Mtumiaji:Alex Rweyemamu
Mandhari
Alex Rweyemamu, ni mchangiaji wa kujitolea katika miradi ya Wikimedia hapa Tanzania. Nashiriki kikamilifu katika uhariri na maendeleo ya maudhui kwenye Wikipedia ya Kiswahili, WikiKamusi, Wikidata, Wikimedia Commons, na Meta-Wiki.
Ninaamini katika nguvu ya maarifa, na ndoto yangu ni kuona maarifa ya mtandaoni yanapatikana kwa lugha ya Kiswahili kwa kila mtu bila vizuizi vya lugha wala teknolojia. Kupitia uhariri wangu, nalenga kusaidia jamii kupata taarifa sahihi, zinazowezesha na kuelimisha.
Ninajihusisha pia na malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) hasa Lengo la 4: Elimu Bora, nikiamini kuwa elimu salama, jumuishi, na ya kidijitali ni haki ya msingi kwa kila mtu.