika kwenda kula mafichoni ili kuepuka hujuma hasa suala la kuwekewa 'vitu' mbalimbali kwenye chakula. [91]
kuona
Nimesema sitaki kuona hakimu wa kike ananisomea kesi yangu. [92]
kupigwa
Lakini baba, mnalalamika kupigwa viboko. [93]
kupimwa
Baada ya namba kujulikana ndio wanachukuliwa wachezaji wenye namba hizo mara tu baada ya mechi kwenda kupimwa ili kujua kama wanatumia dawa za kuongeza nguvu au la. [94]
kurejea
Hali kadhalika, atakwenda Arusha na kutembelea Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Halaiki (ICTR) na baadaye kurejea jijini Dar es Salaam. [95]
kwake
Lakini jana, Waziri Ngeleja aliiambia Mwananchi katika mahojiano ofisini kwake kuwa kununua mitambo hiyo hakutakuwa na chembechembe zozote za ufisadi ingawa wengi wanahisi hivyo. [96]
kwao
Alizungumzia Saccos hiyo, Kapteni Yamungu alisema ni vizuri kwa wanachama wa chama hicho kuiga mfano huo wa Mnali wa kutetea mambo yaliyo na manufaa kwao kwa ajili ya kuendeleza Saccos hiyo na hatimaye kuwa benki yenye lengo la kuwainua kiuchumi. [97]
kwetu
Mfano mzuri wa kukataa kwetu kuibiwa kura tutaonyesha katika uchaguzi mdogo wa uwakilishi katika jimbo la Magogoni Zanzibar. [98]
la
WAKATI Bunge la Jamhuri ya Muungano likiwa limenawa mikono katika mpango wa kununua mitambo ya kufua umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ameonyesha msimamo kutetea mpango huo, akisema si wa kifisadi. [99]
labda
Mke huyo amekuwa akisemwa lakini hajirekebishi labda ni kutokana na umri wake na huyo marehemu ambaye alizaa naye mtoto mmoja. [100]
lake
Wakati Profesa Safari akijieleza, wajumbe walikuwa wakimzomea na baadaye kumrushia maswali yaliyomtingisha, ikiwa ni pamoja na kutaka ataje jina la katibu wa tawi lake, swali ambalo alibabaika kulijibu. [101]
lao
Huu ni wakati mwafaka wa kujenga kikosi kipya cha Tanzania chenye wachezaji wenye nidhamu na uwezo wa kujitolea kwa ajili ya taifa lao. [102]
letu
Alisema kuwa mara baada ya Rais kutangaza uamuzi wake, wazazi wilayani Bukoba walimuona Mnali kuwa ni shujaa ambaye aliyekuwa na uchungu na taifa letu katika sekta ya elimu. [103]
lini
Bado hatujajua mechi inachezwa lini kwa kwa sababu mpaka sasa wapinzani wetu hawajatutumia barua ya kutujulisha ila tunadhani timu itaondoka hapa Machi 8 au 9 kwenda huko, alisema Madega. [104]
maana
Wajumbe wa mkutano mkuu wa CUF wamepotosha na kuharibu maana ya demokrasia ndani ya CUF na kutumia vibaya nafasi hiyo ya kuchagua viongozi. [105]
mabao
Matokeo hayo yamewaondosha kabisa wenyeji katika michuano hiyo, sasa watacheza na Senegal Jumamosi, mchezo wa kukamilisha ratiba katika mchezo wa kwanza walifungwa mabao 3-0 na Zambia. [106]
madereva
Katika ajali hizo, abiria 875 na madereva 152 walifariki dunia. [107]
madini
MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Kaskazini imeiamuru kampuni za The Guardian Limited na Printa Afrique Limited za Dar es Salaam kumlipa mfanyabiashara maarufu wa madini wa Arusha, Justin Nyari fidia ya Sh350 milioni kutokana na kumkashifu katika sakata la madini ya tanzanite. [108]
mapema
Mkewe huyo alikuwepo tena aliwahi mapema sana kufua, kitu ambacho ni tofauti na siku nyingine," alisema ofisa huyo. [109]
matako
WAISHIWA wenzangu, naomba mnisamehe maana niko kusini ya mbali ndiyo maana yawezekana nimepitwa na wakati lakini kama mtu anayethamini sana matako yangu yasiharibiwe na matakwa ya wengine, imebidi niwaletee barua na mijadala niliyoipata. [110]
mauaji
Kaluba alisema hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa akihusishwa na mauaji hayo na juhudi zinaendelea kuwanasa waliohusika. [111]
mbali
Jaji Sambo alisema mbali na fidia hiyo pia washitakiwa watatakiwa kulipa riba ya asilimia 12 ya fedha hizo kwa mwaka tangu siku ya hukumu hiyo kutolewa hadi siku ya malipo ya fidia hiyo. [112]
mbaya
Aliutumia mhadhara huo kuyakumbusha mataifa yaliyoendelea kuhusu hali mbaya iliyonayo Afrika ambayo inahitaji jitihada za ziada zitakazoliwezesha bara hilo kurejea katika mafanikio. [113]
mbovu
Sisi tunaunga mkono dhamira ya TRL kuwa ni njema na yenye malengo ya kuboresha usafiri wa treni ambao kwa muda mrefu umekuwa wa karaha kwa abiria kutokana na usimamizi mbovu na vitendo vya baadhi ya wafanyakazi wasiokuwa waaminifu ambao wamekuwa wanajaza abiria kupita kiasi kwa lengo la kujinufaisha wao badala ya shirika. [114]
mbuzi
Mfungwa huyo, ambaye aliachiwa huru Februari 5 mwaka huu, alikuwa akitumikia kifungo cha miaka mitano jela kwa kosa la kuiba mbuzi watatu. [115]
mchezaji
Hakuna nafasi ya majina, hakuna mchezaji nyota kwenye kikosi changu ambaye hana msaada basi tu anachaguliwa kwa kuwa jina lake linajulikana. [116]
mia
Uliziangalia hizo dalili ukawa na uhakika wa asilimia mia moja kuwa anakutenda. [117]
miaka
Meneja wa Vodacom Foundation, Isaya Mwakifulefule alisema kuwa kampuni hiyo imetoa vifaa hivyo katika kusherehekea miaka mitatu ya Vodakom Foundation nchini, ambacho ni kitengo cha kampuni hiyo kinachojihusisha na huduma kwa jamii. [118]
michezo
Caf limeamua kuchukua hatua hivyo ili kuongeza nguvu katika vita ya kupambana na dawa za kuongeza nguvu katika michezo, jambo linalopigwa vita kwa nguvu zote duniani na taasisi mbalimbali za michezo. [119]
miezi
Mdau mmoja ameiambia Mwananchi vipimo hivyo ambavyo husafirishwa nchini Tunisia kwa ajili ya vipimo huenda majibu yake yakatoka hata baada ya miezi miwili, lakini daktari wa Taifa Stars, Juma Sufiani ambaye huongozana na wachezaji hao kwa ajili ya kupimwa alisema, huenda majibu yakapatikana mapema zaidi. [120]
mimba
Maputo, Msumbiji kujadili na kusaini mkataba utakaotoa haki kwa wanawake ya kuwa na maamuzi binafsi katika masuala uzazi na utoaji mimba. [121]
mipira
Hata hivyo, Henry na Nizar walionekana kupwaya kwa vipindi hata kupoteza mipira mfululizo. [122]
mipya
Kuhusu gharama za kununua mitambo mipya kulinganisha na gharama za mitambo ya mitumba ya Dowans, Ngeleja alijibu: "Tuliwahi kupata mtaalamu akasema hii ya Dowans ni kati ya dola 58 hadi 60 milioni, wakati mipya ni kati ya dola 120 milioni. [123]
mke
Kati ya watu hao, ambao majina yao tumeyahifadhi, yumo mke wa marehemu anayedaiwa kushirikiana na hawara yake kumuua kikatili mumewe Moshi Nyibu. [124]
moyoni
Leo spendi kupoteza muda kuamkia hapa kwani niliyonayo ni mengi moyoni nataka niyatue hapa. [125]
mrefu
Majirani hao walidai kuwa uhusiano wa kijana huyo na mwanamke huyo ulianza muda mrefu kiasi kwamba ilifikia hatua ya mwanamke huyo kulala vyumba tofauti na mumewe. [126]
msj
Angalia msj yoyote ambayo huielewi chukua namba. [127]
muda
Alitoa maoni hayo muda mfupi baada ya kupata mapokezi makubwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere yaliyoambatana na gwaride pamoja na ngoma za jadi. [128]
mumeo
Unakumbuka nilitaja dalili ambazo zinaweza kukuhakikishia kuwa mumeo ana mwanamke nje. [129]
mwa
Alisema, licha ya ugumu huo, atahakikisha kuwa katika awamu hii wizi wa kura unakoma katika chaguzi nchini na wataanzia katika uchaguzi mdogo wa uwakilishi jimbo la Magogoni na ule wa serikali za mitaa mwishoni mwa mwaka huu. [130]
mwalimu
Lakini ukweli ni kwamba maandalizi hayakutosha na hivyo watoto walemavu na wengine walijazana madarasani (kufikia watoto 150 kwa mwalimu mmoja), na kukosa huduma wanazotakiwa kupata. [131]
namba
Katika hukumu hiyo ya kesi ya madai namba 35 ya mwaka 2001 iliyosomwa Jumatatu, Jaji Kakosulo Sambo aliiamuru The Guardian Limited, inayomiliki gazeti la Kiingereza la Financial Times na kampuni ya uchapishaji ya Printa Afrique Limited, kumlipa Nyari fidia hiyo baada ya kuridhika na ushahidi wa upande wa mlalamikaji. [132]
nao
Yamungu, ambaye pia ni katibu wa wakuu wa wilaya Tanzania Bara, alisema kuwa kitendo alichokifanya Mnali ni sawa na maamuzi aliyoyatoa Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuwa katika ziara yake ya mikoa ya kanda ya ziwa baada ya kukerwa na vitendo vya baadhi ya watu wanaowaua walemavu wa ngozi(Albino) na kutaka nao wauawe. [133]
naye
Inaonyesha jinsi wana CUF walivyo na imani naye. [134]
nayo
Hali mkataba wa Dowans ukiwa umeshaisha, kampuni hiyo imewasilisha mashtaka Mahakama ya Kimataifa ya Biashara dhidi ya Tanesco, ambayo nayo imeshikilia mitambo ya Dowans ikisema kuwa itatumika kama fidia iwapo shirika hilo la serikali litashinda kesi hiyo. [135]
ndio
Ndugu wajumbe uchaguzi wa Magogoni ndio utakuwa kipimo cha uchaguzi mkuu wa mwaka 2010... kama tutakuwa na uchaguzi au mapambano; kama uchaguzi au uchafuzi,” alisema Prof. [136]
ndoa
Baadhi ya majirani wa Nyibu walidai kuwa kijana huyo, mkazi wa Bunda eneo la Nyansura, amekuwa na mahusiano ya kipenzi na mwanamke huyo kiasi kwamba kumekuwa na kutokuelewana ndani ya ndoa. [137]
ndugu
Haya ya kuwa siogopi, ndugu wajumbe, yanathibitishwa na kugombea tena nafasi hii. [138]
ngazi
Lakini hali ya kuwalazimisha wachezaji kupanda kwenye basi hilo tayari ilionyesha kulikuwa na walakini na askari mmoja aliiambia Mwananchi kwamba ule ni utaratibu ingawa mmoja alikiri kwamba ilikuwa ni amri kutoka ngazi za juu zinazoshughulikia masuala ya usalama katika michuano ya CHAN ambao walitaka kuona lazima wachezaji wa Stars wapande basi hilo. [139]
ni
Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini ilishashauri kuwa serikali isinunue mitambo hiyo kutokana na kuwa imeshatumika, ikieleza kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria ya manunuzi ya umma, lakini serikali imeonekana kupitia mlango mwingine na kuwasilisha mpango huo kwenye kamati nyingine ya bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, ambayo iliomba kamati hizo zikutanishwe ili kutoa uamuzi kuhusu mpango huo. [140]
nia
Alisema kuwa kama Afrika itakuwa na nia thabiti na utashi wa kuondokana na umasikini , inaweza kufikia matarajio yake ingawa suala litakuwa ni muda. [141]
nini
Dk Kashililah alisema bunge halima mamlaka ya kuilazimiasha au kuikataza serikali kununua bali kazi yake ni kusimamia na kuhoji baada ya serikali kumua na kuongeza kuwa anashangaa ni kwa nini lishirikishwe sasa. [142]
nusu
Stars inahitaji kushinda mechi ya kesho dhidi ya Zambia kwa idaidi yoyote ili ipate nafasi ya kusonga hadi hatua ya nusu fainali huku Chipolopolo ikiwa inahitaji sare tu kupata nafasi ya kusonga mbele. [143]
nyota
Maximo alitoa kauli muda mfupi baada Stars kupambana hadi dakika ya mwisho na kuwashinda wenyeji Ivory Coast huku wachezaji kadhaa nyota wa kikosi hicho, Haruna Moshi 'Boban' na Athuman Idd ëChujií wakiwa jukwaani bila ya maelezo. [144]
nzuri
Akaongeza, 'Sasa ni nafasi nzuri kwa nchi za Mashariki na Kusini kuonyesha kwamba watahamini wa mambo wamekua wanakosea kwamba hata huko kuna ubora tena wa juu. [145]
pale
Ule ni uhuni hakuna kitu pale," alisema Profesa Safari. [146]
pia
Lakini pia Ki-moon alikuwa na ujumbe kwa Afrika na viongozi wake akisema kuwa bara hilo limechoshwa na migogoro isiyokwisha inayorudisha nyuma mafanikio na ufanisi. [147]
pili
Katika hatua nyingine, Makali alisema chaguo la pili la wanafunzi wa kidato cha kwanza mkoani Dar es Salaam, limekamilika na wanafunzi hao wanatajiwa kuanza shule Machi 15 mwaka huu. [148]
riba
Naye ofisa ushirika wa wilaya ya Maswa, Godfrey Mzava aliwataka viongozi wa chama hicho kufuata taratibu walizojiwekea katika ushirika wao na kwamba wasiogope kukopa ili waweze kukatwa riba, vinginevyo Saccos hiyo itakufa. [149]
saa
Katibu Mkuu huyo aliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jana saa 8:53 mchana na kulakiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe. [150]
safi
Mashabiki wa ivory Coast waliigeuka timu yao na kuanza kushangilia kwa nguvu wageni hao ambao walionyesha soka safi ya kujiamini na kuweza kuwabana wenyeji katika kila idara. [151]
sakata
Utata wa mitambo hiyo ya Dowans sasa unaendelea kama sakata la zabuni ya ufuaji umeme wa dharura lilivyoanza. [152]
sana
Nchi haiongozwi kwa hisia," alisema Ngeleja, ambaye alitetea sana mpango wa kununua mitambo hiyo wakati akiongea na waandishi kuhusu uamuzi wa serikali kukubaliana na ushauri wa kamati ya bunge wa kuzuia kununuliwa kwa mitambo hiyo. [153]
sasa
Kwa sasa mitambo hiyo inashikiliwa na Tanesco, ambalo linadai kuwa itatumika kama fidia iwapo shirika hilo litashinda kwenye kesi ambayo Dowans imefungua dhidi ya Tanesco kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara iliyo Paris, Ufaransa. [154]
sera
Lakini kutokana na mapungufu katika sera na sheria pamoja na utekelezaji mbovu, haki za watu wenye ulemavu zimekuwa zikipuuzwa. [155]
shuleni
Wasichana wengi wa Tanzania wamekuwa wakiacha au kuachishwa masomo kutokana na kupata mimba wakiwa shuleni, wengine wakiwa na umri mdogo na hivyo huwaletea matatizo wakati wa kujifungua. [156]
sisi
Wizi wa kura sasa basi; ikiwa wao ni wababe na sisi ni wababe vilevile; wakitunisha misuli na sisi tutatunisha. [157]
siyo
Mganga wa jadi mkoani Morogoro, Hamis Nguvumali anasema wale wanaotumia viungo vya binadamu ni wale wanaoshiriki uchawi na kamwe siyo waganga. [158]
soka
Lakini walikua hawajapata vitu vingi sana kwa ajili ya kujenga msingi mzuri wa soka, watu wa magharibi ya Afrika wana uhakika na mambo haya na pia kuwa karibu na Ulaya imewasaidia. [159]
tabia
Pia alikemea tabia ya baadhi ya wanachama ya kupenda kukopa, lakini wanashindwa kulipa kwa wakati, jambo ambalo alisema linawafanya wanachama wengine kushindwa kukopa. [160]
takwimu
Kwa mujibu wa takwimu hizo, mwaka 2008 Mkoa wa Dar es Salaam uliongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu waliofariki. [161]
tatu
MKUU wa wilaya ya Maswa, James Yamungu, amempongeza aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, Albert Mnali, akimwita kuwa ni shujaa kutokana na kitendo chake cha kuchapa viboko walimu wa shule tatu za msingi na kusababisha atimuliwe kazi na Rais Jakaya Kikwete. [162]
treni
JANA Shirika la Reli Tanzania (TRL) limetangaza dhamira ya kuboresha huduma kwa abiria kwamba itaongeza treni ya tatu kwenda Kigoma ikiwa na mabehewa 10 ya daraja la tatu itakayowezesha wasafiri kukaa tu. [163]
tu
Alipoulizwa kama kuna msukumo wowote kutoka kwa watu ambao walituhumiwa kuhusika katika mpango wa kuifanikisha Richmond kushinda zabuni ya ufuaji umeme wa dharura, Ngeleja alijibu: "Umeangalia maslahi ya taifa tu. [164]
ubovu
Mkurugenzi Mkuu Sumatra, Israel Sekirasa anasema kuwa asilimia 76 ya ajali za barabarani zinasababishwa na makosa ya kibinadamu huku asilimia 16 ikichangiwa na ubovu wa magari. [165]
ukawa
Ubora wa elimu ukawa shakani kwani suala si kuwaandikisha tu watoto shule, bali dhana ya uwekezaji, kwa maana wapate elimu inayayokidhi viwango vya ubora ili baadaye washiriki kikamilifu katika masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. [166]
umri
WATU watatu wakazi wa kitongoji cha madukani kijiji cha Nyiberekera kata ya Issenye wilayani Serengeti wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua kikatili mtu mmoja mwenye umri wa miaka 64 baada ya kumchinja na baadaye kutumbukiza mwili wake chooni. [167]
ustawi
Mapungufu haya ni pamoja na kukosekana kwa walimu wa kutosha kwa ajili ya watoto wenye ulemavu, shule na mazingira yanayofaa kwa watoto wenye ulemavu, vifaa vya kujifunzia na masuala yanayohusiana na ustawi wao kwa ujumla ili waweze kufaidi elimu, kwa mfano, huduma za afya. [168]
utawala
Alisema kuwa katika mataifa yanayoendeleza ufisadi, utawala bora ni changamoto kubwa ambazo zinatakiwa kuainishwa na akaisifu Tanzania kwa jitihada zake za kukabiliana na changamoto hizo. [169]
uzazi
Anasema baada ya kupima na kujua afya zao wapenzi watafaidika moja kwa moja kutokana na kujua namna ya kuendesha maisha yao wakiwa waathirika na pia elimu ya uzazi watakayopewa itawawezesha kuzuia maambukizi ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. [170]
vifo
Takwimu za polisi zinaonyesha kuwa albino 37 waliuawa hadi kufikia mwaka jana, Mkoa wa Mwanza ukiongoza kwa kuwa na mauaji 19, ukifuatiwa na Mikoa ya Shinyanga, Kigoma, na Mara ambayo kila mmoja uliripotiwa vifo vya walemavu hao wanne, Kagera waliuawa watatu na Mbeya mmoja. [171]
vijana
Wakati huo, Nyari alikuwa kamanda wa vijana wa CCM wilayani Simanjiro. [172]
vikao
Aidha aliwataka wanachama wake kushikamana kwa pamoja na kumaliza tofauti zao ndani ya vikao vya chama ili wakitoka wafanye kazi kwa ushirikiano na mshikamano. [173]
vipimo
Katika mechi ya kwanza Mrisho Ngassa na kiungo chipukizi Mwinyi Kazimoto walichukuliwa vipimo hivyo kwa mara ya kwanza. [174]
viti
Kanuni nyingine ngumu kwa wamiliki ni ile inayowataka kuwa na vinakili mwendo aina ya 'tachograph' na kuweka mikanda ya kufunga katika viti vya abiria. [175]
vituo
Maelezo hayo yametolewa wakati shirika hilo tayari limeanzisha safari za treni mbili kwenda mikoa ya Mwanza na Kigoma zinazosimama katika vituo vichache ukilinganisha na zamani. [176]
vya
Ngeleja alisema vipo vyombo vya serikali vinavyosimamia sheria na vinafanya kazi kwa umakini na akahoji: "Hivi watu hawaoni vigogo wanavyoburuzwa mahakamani, sasa watu wanafikiri serikali imelala, kwanini tuendeshe nchi kwa hisia. [177]
wakitoa
Alisema licha ya kuwa serikali na wadau mbalimbali wamekuwa wakitoa kipaumbele kwa akina mama wajawazito na watoto, bado serikali inapaswa kuweka mikakati mathubuti ili kuondokana na matatizo yanayowakumba. [178]
wala
Serikali haiwezi kuzembea wala kufumbia macho vitendo vya kifisadi. [179]
walio
Tumeamua kuanzisha mradi wa upimaji kwa watu walio wapenzi baada ya kupata fedha za kuuendesha nchi nzima. [180]
wameharibika
Watoto wameharibika kwa sababu walimu wameharibika. [181]
wanapiga
Na hasa kwa walimu! Wao wanapiga viboko kila siku kama mtoto hafanyi kazi. [182]
wanatakiwa
MASHABIKI wa Yanga wanaotaka kwenda Cairo, Misri kwa ajili ya kuishangilia timu hiyo wanatakiwa kulipa dola 800 Sh1.04 milioni. [183]
wangu
Mbali ya kuzindua kitabu changu, nitaamua shauri la kufanya pamoja na kesi ya uanachama wangu," alisema Profesa Safari. [184]
wao
Ki-moon aliahidi kuwa Umoja wa Mataifa utayaunga mkono mataifa hayo kuonyesha mfano na mafanikio ambayo yakitekelezwa hatua hizo kwa pamoja yanaweza kukabiliana na umasikini wa watu wao. [185]
wapi
Haya, wapi na wapi sasa? Hatimaye mtu wenu amegundua kwamba njia ya kutawala ni viboko. [186]
wapo
Yawezekana ni kutokana na mazoea na kuamini kuwa kwa kuwa wapo ndani ya ndoa au wamekuwa wakifanya mapenzi kwa muda mrefu basi wapo salama. [187]
washiriki
Kwanza, harakati za haki za binadamu zimeendelea kusisitiza upatikanaji wa haki za msingi kwa watu wenye ulemavu ili nao washiriki kikamilifu katika uzalishaji mali na fursa nyingine za kimaendeleo. [188]
wasi
Unaweza ukutane na namba ambayo ameisevu kwa jina la kiume, lakini ukawa na wasi wasi nayo, tafuta simu nyingine weka private namba kisha piga, sikiliza sauti inayopokea. [189]
wenu
Na tulifaidi ubwana hadi wengi wenu nao wakataka kuwa mabwana kama sisi. [190]
wote
KOCHA wa Taifa Stars ametoa kauli ya tahadhari kwa wachezaji wote ambao hawana msaada kwenye kikosi chake, wasiotaka ushirikiano na kujituma uwanjani atawaengua kwenye timu hiyo baada ya mashindano. [191]
yana
Malengo ya kubadili mfumo wa Polisi ya kiutendaji yana dhamira maridhawa ya kupunguza uhalifu katika jamii na kukiimarisha kisiwa cha amani kilichopo nchini. [192]
yao
Alisema kuwa mgogoro wa kiuchumi ulioikumba dunia, mabadiliko ya hali ya hewa, kutokuwapo uhakika wa chakula na vita kunaweza kurudisha nyuma mafanikio yaliyofikiwa na nchi moja moja katika malengo yao ya kufikia malengo ya milenia (MDGs). [193]
yetu
ALIYEKUWA kocha wa Taifa Stars, Syllersaid Mziray, amesema mfumo anaotumia kocha Mbrazil Marcio Maximo ni mgumu kutokana na uzoefu mdogo wa timu yetu ya Taifa. [194]
yeye
Inaelezwa uamuzi huo ulikuwa ni wa kocha wa Ivory Coast ambaye amekuwa akifanya mazoezi ya timu yake kuwa ni siri kubwa huku yeye akiwa anaongoza kuwa kocha anayetembelea mazoezi au mechi za timu za wenzake kama alivyofunga safari hadi Uganda wakati wa michuano ya Chalenji kuiona Stars na Zambia iliyombebesha mabao 3-0 kwenye mechi ya ufunguzi. [195]
yote
Pili, watoto wenye ulemavu ni kundi lililosahaulika katika makundi yote ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu, wamekuwa wakikosa fursa ya kujiendeleza kielimu na michezo. [196]
yule
Tena yule Bwana Padre alijua kazi yake. [197]
zaidi
Mifano hii inaonyesha kwamba Afrika inaweza kufanya vyema zaidi kama kuna utashi," alisema katika mhadhara wa wazi uliohudhuriwa na wanadiplomasia, mawaziri, wanataaluma, jumuiya ya wafanyabiashara na wananchi. [198]
zile
Akizungumza katika hoteli ya Golf jijini hapa, Maximo alisema atachukua uamuzi mkubwa wa kufanya mabadiliko katika kikosi chake baada ya mashindano haya na wachezaji watakaopata nafasi ni vijana na Watanzania wasahau tena zile tabia za majina kwa kuwa si yanayocheza. [199]
zote
Angalia wengine kama Kingi, kacheza kwa nguvu zote. [200]